• ePaper
Saturday, November 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Burudani

AZAM YAZITOLEA MACHO WYDAD, NAIROBI UTD NA AS MANIEMA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 7, 2025
in Burudani, Kitaifa, Michezo
0
AZAM YAZITOLEA MACHO WYDAD, NAIROBI UTD NA AS MANIEMA
0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

UONGOZI wa klabu ya Azam FC umeweka wazi kuwa macho yote yapo katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Katika michuano hiyo, Azam imepangwa kundi B sambana na Wydad AC ya Morocco, Nairobi United ya Kenya na AS Maniema ya DR Congo.

Akizungumzia na UHURU jijini Dar es Salaam, kuelekea katika michuano hiyo, Mwenyekiti wa klabu hiyo, Nassor Idrisa ‘Father’ alisema Azam msimu huu imejipanga vizuri kufanya vyema katika michuano hiyo.

 “Unaona kwa sasa Azam ina mabadiliko makubwa na hata inavyocheza tofauti  na msimu uliopita, hiyo inaonesha ni jinsi gani tunahitaji ushindi na kufika mbali katika mashindano hayo na kuweka rekodi safi,” alisema.

‘Father’ alisema kundi ambalo wamepangwa ni gumu lakini hakuna kinachoshindikana.

“Hapa tunaendelea kujipanga vizuri kuhakikisha tunafanyia kazi upungufu uliotokea katika michezo iliyopita,”alisema.

Hata hivyo, Mwenyekiti huyo alisema kuwa wanajisikia furaha kubwa kufanya kazi na kocha wao, Florent Ibenge ambaye anazidi kukiweka vizuri kikosi chao.

Kabla ya Azam FC kuanza kucheza mechi hizo za kimataifa, itakuwa na mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara.

Azam itacheza  ugenini dhidi ya timu ya Namungo, mechi hiyo imepangwa kupigwa Jumapili katika Uwanja wa Majaliwa.

Previous Post

YANGA, SIMBA ZAANZA KUCHONGA 

Next Post

WANASIASA WAGUSIA USHINDI WA RAIS DK. SAMIA

Next Post
WANASIASA WAGUSIA USHINDI WA RAIS DK. SAMIA

WANASIASA WAGUSIA USHINDI WA RAIS DK. SAMIA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

KIBAIGWA IMEFUNIKA, OKTOBA WANATIKI KWA DK. SAMIA

KIBAIGWA IMEFUNIKA, OKTOBA WANATIKI KWA DK. SAMIA

3 months ago
DK. SAMIA : WANAWAKE TUNA UWEZO KUONGOZA

DK. SAMIA : WANAWAKE TUNA UWEZO KUONGOZA

1 month ago

Popular News

  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAAGIZO MATATU KWA DK. NCHEMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NI MARIDHIANO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.