• ePaper
Wednesday, March 18, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

MSAMAHA WA RAIS DK. SAMIA WAGUSA WAFUNGWA WAZEE, WENYE UJAUZITO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 10, 2025
in Habari, Kitaifa
0
MSAMAHA WA RAIS DK. SAMIA WAGUSA WAFUNGWA WAZEE, WENYE UJAUZITO

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan

0
SHARES
8
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ametoa msamaha kwa wafungwa 1,036, miongoni mwao 22 wameachiwa huru na 1,014 wamepunguziwa adhabu zao, watabaki gerezani na kuendelea kutumikia sehemu ya vifungo vilivyobaki.

Dk. Samia amefanya hivyo katika maadhimisho ya miaka 64 ya Uhuru wa Tanzania Bara na ametumia mamlaka aliyopewa chini ya Ibara ya 45 (1)(a) – (d) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977, kutoa msamaha kwa wafungwa kwa masharti.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani, George Simbachawene, msamaha huo wa Rais aliuotoa kwa wafungwa wote wenye sifa stahiki wapunguziwe moja ya sita (1/6) ya adhabu zao wanazozitumikia hivi sasa baada ya punguzo la kawaida la moja ya tatu (1/3), linalotolewa chini ya Kifungu cha 49(1) cha Shería ya Magereza Sura ya 58.

Taarifa hiyo ilisema wafungwa hao sharti wawe wamehukumiwa kifungo cha kuanzia miaka miwili na kuendelea, ambao wametumikia robo ya adhabu zao gerezani na wawe wameingia gerezani kabla ya Oktoba 15, 2025, isipokuwa wafungwa walioorodheshwa katika sharti la 2(i — xvi).

Sehemu ya taarifa hiyo ilisema wafungwa wenye magonjwa ya kudumu au sugu ambão wapo katika hatua ya mwisho, lazima wathibitishwe na jopo la waganga chini ya uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa/Mganga Mkuu wa Wilaya isipokuwa wafungwa hao wasiwe wametenda makosa yaliyoorodheshwa katika kipengele cha 2(i – xvi).

“Wafungwa wazee wenye umri wa miaka sabini au zaidi, umri huo uthibitishwe na jopo la waganga chini ya uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa/Mganga Mkuu wa Wilaya isipokuwa wafungwa hawa wasiwe wametenda makosa yaliyoorodheshwa katika kipengele cha 2(i – xvi).

“Wafungwa wa kike walioingia na ujauzito gerezani au wenye watoto wanaonyonya au wasionyonya waliohukumiwa kifungo cha mwaka mmoja na kuendelea, isipokuwa wafungwa hao wasiwe wametenda makosa yaliyoorodheshwa katika kipengele cha 2(i – xvi),”ilifafanua taarifa hiyo.

Taarifa iliongeza,  pia, wafungwa wenye ulemavu wa mwili na akili wasio na uwezo wa kufanya kazi, ulemavu huo uthibitishwe na jopo la waganga chini ya uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa/Mganga Mkuu wa Wilaya isipokuwa wafungwa hao wasiwe wametenda makosa yaliyoorodheshwa katika kipengele cha 2(i – xvi).

Ililiongeza pia, wafungwa waliohukumiwa adhabu ya kuwekwa kizuizini (Under President’s Pleasure) ambao wamekaa gerezani kuanzia miaka kumi zaidi.

WASIOHUSIKA

Aidha, msamaha huo hauwahusishi wafungwa wanaotumikia vifungo vya nje na wale waliowahi kukiuka masharti chini ya Sheria ya Bodi za Parole Sura ya 400 (R.E 2023) na kurudishwa gerezani kutumikia adhabu zao, Sheria ya Huduma kwa Jamii Sura ya 291 (R.E 2023) na Kanuni za Kifungo cha Nje.

Pia, msamaha huo hauwahusu wafungwa waliopatikana na hatia na kuhukumiwa kifungo gerezani kwa makosa ya uhujumu uchumi, matumizi mabaya ya madaraka, utakatishaji wa fedha, rushwa na usafirishaji au kujihusisha kwa namna yoyote ile na dawa za kulevya ikiwemo bangi.

“Wafungwa waliopatikana na hatia na kuhukumiwa kifungo gerezani kwa makosa ya kujamiana, utekaji au wizi wa watoto, kupoka, kuwapa mimba wanafunzi au makosa yoyote yale yanayohusiana na ukatili dhidi ya watoto na kujihusisha kwa namna yoyote ile na biashara haramu ya binadamu.

“Wafungwa waliopatikana na hatia na kuhukumiwa kifungo gerezani kwa makosa ya unyang’anyi, unyang’anyi wa kutumia nguvu, unyang’anyi wa kutumia silaha, kumiliki silaha, risasi, milipuko au kujaribu kutenda makosa hayo,”.

Pia, msamaha wa Rais hauwahusu wafungwa waliopatikana na hatia na kuhukumiwa kifungo gerezani kwa makosa ya kukutwa na viungo vya binadamu, wafungwa wanaotumikia kifungo gerezani kwa makosa ya kujihusisha kwa namna yoyote ile na nyara za Serikali au ujangili na wafungwa wanaotumikia kifungo gerezani kwa makosa ya wizi au ubadhilifu wa fedha za Serikali.

Msahamaha huo wa Rais pia hauwahusu wafungwa wanaotumikia vifungo gerezani kwa makosa ya kutoroka au kujaribu kutoroka chini ya ulinzi halali au kusaidia kutendeka kwa makosa hayo,  wafungwa wenye makosa ya kujaribu kuua, kujiua na kuua watoto wachanga.

Pia, msamaha huo hauwahusu wafungwa wenye makosa ya ugaidi, uharamia na makosa ya kimtandao, wafungwa wanaotumikia kifungo cha pili au warudiaji, wafungwa waliowahi kupata msamaha wa Rais  na wafungwa waliotenda makosa ya kinidhamu gerezani ambao makosa hayo hayajatimiza miaka mitatu mpaka kufikia Desemba 9, 2025.

Makosa mengine ambayo hayana msamaha wa Rais ni wafungwa wa madeni, wafungwa waliopatikana na hatia ya mauaji au kuhukumiwa adhabu ya kifo na wafungwa wanaotumikia kifungo cha maisha gerezani.

Taarifa hiyo Ilisisitiza kuwa, ni matarajio ya Serikali kuwa wafungwa walioachiliwa huru Desemba 9, mwaka huu, watarejea katika jamii kushirikiana na wananchi wenzao katika ujenzi wa Taifa na kwamba watajiepusha kutenda makosa ili wasirejee tena gerezani.

Previous Post

TASAF KIELELEZO CHA MAFANIKIO MIAKA 64 YA UHURU

Next Post

MKENDA AANIKA MAGEUZI MAKUBWA SEKTA YA ELIMU

Next Post
MKENDA AANIKA MAGEUZI MAKUBWA SEKTA YA ELIMU

MKENDA AANIKA MAGEUZI MAKUBWA SEKTA YA ELIMU

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MAFWELE NA WENZAKE 42 KUTOA USHAHIDI KESI YA KUGHUSHIVIBALI VYA KUMILIKI SILAHA

MAFWELE NA WENZAKE 42 KUTOA USHAHIDI KESI YA KUGHUSHIVIBALI VYA KUMILIKI SILAHA

1 day ago
MBETO : HAKUNA WA KUZUIA USHINDI WA CCM ZANZIBAR 2025-2030

MBETO : HAKUNA WA KUZUIA USHINDI WA CCM ZANZIBAR 2025-2030

7 months ago

Popular News

  • MANDONGA AJA KIVINGINE

    MANDONGA AJA KIVINGINE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YATUMIA BILIONI 64/- KUBORESHA UWANJA WA NDEGE IRINGA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU AWAWEKA MTEGONI VIGOGO WILAYA, HALMASHAURI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ALAMA TATU KUMUENZI JPM

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI KUIFANYA TANZANIA KITOVU CHA BIASHARA – DK. YONAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?