MANCHESTER, Uingereza
MECHI za marudiano za hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya zinatarajiwa kupigwa leo kwa michezo minne katika viwanja tofauti.
Katika michuano hiyo, Manchester City ya Uingereza itakuwa nyumbani kuchuana na Real Madrid ya Hispania katika Uwanja wa Etihad saa 5:00 usiku.
Man City itachuana na Madrid ikiwa na kumbukumbu ya kukubali kichapo cha mabao 3-0 katika mtanange wa kwanza uliopigwa Uwanja wa Santiago Bernabeu, Hispania.
Arsenal ya Uingereza ambayo awali ilitoka sare 1-1 leo itakuwa nyumbani kurudiana na Bayer Leverkusen ya Ujerumani katika Uwanja wa Emirates, London saa 5:00 usiku.
Chelsea ya Uingereza leo saa 5:00 usiku itakuwa nyumbani katika Uwanja wa Stamford Bridge kuchuana na PSG ya Ufaransa, ambapo katika mechi ya awali, Chelsea ilikubali kichapo cha mabao 5-2.
Mchezo wa mapema siku ya leo, utakuwa kati ya Sporting ya Ureno na Bodo Glimt ya Norway katika Uwanja wa Jose Alvalade saa 2:45 usiku.
Katika mtanange wa kwanza, Bodo Glimt iliibuka na ushindi wa mabao 3-0 nyumbani.




