• ePaper
Sunday, June 14, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

RAIS DK. SAMIA AWALILIA WATUMISHI WALIOFARIKI AJALI YA BOTI KIGOMA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
March 14, 2026
in Habari, Kitaifa
0
RAIS DK. SAMIA AWALILIA WATUMISHI WALIOFARIKI AJALI YA BOTI KIGOMA
0
SHARES
11
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na WAANDISHI WETU

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ametuma salamu za pole kwa Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Balozi Simon Sirro, kutokana na vifo vya watumishi wa afya saba waliofariki dunia baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kuzama Ziwa Tanganyika.

Vifo hivyo vilitokea Machi 14, 2026 asubuhi wakati watumishi hao wakienda kuhudumia wananchi wa Kata ya Kagunga Kijiji cha Kagunga.

Rais Dk. Samia alitoa salamu hizo jana kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa X zamani Twitter.

“Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya vifo vya ndugu zetu saba, watumishi wa afya mkoani Kigoma, waliofariki baada ya boti yao kuzama katika Ziwa Tanganyika leo (jana) asubuhi wakati wakielekea kutimiza majukumu yao ya kuwahudumia wananchi kwenye Kata ya Kagunga Kijiji cha Kagunga,” alieleza.

Aidha, Rais Dk. Samia aliwataka Watanzania kuungana kuwaombea kwa Mungu marehemu hao wapumzike kwa amani na awape uponyaji majeruhi wanaoendelea kupata matibabu.

“Ninatoa salamu za pole kwa Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Mheshimiwa Simon Sirro, familia za wafiwa, ndugu, jamaa, marafiki na Watanzania wote kwa msiba huu,” alisema.

Kwa upande wake Waziri wa Afya, Mohamed Mchengerwa alisema amepokea kwa masikitiko taarifa za vifo vya watumishi hao, huku akitoa pole kwa watumishi wote wa afya nchini.

Alisema watumishi wa afya wamekuwa wakifanya kazi kubwa ya kujitolea katika kuokoa maisha ya wananchi, wakati mwingine wakifika katika maeneo yasiyofika kirahisi.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Balozi Sirro, alitoa pole kwa uongozi wa Halmashauri ya Wilaya Kigoma na familia za waliopatwa na tukio hilo na kueleza serikali ipo tayari kutoa msaada utakaohitajika.

KAMANDA ZIMAMOTO

Aidha, Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa Kigoma, Michael Maganga alisema ajali hiyo ilitokea saa mbili asubuhi, jana katika Kijiji cha Kalalangabo, Manispaa ya Kigoma Ujiji.

Alisema waliothibitika kupoteza maisha miili yao imepatikana, japokuwa wengine watatu waliokuwa katika boti hiyo hawakuwa wamepatikana.

“Watu wengine tisa waliokuwa kwenye boti hiyo waliokolewa na wanapatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Kigoma, Maweni, juhudi za kutafuta miili ya watu watatu zinaendelea,” alisema.

Kamanda huyo alisema upepo mkali ulioanza asubuhi na kusababisha mawimbi makubwa ndiyo chanzo cha ajali hiyo.

MVUA YAUA WATU TISA SINGIDA

Wakati huo huo, watu tisa wakiwemo watoto saba wamefariki dunia mkoani Singida kufuatia mvua inayoendelea kunyesha nchini.

Athari nyingine ambazo zimejitokeza mkoani humo ni kuharibika miundombinu ya barabara na kubomoka madaraja mawili.

Kauli hiyo ilitolewa juzi na Mkuu wa Mkoa Singida, Halima Dendego alipozungumza na gazeti hili wakati akieleza hali ya mvua inayoendelea kunyesha mkoani humo.

“Tumepata vifo vya watoto saba na watu wazima wawili, tunamuomba Mungu awapumzishe watu wetu, tunaendelea kuchukua tahadhari kadri ya siku hadi siku.

“Athari nyingine tulizopata ni barabara nyingi zimeharibika na madaraja mawili yamepata hitilafu kubwa kwa ujumla na miundombinu imeharibika,” alisema.

Aidha, alisema serikali ya mkoa huo inaendelea kurabati miundombinu hiyo iliyoharibika kwa dharura na kuhakikisha inarudi katika hali yake ya awali.

Pia, alisema mkoa huo hupata mvua kuanzia Oktoba hadi Februari kila mwaka kwa wastani wa milimita 800, ambapo msimu huu mvua ilianza kunyesha Novemba mwishoni na kuendelea hadi Machi.

Akizungumzia hali ya mvua, Dendego alisema imepita kiwango kinachotarajiwa na kusababisha mafuriko katika baadhi ya maeneo.

Hivi karibuni Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), iliwataka wananchi kuchukua tahadhari kufuatia mvua inayoendelea kunyesha nchini kutokana kuunganika na mvua za masika na vuli.

IMEANDIKWA NA ZIANA BAKARI (DAR) NA FADHILI ABDALLAH (KIGOMA).

Previous Post

WATANZANIA SABA WAWASILI NCHINI KUTOKEA IRAN

Next Post

DK. MWIGULU AKERWA MICHANGO SHULENI

Next Post
DK. MWIGULU AKERWA MICHANGO SHULENI

DK. MWIGULU AKERWA MICHANGO SHULENI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

RAIS DK. SAMIA ABADILI MATUMIZI YA FEDHA

RAIS DK. SAMIA ABADILI MATUMIZI YA FEDHA

2 months ago
TANZANIA YANG’ARA MKUTANO MKUU WA KUPAMBANA NA RUSHWA JIJINI DOHA, QATAR

TANZANIA YANG’ARA MKUTANO MKUU WA KUPAMBANA NA RUSHWA JIJINI DOHA, QATAR

6 months ago

Popular News

  • RAIS DK. SAMIA ATAKA MIKOPO ISIWE MZIGO

    RAIS DK. SAMIA ATAKA MIKOPO ISIWE MZIGO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • AFRIKA KUCHOCHEA UTUNZAJI MAZINGIRA KUPITIA NISHATI SAFI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWAKINYO AOMBA RADHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA, SIMBA NI KIVINGINE ZAIDI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MEXICO YAANZA KWA KISHINDO WC, KADI ZATEMBEA HATARI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?