• ePaper
Monday, September 14, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

SIMBA HII GUSA UNASE CAFCL

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 14, 2026
in Burudani, Habari, Michezo
0
SIMBA HII GUSA UNASE CAFCL
0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

UNAWEZA kusema Simba hii gusa unase baada ya jana, kuitandika Mighty Wanderers ya Malawi kwa mabao 6-1.

Matokeo ya mchezo huo wa Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL), yameifanya Simba kutinga hatua inayofuata kwa ushindi wa jumla wa mabao 7-1.

Timu hizo za Simba na Mighty Wanderers zilishuka dimbani katika mchezo huo wa marudiano wa raundi ya awali, uliopigwa kuanzia saa 10:00 jioni katika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Wekundu wa Msimbazi katika mchezo wa kwanza, walishinda bao 1-0 wakiwa ugenini.

Katika pambano hilo la jana, Simba ilipata bao la kuongoza dakika ya saba ya mchezo kupitia kwa Clatous Chama  kwa shuti kali, Chama alimalizia pasi safi kutoka kwa Anicet Oura.

Kasi ya Simba iliongezeka katika dakika ya 26 ya mchezo huo, baada ya Libasse Gueye kupiga shuti kali na mpira kutinga wavuni, Gueye alipokea pasi  kutoka kwa Elie Mpanzu.

Bao la tatu la Simba, lilipachikwa wavuni na Chama katika dakika ya 33 baada ya kupokea mpira kutoka kwa Oura.

Dakika ya 69, Gueye alifunga bao la nne huku bao la tano lilipachikwa wavuni dakika ya 88 na Keletso Makgalwa.

Makgwala alimalizia pasi kutoka kwa Ismail Mgunda ambaye aliingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Gueye.

Bao la sita, lilipachikwa wavuni na Morice Abraham aliyeingia dakika ya 62 ya mchezo akichukua nafasi ya Chama ambapo alipiga shuti kali lililotinga wavuni.

Kufuatia ushindi huo, Simba itakutana na timu ya FC 15 de Agosto de Akonibe ya Guinea ya Ikweta.

Timu hiyo ya Guinea Ikweta ilifanikiwa kutinga hatua nyingine baada ya kuitoa Fomboni FC ya Comoros katika raundi ya pili ya mchujo.

Awali, pambano hilo, lilianza kwa kasi huku timu zote zikishambuliana kwa zamu  ambapo dakika ya tatu ya mchezo, Mpanzu alikosa bao baada ya kupiga shuti kali na kipa wa Mighty Wanderers, Dalitso Phiri aliokoa.

Mighty Wanderers walijibu ambapo dakika ya nne, Lameck Mithi alipiga shuti kali na mpira  ulitoka nje ya lango.

Mighty Wanderers walipata bao la kwanza katika mchezo huo kwa njia ya mkwaju wa penalti,dakika ya 44 iliyopigwa na Isaac Kaliati.

Wanderers walipata mkwaju huo wa penalti baada ya Ismael Toure wa Simba kumfanyia madhambi, nyota wa Wanderers, Clement Nyondo katika eneo la hatari.

Kipindi cha pili, ilianza kwa kutafuta matokeo ambapo dakika ya  dakika ya 50,Chama alikosa bao baada ya kupiga shuti kali na kipa ,Phiri aliokoa mpira huo.

Mighty Wanderers katika dakika ya 57, walifanya shambulizi kupitia kwa  Thierry Sama ambaye alifumua shuti lililookolewa,kipa Mahamadou Kassali.

Msimu uliopita, Simba iliishia hatua ya makundi ya michuano hiyo ikipangwa na timu za Petro de Luanda, Stade Malien na Esperance de Tunis.

Mara ya mwisho Simba kucheza hatua ya nusu fainali ya CAFCL (zamani Klabu Bingwa Afrika), ilikuwa mwaka 1974.

Wakati huo huo, timu ya Singida Black Stars imesonga mbele katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika, baada ya kuifunga Al Ghazala kwa jumla ya mabao 10-I.

Simba iliwakilishwa na Mahamadou Kassali, Nathaniel Chilambo, Antony Mligo, Rushine De Reuck, Yusuph Kagoma, Libasse Gueye, Neo Maema, Elie Mpanzu, Clatous Chama na Anicet Oura.

Mighty Wanderers: Dalitso Phiri, Promise Kamwendo, Lameck Mithi, Felix Zulu, Blessings Singini, Gaddie Chirwa, Issac Kaliati, Timothy Silwimba, Rajab Nyirenda, Stanley Sanudi.

Previous Post

UNDANI UGONJWA WA FIGO NA MATIBABU YAKE

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

TOTTENHAM YAHAMIA KWA AKANJI

TOTTENHAM YAHAMIA KWA AKANJI

1 year ago
TAIFA STARS AFCON 2027 INAWEZEKANA

TAIFA STARS AFCON 2027 INAWEZEKANA

8 months ago

Popular News

  • SIMBA HII GUSA UNASE CAFCL

    SIMBA HII GUSA UNASE CAFCL

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • UNDANI UGONJWA WA FIGO NA MATIBABU YAKE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA NI KIONGOZI WA MATOKEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA, NDEJEMBI TURUFU YA MAENDELEO KWA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI AONYA, ATOA SIKU 60 WENYE SILAHA HARAMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?