• ePaper
Wednesday, July 29, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Biashara

RC MAKALLA ATAKA MPANGO MKAKATI WA UTALII UKIJUMUISHA FURSA NA MAANDALIZI YA AFCON 2027

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 25, 2025
in Biashara, Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
RC MAKALLA ATAKA MPANGO MKAKATI WA UTALII UKIJUMUISHA FURSA NA MAANDALIZI YA AFCON 2027

MKUU wa Mkoa wa Arusha, CPA Amos Makalla

0
SHARES
8
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETIU

MKUU wa Mkoa wa Arusha, CPA Amos Makalla, amefanya kikao cha pamoja na wadau wa Utalii Arusha leo Alhamisi Septemba 25, 2025, lengo la kupokea changamoto zinazowakabili wadau na sekta ya utalii huku akisisitiza kuandaliwa kwa Mkakati wa miaka mitano wa ukuzaji utalii katika Mkoa wa Arusha.

Katika kikao hicho, CPA. Makalla amesema kuwa mkakati huo utaunganisha sekta mtambuka zinazohusiana na utalii, ikiwemo sekta ya michezo, mkakati ambao uhusika na maandalizi ya mapokezi ya wageni na watalii wakati wa michuano ya Mpira wa miguu kwa Mataifa ya Afrika AFCON 2027.

“Mpango kazi huo utahusisha kuwepo kituo cha utalii kitakachokuwa na nyaraka za utalii, tafiti za wanyamapori na na maonesho ya tamaduni za kitanzania hivyo timu nitakayoiunda itahusisha wataalamu kutoka Serikalini na wadau wa utalii ili sote tuzungumze lugha moja kwenye safari ya kukuza utalii Mkoa wa Arusha.” Amesema.

Aidha amesisitiza suala la uhifadhi endelevu Mkoani Arusha, usafi pamoja na utunzaji wa mazingira akieleza kuwa uhifadhi na utalii ni masuala yanayotegemeana na bila ya uhifadhi hakuna utalii utakaofanyika nchini.

Naye Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo Tanzania BMT, Neema Msitha, amebainisha kufurahishwa na mpango huo wa Mkoa akieleza utayari wa Wizara ya Michezo na Baraza kushirikiana katika maandalizi ya mpango huo utakaoeleza pia fursa za michuano ya AFCON na namna ya kuunganisha na sekta ya Utalii.

Baraza la michezo Taifa BMT na Bw. Eliufoo Nyambi, Mkurugenzi msaidizi wa maendeleo ya michezo kutoka Wizara ya habari, utamaduni, sanaa na michezo wameeleza kufurahishwa na mpango huo wa Mhe. Makalla na kueleza utayari wao katika kushirikiana na Mkoa kwenye uandaaji wa mpango huo pamoja na kuzieleza fursa zitakazotokana na michuano hiyo ya AFCON na namna ya kuiunganisha na sekta ya Utalii Mkoani Arusha.

Previous Post

KAHAWA YA TANZANIA KUONGEZEWA THAMANI KABLA YA KUPELEKWA NJE

Next Post

DK. SAMIA AAHIDI WAKULIMA DAWA YA KUPULIZIA MIKOROSHO BILA MALIPO

Next Post
DK. SAMIA AAHIDI WAKULIMA DAWA YA KUPULIZIA MIKOROSHO BILA MALIPO

DK. SAMIA AAHIDI WAKULIMA DAWA YA KUPULIZIA MIKOROSHO BILA MALIPO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. MWIGULU AWAONYA MADEREVA WA SERIKALI

DK. MWIGULU AWAONYA MADEREVA WA SERIKALI

8 months ago
DK. SAMIA KUWAINUA WANANCHI KIUCHUMI

DK. SAMIA KUWAINUA WANANCHI KIUCHUMI

10 months ago

Popular News

  • MVUTANO MAZISHI YA WAMBURA WAFIKA KORTINI, DALILI ZA MARIDHIANO ZACHOMOZA

    MVUTANO MAZISHI YA WAMBURA WAFIKA KORTINI, DALILI ZA MARIDHIANO ZACHOMOZA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA ATAJA SIFA ZA MAWASILIANO SERIKALINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • 50 BORA ‘FORM SIX’ KUSOMA AI NJE YA NCHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DHAHABU YENYE THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 1.2/- YAKAMATWA IKITOROSHWA DAR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA ATAKA UADILIFU, USHIRIKIANO NA MATOKEO KWA VIONGOZI WAPYA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?