• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Biashara

RC MAKALLA ATAKA MPANGO MKAKATI WA UTALII UKIJUMUISHA FURSA NA MAANDALIZI YA AFCON 2027

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 25, 2025
in Biashara, Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
RC MAKALLA ATAKA MPANGO MKAKATI WA UTALII UKIJUMUISHA FURSA NA MAANDALIZI YA AFCON 2027

MKUU wa Mkoa wa Arusha, CPA Amos Makalla

0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETIU

MKUU wa Mkoa wa Arusha, CPA Amos Makalla, amefanya kikao cha pamoja na wadau wa Utalii Arusha leo Alhamisi Septemba 25, 2025, lengo la kupokea changamoto zinazowakabili wadau na sekta ya utalii huku akisisitiza kuandaliwa kwa Mkakati wa miaka mitano wa ukuzaji utalii katika Mkoa wa Arusha.

Katika kikao hicho, CPA. Makalla amesema kuwa mkakati huo utaunganisha sekta mtambuka zinazohusiana na utalii, ikiwemo sekta ya michezo, mkakati ambao uhusika na maandalizi ya mapokezi ya wageni na watalii wakati wa michuano ya Mpira wa miguu kwa Mataifa ya Afrika AFCON 2027.

“Mpango kazi huo utahusisha kuwepo kituo cha utalii kitakachokuwa na nyaraka za utalii, tafiti za wanyamapori na na maonesho ya tamaduni za kitanzania hivyo timu nitakayoiunda itahusisha wataalamu kutoka Serikalini na wadau wa utalii ili sote tuzungumze lugha moja kwenye safari ya kukuza utalii Mkoa wa Arusha.” Amesema.

Aidha amesisitiza suala la uhifadhi endelevu Mkoani Arusha, usafi pamoja na utunzaji wa mazingira akieleza kuwa uhifadhi na utalii ni masuala yanayotegemeana na bila ya uhifadhi hakuna utalii utakaofanyika nchini.

Naye Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo Tanzania BMT, Neema Msitha, amebainisha kufurahishwa na mpango huo wa Mkoa akieleza utayari wa Wizara ya Michezo na Baraza kushirikiana katika maandalizi ya mpango huo utakaoeleza pia fursa za michuano ya AFCON na namna ya kuunganisha na sekta ya Utalii.

Baraza la michezo Taifa BMT na Bw. Eliufoo Nyambi, Mkurugenzi msaidizi wa maendeleo ya michezo kutoka Wizara ya habari, utamaduni, sanaa na michezo wameeleza kufurahishwa na mpango huo wa Mhe. Makalla na kueleza utayari wao katika kushirikiana na Mkoa kwenye uandaaji wa mpango huo pamoja na kuzieleza fursa zitakazotokana na michuano hiyo ya AFCON na namna ya kuiunganisha na sekta ya Utalii Mkoani Arusha.

Previous Post

KAHAWA YA TANZANIA KUONGEZEWA THAMANI KABLA YA KUPELEKWA NJE

Next Post

DK. SAMIA AAHIDI WAKULIMA DAWA YA KUPULIZIA MIKOROSHO BILA MALIPO

Next Post
DK. SAMIA AAHIDI WAKULIMA DAWA YA KUPULIZIA MIKOROSHO BILA MALIPO

DK. SAMIA AAHIDI WAKULIMA DAWA YA KUPULIZIA MIKOROSHO BILA MALIPO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA ASISITIZA VIJANA KULINDA AMANI

DK. SAMIA ASISITIZA VIJANA KULINDA AMANI

2 days ago
DK. BASHIRU AELEZEA UJASIRI WA DK. SAMIA

DK. BASHIRU AELEZEA UJASIRI WA DK. SAMIA

1 month ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.