• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 13, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan

0
SHARES
1
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MUSSA YUSUPH,

Geita

MGOMBEA Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan, amewahakikishia wananchi kuleta maendeleo na kujenga uchumi jumuishi.

Akizungumza katika mkutano wake wa kampeni uliofanyika viwanja vya Shule ya Msingi Bukombe, Dk. Samia, aliwahakikishia wananchi kwamba, atawatumikia kuleta maendeleo na kujenga taifa jumuishi.

Alisema wachimbaji wa wilaya hiyo, walikuwa wakivamia Pori la Akiba Kigosi Moyowosi, kuchimba madini ya dhahabu kwa njia isiyo rasmi.

Alieleza kuwa, rasilimali hiyo ambayo Mungu ameishusha nchini, iwanufaishe vijana na serikali, imeamua kuwamilikisha baadhi ya maeneo kuliko vijana kuendelea kuiba. 

“Kuliko wapigwe na askari wa uhifadhi, wapelekwe mahakamani, nikasema hapana. Nikamtaka Dk. Doto Biteko (Naibu Waziri Mkuu) na wenzake serikalini, waangalie namna watakavyoweza kufanya rasilimali hiyo iwafae vijana wa Bukombe.

Aliongeza: “Leo wanachimba, wanauza, tumewajengea masoko na maisha yanakwenda vizuri sana.

“Huku ndiko kujenga utu wa Mtanzania, ndiko kujenga utu wa vijana wetu. Ndiko kuwawezesha waendelee na maisha yao yawe mazuri, wapate heshima ya kutosha.”

Kwa upande wa kilimo, Dk. Samia, alisema wapo wakulima ambao kwa muda mrefu, walikuwa wakitaka kuvuna kwa kiasi kikubwa, wapate fedha za kutosha kuendesha maisha yao

Alibainisha hatua zilizochukuliwa na serikali kuwapatia ruzuku ya mbolea, dawa za kilimo kisha kuwajengea skimu za umwagiliaji walime na kuzalisha mazao kwa wingi.

Previous Post

DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

Next Post

MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

Next Post
MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

AHADI 5 ZA MGOMBEA URAIS WA CCM, IGUNGA

AHADI 5 ZA MGOMBEA URAIS WA CCM, IGUNGA

1 month ago
DK. SAMIA AWAPA FARAJA WENYE MAHITAJI MAALUMU

DK. SAMIA AWAPA FARAJA WENYE MAHITAJI MAALUMU

1 day ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.