• ePaper
Wednesday, March 18, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 13, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan

0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MUSSA YUSUPH,

Geita

MGOMBEA Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan, amewahakikishia wananchi kuleta maendeleo na kujenga uchumi jumuishi.

Akizungumza katika mkutano wake wa kampeni uliofanyika viwanja vya Shule ya Msingi Bukombe, Dk. Samia, aliwahakikishia wananchi kwamba, atawatumikia kuleta maendeleo na kujenga taifa jumuishi.

Alisema wachimbaji wa wilaya hiyo, walikuwa wakivamia Pori la Akiba Kigosi Moyowosi, kuchimba madini ya dhahabu kwa njia isiyo rasmi.

Alieleza kuwa, rasilimali hiyo ambayo Mungu ameishusha nchini, iwanufaishe vijana na serikali, imeamua kuwamilikisha baadhi ya maeneo kuliko vijana kuendelea kuiba. 

“Kuliko wapigwe na askari wa uhifadhi, wapelekwe mahakamani, nikasema hapana. Nikamtaka Dk. Doto Biteko (Naibu Waziri Mkuu) na wenzake serikalini, waangalie namna watakavyoweza kufanya rasilimali hiyo iwafae vijana wa Bukombe.

Aliongeza: “Leo wanachimba, wanauza, tumewajengea masoko na maisha yanakwenda vizuri sana.

“Huku ndiko kujenga utu wa Mtanzania, ndiko kujenga utu wa vijana wetu. Ndiko kuwawezesha waendelee na maisha yao yawe mazuri, wapate heshima ya kutosha.”

Kwa upande wa kilimo, Dk. Samia, alisema wapo wakulima ambao kwa muda mrefu, walikuwa wakitaka kuvuna kwa kiasi kikubwa, wapate fedha za kutosha kuendesha maisha yao

Alibainisha hatua zilizochukuliwa na serikali kuwapatia ruzuku ya mbolea, dawa za kilimo kisha kuwajengea skimu za umwagiliaji walime na kuzalisha mazao kwa wingi.

Previous Post

DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

Next Post

MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

Next Post
MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

UKWASI MIFUKO HIFADHI YA JAMII NCHINI, WAPAA

UKWASI MIFUKO HIFADHI YA JAMII NCHINI, WAPAA

1 month ago
DK. MWIGULU ATOA SIKU 10

DK. MWIGULU ATOA SIKU 10

4 months ago

Popular News

  • MANDONGA AJA KIVINGINE

    MANDONGA AJA KIVINGINE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YATUMIA BILIONI 64/- KUBORESHA UWANJA WA NDEGE IRINGA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU AWAWEKA MTEGONI VIGOGO WILAYA, HALMASHAURI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ALAMA TATU KUMUENZI JPM

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI KUIFANYA TANZANIA KITOVU CHA BIASHARA – DK. YONAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?