• ePaper
Thursday, April 30, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

‘MLIOGHUSHI AKAUNTI ZA JKT MITANDOANI ZIFUTENI HARAKA’

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 8, 2025
in Habari, Kitaifa
0
‘MLIOGHUSHI AKAUNTI ZA JKT MITANDOANI ZIFUTENI HARAKA’
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na HAPPINESS MTWEVE,
Dodoma

JESHI la Kujenga Taifa (JKT), limewataka watu waliofungua mitandao ya kughushi, kwa kutumia jina, nembo, rangi, namba za vikosi, majina ya vikosi au kambi, kuzifunga mara moja akaunti hizo.

Onyo hilo lilitolewa jijini hapa kwa vyombo vya habari na Kurugenzi ya Mawasiliano JKT Makao Makuu.

Pia, lilisisitiza yeyote atakayebainika anaendelea kutumia akaunti hizo za mitandao ya kijamii atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Taarifa hiyo ilifafanua katika utekelezaji wa majukumu yake, JKT imekuwa na utaratibu wa kutoa taarifa zinazohusu shughuli zake kupitia vyombo vya habari au mitandao ya kijamii nchini.

“Tuna tovuti ambayo ni www.jkt.tz na mitandao ya kijamii ya JKT kwa Instagram ni jkttanzania na YouTube JKTTanzania au Twitter (x) ni JKTonline tz,”ilifafanua taarifa hiyo.

Jeshi hilo limedai hivi karibuni kumejitokeza baadhi ya watu kufungua akaunti za kughushi katika mitandao ya kijamii kwa kutumia jina, nembo na rangi za JKT na kuaminisha umma akaunti hizo za jeshi hilo la kujenga taifa.

Ilisema akaunti hizo, zimekuwa zikipakia maudhui yenye kuleta taharuki kwa jamii kuhusiana na shughuli zinazofanywa na JKT.

“Tunakumbusha wananchi kuendelea kupata taarifa sahihi zenye uhakika zinazolihusu kutoka makao makuu ya JKT,” iliongeza taarifa hiyo.

Previous Post

WANASIASA WAGUSIA USHINDI WA RAIS DK. SAMIA

Next Post

JKT TZ, SIMBA BALAA LIPO HAPA

Next Post
JKT TZ, SIMBA BALAA LIPO HAPA

JKT TZ, SIMBA BALAA LIPO HAPA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. MWIGULU ASHUSHA PRESHA UPATIKANAJI WA MAJI SAFI

DK. MWIGULU ASHUSHA PRESHA UPATIKANAJI WA MAJI SAFI

4 months ago
KAULI UN YAWAKOSHA MABALOZI, WAHADHIRI

KAULI UN YAWAKOSHA MABALOZI, WAHADHIRI

4 months ago

Popular News

  • TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VYALENGA KUIJENGA JAMII KIUCHUMI NA KIROHO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUVUMILIANA MUHIMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI SANGU ABAINISHA HIFADHI SKIMU INAVYOENDA KUBADILI MAISHA YA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?