• ePaper
Sunday, May 17, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

FOLZ  AKILI YOTE KWA WAMALAWI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 16, 2025
in Burudani, Habari, Michezo
0
FOLZ  AKILI YOTE KWA WAMALAWI
0
SHARES
8
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na ABDUL DUNIA

LICHA ya kukiri mechi dhidi ya Silver Strikers ya Malawi itakuwa ngumu, Kocha wa Yanga, Romain Folz, amesema lengo lao ni kupata matokeo mazuri katika mtanange huo.

Yanga itachuana na Silver Strikers katika mechi ya hatua ya pili ya mtoano ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL), utakaopigwa Oktoba 18, 2025, katika Uwanja wa Taifa wa Bingu uliopo Lilongwe, Malawi.

Yanga ilianza michuano hiyo kwa ushindi wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya Wiliete de Benguela ya Angola kabla ya kushinda 2-0 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Silver Strikers ilitinga hatua hiyo kwa kuitoa Elgeco Plus ya Madagascar kwa faida ya bao la ugenini.

Katika mchezo wa kwanza uliochezwa Mauritius, Silver Strikers ilitoka sare ya bao 1-1 dhidi ya mwenyeji kabla ya kutoka suluhu katika dimba la Bingu nchini Malawi.

Akizungumzia mchezo huo, Folz alisema anaiandaa vyema timu yake kuhakikisha inapata matokeo mazuri licha ya mechi hiyo kuwa ngumu.

“Tunafanya kila linalowezekana kujiandaa vyema kuwakabili wapinzani wetu, ni ligi ya mabingwa hivyo kila timu ina ubora na kama isingekuwa hivyo basi timu kama hizo zisingekuwepo.

(Silver Strikers) Ni timu nzuri lakini tumefanya uchambuzi kuhusu wao, tunawaheshimu lakini hatimaye matokeo mazuri ndiyo kitu tunachotaka kupata,” alisema.

Mshindi wa jumla wa mechi mbili za hatua hiyo ndiyo itatinga hatua ya makundi ya CAFCL msimu huu.

Timu zinazoshiriki hatua za awali katika Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) zitavuna dola za Marekani 100,000 ambazo ni zaidi ya sh. milioni 244 za Tanzania.

Katika CAFCL, timu zitakazotinga hatua ya makundi zitakuwa na uhakika wa kuvuna dola za Marekani 700,000 ambazo ni zaidi ya sh. bilioni 1.7 za Tanzania.

Timu zitakazotinga robo fainali, kila moja itakuwa na uhakika wa kuvuna dola za Marekani 900,000 ambazo ni zaidi ya sh. bilioni 2.2 wakati zitakazoishia nusu fainali zikivuna dola za Marekani milioni 1.2 ambazo ni zaidi ya sh. bilioni 2.9 za Tanzania.

Bingwa wa CAFCL msimu huu, anatarajiwa kuondoka na dola za Marekani milioni 4 ambazo ni zaidi ya sh. bilioni 9.7 za Tanzania wakati mshindi wa pili ikiondoka na dola za Marekani milioni 2 ambazo ni zaidi ya sh. bilioni 4.9 za Tanzania.

Previous Post

PANTEV KICHEKO SIMBASC

Next Post

DK. SAMIA KUVALIA NJUGA SHIDA YA MAJI

Next Post
DK. SAMIA KUVALIA NJUGA SHIDA YA MAJI

DK. SAMIA KUVALIA NJUGA SHIDA YA MAJI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA KUANZA MASOMO KWA MKUPUO

WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA KUANZA MASOMO KWA MKUPUO

5 months ago
DK. NCHIMBI ATOA AGIZO KWA PROF. MKENDA

DK. NCHIMBI ATOA AGIZO KWA PROF. MKENDA

5 months ago

Popular News

  • DK. MWIGULU AHIMIZA WANANCHI KUIOMBEA AMANI YA NCHI

    DK. MWIGULU AHIMIZA WANANCHI KUIOMBEA AMANI YA NCHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. KIKWETE ASHIRIKI MAZISHI YA KITAIFA YA RAIS MSTAAFU MOGAE WA BOTSWANA, AKIMWAKILISHA RAIS DK. SAMIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DANGOTE AIPONGEZA SERIKALI, AANGAZIA FURSA ZA UWEKEZAJI NCHINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TANZANIA NI NCHI YA PILI AFRIKA KUWA NA HADHI YA  UTALII WA JIOLOJIA (GEOPARK MUSEUM)

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAIPONGEZA PUMA ENERGY KWA MFUMO MPYA WA KIDIJITALI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?