• ePaper
Friday, November 14, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Burudani

PANTEV KICHEKO SIMBASC

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 16, 2025
in Burudani, Habari, Michezo
0
PANTEV KICHEKO SIMBASC
0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

WAKATI kikosi cha Simba kikitarajiwa kuondoka nchini leo, kocha wa timu hiyo Dimitar Pantev amesema ana furaha na nyota wake baada ya kupata ushindi katika mechi mbili za kirafiki.

Pantev ametoa kauli hiyo Dar es Salaam, baada ya timu yake kuibuka na ushindi dhidi ya Al Hilal Omdurman ya Sudan kwa kuifunga mchezo wa kwanza mabao 2-1 kabla ya juzi kupata ushindi wa mabao 4-1, michezo hiyo ilipigwa katika Uwanja wa Gymkhana.

“Ushindi ambao tumeupata katika mechi zetu mbili za kirafiki dhidi ya Al Hilal, umetuongezea morari ya kutosha kuhakikisha tunapata ushindi tukiwa ugenini  katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika kabla ya kumalizia nyumbani,”alitamba kocha huyo.

Pantev alisema Simba imejipanga vizuri kushinda mchezo wake wa kwanza wa hatua ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Nsingizini Hotspurs utakaochezwa Jumapili, wiki hii nchini Eswatin.

Mechi hiyo ya raundi ya kwanza inatarajiwa kuchezwa katika Uwanja wa Uwanja wa Somhlolo, uliopo Lobamba nchini humo saa 10:00 jioni.

“Nimepata taswira ya jinsi gani ya kukitengeneza kikosi hicho hasa kuelekea katika mchezo  huu wa Kimataifa.

“Ukweli mechi hizo zimewapa morari ya kutosha wachezaji wangu  kuhakikisha tunashinda mchezo dhidi ya Nsingizini, nina imani tutafanya vizuri,”alisema.

Hata hivyo, Pantev alisema hivi sasa hawezi kubadilisha kila kitu kwa wakati mmoja, lakini anahitaji timu inayocheza kwa mpangilio, kushambulia na kulinda kwa pamoja, kitu ambacho amesema amekiona wachezaji wake wanakifanya.

“Nilipokuwa najiunga na Simba, niliomba mechi za kirafiki za kimataifa, kuona namna gani timu inacheza, hivyo mechi hizo mbili ni kwa ajili ya kujenga maelewano ya kimbinu.

“Tunahitaji kuwa na timu inayocheza kwa mpangilio, inayoshambulia kwa hesabu na kujilinda kwa pamoja, hizi ndizo mechi zinazoniwezesha kuona nani yuko tayari kupigania nembo ya Simba, ” alisema kocha huyo.

Alisema pamoja na kwamba kikosi chake kinacheza bila baadhi ya wachezaji ambao wapo katika vikosi vya timu za taifa, lakini waliobaki wanakuwa tayari kiakili na kimwili ili wakirejea iwe rahisi kwake kuunganisha mfumo.

Previous Post

DK. SAMIA AWAPA KICHEKO KARAGWE

Next Post

FOLZ  AKILI YOTE KWA WAMALAWI

Next Post
FOLZ  AKILI YOTE KWA WAMALAWI

FOLZ  AKILI YOTE KWA WAMALAWI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

SADC WAMPONGEZA RAIS DK. SAMIA KWA USHINDI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 2025

SADC WAMPONGEZA RAIS DK. SAMIA KWA USHINDI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 2025

6 days ago
DK. SAMIA AAHIDI MAGEUZI MAKUBWA YA KILIMO

DK. SAMIA AAHIDI MAGEUZI MAKUBWA YA KILIMO

2 months ago

Popular News

  • DK. MWIGULU ATUMA SALAMU KWA WALA RUSHWA, WAZEMBE

    DK. MWIGULU ATUMA SALAMU KWA WALA RUSHWA, WAZEMBE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NYOTA TAIFA STARS  MZUKA UMEPANDA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RONALDO KUTUNDIKA DALUGA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JINA LA WAZIRI MKUU MTEULE KUWASILISHWA BUNGENI LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWAKINYO KUPANDA ULINGONI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.