• ePaper
Wednesday, September 9, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

WFP KUENDELEZA USHIRIKIANO NA TANZANIA USIMAMIZI WA MAAFA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
June 4, 2026
in Habari, Kitaifa
0
WFP KUENDELEZA USHIRIKIANO NA TANZANIA USIMAMIZI WA MAAFA
0
SHARES
9
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI MAALUMU, Morogoro

SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (World Food Programme -WFP), limesema litaendeleza ushirikiano na serikali ya Tanzania katika kuhakikisha masuala ya menejimenti ya maafa yanaendelea kutekelezwa kwa tija na malengo yaliyokusudiwa kwa kuimarisha uwezo wa kitaalamu na Kiteknolojia kwa kutumia teknolojia za kisasa.

Hayo yameelezwa na Naibu Mkurugenzi wa WFP Tanzania, Christine Mendes wakati wa ufunguzi wa warsha ya zoezi la uigaji la uratibu wa utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji wakati wa dharura inayoendelea mkoani Morogoro.

Christine amesema ushirikiano hususan katika kuwezesha utekelezaji wa Mradi wa Field-Based Preparedness Project (FBPP), ambapo katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, mradi huo umechangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha uwezo wa taifa katika sekta ya utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji.

Aidha, alieleza zoezi la uigaji la uratibu wa utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji wakati wa dharura linawakilisha hatua muhimu katika kuendelea kujitolea kwa Tanzania katika kuimarisha utayari wa kitaifa katika uratibu wa masuala ya maafa.

“Katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, Mradi wa Matayarisho ya Uwandani (FBPP) umetoa mafanikio yaliyounganishwa ambayo yameimarisha kwa kiasi kikubwa utayarishaji wa vifaa na mfumo wa kukabiliana na dharura wa Tanzania,” alisema.

Ameongeza WFP itaendeleza ushirikiano wake na serikali na kuwa mstari wa mbele katika kuunga mkono masuala ya menejimenti ya maafa kuyafikia matarajio kwa pamoja kwa kuwa na mfumo wa kukabiliana na hali ya dharura wa kitaifa wenye kasi zaidi, ulioratibiwa vyema na unaostahimili zaidi wenye uwezo wa kutoa hatua za kibinadamu kwa wakati unaofaa.

“Tutumie fursa hii kikamilifu, siyo tu kupima mifumo, lakini kuimarisha mifumo, hivyo tuthibitishe tena dhamira yetu ya pamoja ya kujitayarisha kwa kuwajibikana kulenga kwa dhati kuokona maisha,” amesisitiza Christine.

Previous Post

HESHIMA KUBWA KWA TANZANIA

Next Post

MWANZA KINARA USIMAMIZI MAAFA

Next Post
MWANZA KINARA USIMAMIZI MAAFA

MWANZA KINARA USIMAMIZI MAAFA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

CHAI YA MOTO KUPITA KIASI YATAJWA KUCHOCHEA SARATANI YA KOO

CHAI YA MOTO KUPITA KIASI YATAJWA KUCHOCHEA SARATANI YA KOO

5 months ago
NJOONI MUONE SHOO

NJOONI MUONE SHOO

10 months ago

Popular News

  • RAIS DK. SAMIA, NDEJEMBI TURUFU YA MAENDELEO KWA WATANZANIA

    RAIS DK. SAMIA, NDEJEMBI TURUFU YA MAENDELEO KWA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI AONYA, ATOA SIKU 60 WENYE SILAHA HARAMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NDEJEMBI MZIGONI RASMI, AKEMEA KAZI KWA MAZOEA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUME MIPANGO, NIRC WAJADILI UBORA MIRADI YA UMWAGILIAJI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MASAUNI AANIKA UMAHIRI WA TANZANIA INAVYOLINDA UDONGO, MATUMIZI MBOLEA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?