• ePaper
Sunday, May 17, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

TASWIRA VIGOGO VINNE LIGI KUU BARA IKO HIVI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
March 4, 2026
in Burudani, Michezo
0
TASWIRA VIGOGO VINNE LIGI KUU BARA IKO HIVI
0
SHARES
11
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na WAANDISHI WETU

WAKATI michuano ya Ligi Kuu Bara ikizidi kunoga, kasi ya ukusanyaji wa pointi kwa timu nne kubwa katika mechi 11 za kwanza msimu huu imepungua, ukilinganisha na msimu uliopita.

Timu zilizocheza mechi 11 katika ligi hiyo msimu huu ni kinara Yanga, Simba (3), Azam FC (5) na Singida Black Stars nafasi ya tisa huku nyingine zilizobakia zikicheza kuanzia 13 hadi 17.

Timu hizo nne ambazo zimecheza mechi chache zaidi kutokana na ushiriki wake katika michuano ya kimataifa, msimu huu zimekuwa na kasi ndogo ya ukusanyaji wa alama katika mechi 11 za kwanza tofauti na ilizozikusanya msimu uliopita.

Licha ya kuongoza ligi kwa alama 29, Yanga msimu huu ina upungufu wa alama moja zaidi ya ilizokusanya msimu uliopita wakati Simba iliyopo nafasi ya tatu kwa pointi 24 ina upungufu wa pointi nne ya ilizokusanya msimu uliopita msimu uliopita.

Azam FC ambayo sasa ina pointi 23 katika nafasi ya tano ina upungufu wa alama moja ukilinganisha na msimu uliopita wakati Singida Black Stars iliyopo nafasi ya tisa kwa alama 19 ikiwa na upungufu wa pointi tano ukilinganisha na msimu uliopita.

Kwa mujibu wa takwimu, msimu uliopita katika mechi 11 za kwanza, Yanga ilikusanya alama 30, ikishinda 10 na kufungwa moja wakati Simba ikikusanya pointi 28 ikishinda tisa, sare moja na kufungwa moja.

Azam FC ilivuna pointi 24, ikishinda mechi saba, sare tatu na kufungwa moja sawa na Singida BS.

Msimu huu, Yanga imeshinda mechi tisa, sare mbili wakati Simba ikishinda mechi saba, sare mbili na kufungwa moja, Azam FC ikishinda mechi sita na sare tano huku Singida BS ikishinda michezo mitano, sare nne na kufungwa miwili.

Akizungumzia ushindani wa ligi hiyo msimu huu, aliyekuwa Kocha wa Yanga, Boniface Mkwasa, alisema michuano hiyo msimu huu ni migumu kwani kila timu inaonesha uwezo kuhakikisha inamaliza nafasi za juu.

Alisema baadhi ya timu ambazo hazijawahi kucheza michuano ya kimataifa zimekuwa na shauku ya kushiriki michuano hiyo msimu ujao, hivyo zinapambana kuhakikisha zinamaliza nafasi nne za juu.

“Timu kama JKT Tanzania na Pamba Jiji zimekuwa na kiwango bora zaidi msimu huu na kwamba zinapambana kuhakikisha zinamaliza nafasi nne za juu ili kujihakikishia kushiriki michuano ya kimataifa msimu ujao.

“Ligi bado ni ngumu na kwamba hivi sasa huwezi kujua nani anayeweza kutwaa ubingwa msimu huu, lakini Simba na Yanga lazima zimalize nafasi ya kwanza na ya pili kutokana na uzoefu wao,” alisema Mkwasa.

Kocha na mchambuzi wa soka, Kenedy Mwaisabula ‘Mzazi’ alisema michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu imekuwa na ushindani wa aina yake.

Alisema michuano hiyo imeongeza ushindani baina ya timu kutokana na ubora wa timu zinazoshiriki msimu huu.

Alisisitiza timu zote zimekuwa katika ushindani wa hali ya juu kwani kila moja inataka kumaliza nafasi nzuri katika msimamo wa Ligi na kufikia malengo waliyojiwekea.

“Ushindani ni wa hali ya juu zaidi msimu huu kwani kila timu inataka kumaliza katika nafasi nzuri na kufikia malengo iliyojiwekea.

“Ligi bado ni ngumu kila mmoja anamwomwombea mwenzake mabaya ili apoteze na kumpiku katika msimamo, hivyo bado ushindani utaendelea kuwa mkali zaidi katika mechi zitakazofuata,” alisema Mzazi.

Previous Post

TRA YAJIVUNIA MAFANIKIO NDANI YA SIKU 100 ZA RAIS DK. SAMIA

Next Post

MAAGIZO YA DK. MIGIRO KWA SHULE YA UONGOZI MWALIMU NYERERE

Next Post
MAAGIZO YA DK. MIGIRO KWA SHULE YA UONGOZI MWALIMU NYERERE

MAAGIZO YA DK. MIGIRO KWA SHULE YA UONGOZI MWALIMU NYERERE

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

SERIKALI IMEIMARISHA BARABARA – DK. SAMIA

SERIKALI IMEIMARISHA BARABARA – DK. SAMIA

8 months ago
DK. MWINYI AFUNGUKA MALENGO SERA YA NISHATI

DK. MWINYI AFUNGUKA MALENGO SERA YA NISHATI

8 months ago

Popular News

  • DK. MWIGULU AHIMIZA WANANCHI KUIOMBEA AMANI YA NCHI

    DK. MWIGULU AHIMIZA WANANCHI KUIOMBEA AMANI YA NCHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. KIKWETE ASHIRIKI MAZISHI YA KITAIFA YA RAIS MSTAAFU MOGAE WA BOTSWANA, AKIMWAKILISHA RAIS DK. SAMIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DANGOTE AIPONGEZA SERIKALI, AANGAZIA FURSA ZA UWEKEZAJI NCHINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TANZANIA NI NCHI YA PILI AFRIKA KUWA NA HADHI YA  UTALII WA JIOLOJIA (GEOPARK MUSEUM)

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAIPONGEZA PUMA ENERGY KWA MFUMO MPYA WA KIDIJITALI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?