• ePaper
Wednesday, September 9, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

‘TUTAPELEKA MIRADI KWA WANANCHI WOTE’

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
February 19, 2026
in Habari, Kitaifa
0
‘TUTAPELEKA MIRADI KWA WANANCHI WOTE’
0
SHARES
11
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na ATHNATH MKIRAMWENI, Urambo

KATIBU wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kenani Kihongosi, amesema serikali itaendelea kupeleka maendeleo kwa wananchi wote.

Kihongosi alitoa kauli hiyo alipozungumza na wananchi na wafanyabiashara wa Soko la Ndizi, walioeleza wasiwasi wao kuhusu uamuzi wa kuhamishwa katika eneo la biashara.

Kihongosi alisema mabadiliko ya maendeleo huambatana na faida na changamoto, lakini lengo kuu la serikali ni kustawisha maisha ya wananchi.

Alisema katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, zikiwemo barabara za lami na Reli ya Kisasa (SGR), wakati mwingine wananchi hulazimika kupisha miradi hiyo kwa manufaa ya taifa.

Kuhusu soko jingine kutozinduliwa na Mwenge wa Uhuru, Kihongosi alisema kitendo hicho hakiufanyi mradi kuwa batili, bali huashiria uwepo wa dosari zinazohitaji kurekebishwa.

Kihongosi alimwagiza Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paul Chacha, kushirikiana na Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa, Said Nkumba, kukutana na wafanyabiashara na viongozi wa wilaya kusikiliza hoja zao na kufikia mwafaka.

Alisema haitakuwa busara kutoa uamuzi wa upande mmoja bila mazungumzo ya kina, kwa kuwa utamaduni wa CCM ni kusikiliza wananchi na kushughulikia changamoto zao.

Vilevile, wafanyabiashara wa Soko la Ndizi walieleza wamepokea notisi ya kuhama ifikapo Machi 30, mwaka huu hatua iliyozua hofu ya kupoteza mitaji yao endapo eneo jipya halitakuwa na wateja wa kutosha.

Aidha, aliwahimiza wananchi kuchagua viongozi wa kusimamia maslahi yao kwa mujibu wa sheria na taratibu.

Naye Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tabora, Nkumba, aliwahakikishia wafanyabiashara na wananchi Chama na serikali vimejipanga kutekeleza maelekezo yaliyotolewa kulinda maslahi ya pande zote.

Kihongosi alisema CCM inaendelea kusimamia ustawi wa wananchi kuhakikisha wafanyabiashara wanafanya shughuli zao katika mazingira ya amani na utulivu.

Previous Post

DK. MWIGULU APIGA ‘SPANA’ KONA ZOTE

Next Post

KIHONGOSI AANIKA UIMARA WA CCM KWA WATANZANIA

Next Post
KIHONGOSI AANIKA UIMARA WA CCM KWA WATANZANIA

KIHONGOSI AANIKA UIMARA WA CCM KWA WATANZANIA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. MWIGULU APIGA MARUFUKU WANAFUNZI KUBEBA VIDUMU

DK. MWIGULU APIGA MARUFUKU WANAFUNZI KUBEBA VIDUMU

7 months ago
KIBU DENIS, MANULA WATEMWA STARS

KIBU DENIS, MANULA WATEMWA STARS

1 year ago

Popular News

  • RAIS DK. SAMIA, NDEJEMBI TURUFU YA MAENDELEO KWA WATANZANIA

    RAIS DK. SAMIA, NDEJEMBI TURUFU YA MAENDELEO KWA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI AONYA, ATOA SIKU 60 WENYE SILAHA HARAMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NDEJEMBI MZIGONI RASMI, AKEMEA KAZI KWA MAZOEA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUME MIPANGO, NIRC WAJADILI UBORA MIRADI YA UMWAGILIAJI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MASAUNI AANIKA UMAHIRI WA TANZANIA INAVYOLINDA UDONGO, MATUMIZI MBOLEA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?