• ePaper
Thursday, April 30, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Biashara

TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 10, 2025
in Biashara, Habari, Kimataifa, Kitaifa
0
TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU, 
RIYADH

KATIBU Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dk. Hassan Abbasi, ameihakikishia jumuiya ya kimataifa kuwa hali ya amani na utalii nchini Tanzania iko imara, kufuatia machafuko yaliyotokea katika baadhi ya maeneo wakati na baada ya uchaguzi.

Dk. Abbasi ametoa kauli hiyo leo Novemba 9, 2025, jijini Riyadh, Saudi Arabia, alipokuwa akiongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa 26 wa Baraza Kuu la Shirika la Utalii Duniani (UN Tourism).

Akizungumza wakati akichangia Taarifa ya Utekelezaji ya Mwaka ya Shirika hilo, Dk. Abbasi amesema Tanzania imeendelea kunufaika na programu mbalimbali za UN Tourism, ikiwemo uandaaji wa Mkutano wa Dunia wa Utalii wa Vyakula kwa Kanda ya Afrika uliofanyika Arusha Aprili mwaka huu, pamoja na ufadhili wa miradi ya utunzaji wa mazingira katika Safu za Milima ya Usambara.

“Baada ya changamoto za uchaguzi, Serikali imefanya jitihada kubwa kurejesha hali ya utulivu nchini. Tanzania ni salama, vivutio vyetu vyote viko salama, na tunawakaribisha wajumbe wa mkutano huu na wadau wa utalii kuendelea kutembelea nchi yetu — kivutio bora cha utalii barani Afrika,” amesema Dkt. Abbasi.

Aidha, Tanzania imeendelea kuimarisha nafasi yake ndani ya shirika hilo, ikiwa ni miongoni mwa nchi 32 pekee kati ya wanachama 160 waliochaguliwa kuwa wajumbe wa Kamati ya Utendaji (Executive Committee). 

Pia, Baraza Kuu hilo limeipitisha Tanzania kuwa Mjumbe wa Kamati ya Kuhakiki Wanachama (UN Tourism Credentials Committee).

Mkutano huo unaendelea jijini Riyadh, ambapo pamoja na masuala mengine, utajadili matumizi ya akili bandia (AI) katika kutangaza utalii na uchaguzi wa Katibu Mtendaji mpya wa shirika hilo.

Previous Post

UVCCM YAWAPA POLE WALIOPATA MADHILA

Next Post

BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO DODOMA

Next Post
BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO DODOMA

BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO DODOMA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

PM MWIGULU ASHUSHA RUNGU WIZARA YA MAJI

PM MWIGULU ASHUSHA RUNGU WIZARA YA MAJI

2 months ago
DK. GWAJIMA AONYA ‘WATU WAZIMA OVYO’ MITANDAONI

DK. GWAJIMA AONYA ‘WATU WAZIMA OVYO’ MITANDAONI

4 months ago

Popular News

  • TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VYALENGA KUIJENGA JAMII KIUCHUMI NA KIROHO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUVUMILIANA MUHIMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI SANGU ABAINISHA HIFADHI SKIMU INAVYOENDA KUBADILI MAISHA YA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?