MGOMBEA Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuunguruma leo, katika Mkoa wa Morogoro.
Dk. Samia atafanya mkutano wake wa kwanza eneo la Ngerengere, kisha fungakazi itakuwa katika Viwanja vya Jamhuri ambako atahutubia maelfu ya wananchi katika mji huo.
Jana, CCM ilizindua kampeni zake za uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, mwaka huu.
Mkutano huo wa kampeni ulifanyika katika viwanja vya Tanganyika Packers Kawe, jijini Dar es Salaam.




