• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

DK. SAMIA, BALOZI NCHIMBI WAAHIDIWA KURA ZA KISHINDO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
August 30, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
DK. SAMIA, BALOZI NCHIMBI WAAHIDIWA KURA ZA KISHINDO
0
SHARES
0
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

 Na NJUMAI NGOTA, Mwanza

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Mwanza, Michael Lushinge ‘Smart’,  amesema wamejiandaa kikamilifu kushiriki uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu, huku akimwakikishia Mgombea Mwenza wa Urais wa Chama, Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi kuwa Mgombea wa Urais wa CCM, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, atapata kura za kishindo mkoani humo.

Lushinge amesema hayo Kata ya Mwankulwe, wilayani Kwimba, alipomkaribisha Mgombea Mwenza wa Urais, Balozi Dk.  Nchimbi, kuzungumza na mamia ya wananchi waliohudhuria uzinduzi wa kampeni za CCM.

Amesema Rais Dk. Samia na Mgombea Mwenza wa Urais watapata kura za kutosha na za kishindo mkoani humo.

 “Katika mkoa huu, nikuhakikishie kura za kishindo kwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan. kama unavyofahamu Kanda ya Mwanza na Kanda ya Ziwa, kura zitakuwa za kutosha na ni za kishindo, hivyo tumejipanga kikamilifu kushiriki uchaguzi mkuu.

“Sisi wana-Mwanza tunaingia katika uchaguzi tukiwa kifua mbele, hivi ninavyozungumza tuna mtaji rasilimali, wanachama zaidi ya 700,000  tayari wamejisajili katika mfumo wetu.

“Hao ni wanachama ambao tunawatambua, nikuhakikishie Mkoa wa Mwanza na wana-Kwimba kwa ujumla, tumejiandaa kikamilifu kwa uchaguzi,”amesema.

Amesema Chama kiliteua wagombea wazuri na walifuata utaratibu wa kidemokrasia, hivyo wana uhakika kitapata ushindi wa kishindo.

Ametoa wito kwa wananchi na wanaCCM kuendelea kuwa wamoja na kutunza amani ambayo ni tunu waliyoikuta na kuirithi kutoka kwa wazee wao.

Katika hatua nyingine, Mwenyekiti huyo amesema Balozi Dk. Nchimbi, alikitumikia Chama vizuri alipokuwa Katibu Mkuu na ameacha alama kubwa na mshikamano ndani ya CCM.

“Hakika Chama hivi sasa ni kipya, kipo katika muundo mzuri na thabiti, ninaomba nikushukuru kwa uongozi wako uliotukuka kwa kukiongoza ukiwa Katibu Mkuu,”amesema.

Mwenyekiti huyo alitumia fursa hiyo kumpongeza Katibu Mkuu wa Chama, Balozi Dk. Asha-Rose Migiro kwa kuteuliwa na kudhibitishwa na Mkutano Mkuu wa Halmashauri Kuu Taifa wa CCM.

Previous Post

TANZANIA IPO SALAMA MIKONONI MWA CCM – PETER MSIGWA  

Next Post

GAVU ATAJA SIFA ZA NAFASI URAIS, UBUNGE, UDIWANI

Next Post
Katibu wa Idara ya Organaizesheni ya CCM, Issa Haji Gavu

GAVU ATAJA SIFA ZA NAFASI URAIS, UBUNGE, UDIWANI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA AAHIDI WAKULIMA DAWA YA KUPULIZIA MIKOROSHO BILA MALIPO

DK. SAMIA AAHIDI WAKULIMA DAWA YA KUPULIZIA MIKOROSHO BILA MALIPO

3 weeks ago
BALOZI DK.  NCHIMBI ATAJA MISINGI YA CCM

BALOZI DK.  NCHIMBI ATAJA MISINGI YA CCM

1 month ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.