• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Makala

DK. NCHIMBI : CCM INAJIVUNIA MTAJI MKUBWA WA WANACHAMA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
August 31, 2025
in Makala, Siasa, Uchaguzi
0
DK. NCHIMBI : CCM INAJIVUNIA MTAJI MKUBWA WA WANACHAMA

MGOMBEA Mwenza wa Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk.Emmanuel Nchimbi

0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NJUMAI NGOTA

MGOMBEA Mwenza wa Urais Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, amesema hadi sasa wanachama nchi nzima wa CCM milioni 13.3 wamejiandikisha katika daftari la kudumu la wapigakura kushiriki Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, mwaka huu.

Amesema hakuna chama kingine chochote Afrika Mashariki na Kati kilichokuwa na nusu ya wanachama wa CCM na hiyo inatokana na rekodi ya Chama kwamba wananchi kukipenda Chama kinachojali maendeleo yao.

Balozi Dk. Emmanuel alisema hayo , alipohutubia katika mkutano wa hadhara uliofanyika uwanja wa Furahisha, uliopo wilayani Ilemela.

“WanaCCM waliojiandikisha ni milioni 13.3, hakuna chama kingine chochote Afrika Mashariki na Kati kinao japo nusu ya wanachama wa CCM na hiyo inatokana na rekodi ya Chama, wananchi wanapenda chama kinachojali maendeleo yao.

“Wananchi wanataka chama kinachotafakari kuhusu maisha yao ya baadaye,  wanataka chama kinachohangaika na kero zao. Chama Cha Mapinduzi kwa kiwango kikubwa kimejithibitisha kuyatekeleza hayo,”alisema.

Balozi Dk. Nchimbi alisema katika viti vya madiwani mkoani humo, Chama kimepita bila kupigwa, hakijapata wagombea katika kata 91, ambapo wamepata wagombea katika kata 90.

Aidha, Dk. Nchimbi alitumia fursa hiyo  kuwaomba  wakazi wa Mwanza kumchagua Rais Dk. Samia, wabunge na madiwani na alitumia fursa hiyo kuwanadi wabunge wa mkoa huo.

Balozi Dk. Nchimbi alimwahakikishia ushindi wa kishindo kutoka kwa wakazi wa Mwanza, kutokana na maendeleo makubwa aliyoyafanya.

Alisema dalili za ushindi wa kishindo kwa CCM zimeanza kuonekana kupitia matokeo ya awali ya wagombea wa CCM kupata ushindi mkubwa wa nafasi za udiwani na ubunge jijini Mwanza.

Alisema kara 90 sawa na zaidi ya asilimia 50 ya kata zote za Mwanza wagombea wa CCM wamepita bila kupingwa. 

Alisema hiyo ni  heshima kubwa kutoka kwa wananchi na hiyo ishara kwamba lOktoba 29, mwaka huu wananchi wataipa CCM ushindi wa kihistoria.

Kwa mujibu wa Balozi Dk. Nchimbi, Mkoa jirani wa Geita una majimbo tisa, majimbo saba hayana wapinzani na CCM imepita bila kupingwa kata 91 kati ya kata 122. 

Alisema wananchi wananchi wameonyesha  kwa vitendo Imani waliyonayo kwa Chama na ni  heshima kubwa kwa chama na wamethamini  kazi kubwa ya maendeleo iliyofanywa. 

Kwa mujibu wa Balozi Dk. Nchimbi, wananchi  hawataki maneno, wanataka matokeo na CCM imeonesha kwa vitendo kwamba inajali, hivyo ushindi wa mapema katika kata na majimbo .

 “Dalili hizi si za kawaida, ni dhihirisho la imani ya wananchi kwa chama chenye misingi ya kazi na utu,” alisema.

Alitoa wito kwa wananchi wote kujitokeza kwa wingi Oktoba 29 na kupiga kura kwa CCM kuhakikisha Tanzania inaendelea kusonga mbele kwa kasi ya maendeleo na uongozi wenye utu na kazi.

MAMBO YATAKAYOTEKELEZWA MWANZA

Alisema katika kipindi cha miaka mitano ijayo wamejipanga kutekeleza miradi ya kimkakati mkoani huo.

Balozi Dk. Nchimbi aliitaja baadhi ya miradi hiyo ambayo watatekeleza katika kipindi cha miaka mitano ni kukamilisha ujenzi wa reli ya kisasa ya SGR kutoka Isaka hadi Mwanza, maji na upatikanaji wa meli mpya mbili.

Alisema Chama kimejipanga kutekeleza miradi mbalimbali katika mkoa huo ikiwemo elimu, afya, umeme na maji kwa kuhakikisha wananchi wanaendelea kunufaika na rasilimali za taifa.

Balozi Nchimbi alisema Mwanza ni kitovu cha maendeleo ya Kanda ya Ziwa kutokana na mchango wake katika kilimo, madini na ufugaji.

MAFANIKIO YALIYOPATIKANA MIAKA MINNE

Alisema kuna mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Rais Dk. Samia, ni ujenzi wa zaidi ya madarasa 4,000, vyuo vipya vya VETA vitatu na vituo vya vyuo vikuu vitatu vimeanzishwa mkoani humo.

Akizungumzia sekta ya maji, alisema asilimia 85 ya wakazi wa Mwanza wanapata maji safi na salama hiyo ni sawa na ongezeko la asilimia asilimia 10, ikilinganishwa na miaka iliyopita ambapo visima na mabwawa mapya yakichimbwa kuongeza upatikanaji.

SEKTA YA AFYA

Mgombea Mwenza wa Urais alisema zimejengwa hospitali mbili mpya, kuwekwa mashine za MRI na digital scan tatu na huduma za afya zikiboreka zaidi.

BARABARA

Balozi Dk. Nchimbi alisema zaidi ya kilometa 300 zimeboreshwa, soko kuu na stendi ya mabasi ya Nyegezi vimekamilika na majosho ya mifugo yameongezwa kutoka 53 hadi 77.

ELIMU

Alisema shule za msingi zimeongezeka kutoka 873 mwaka 2020 hadi 973, sekondari kutoka 219 hadi 308, huku kiwango cha ufaulu kikipanda kutoka asilimia 84 hadi 96.

KUHUSU KUZUIA MAITI

Mgombea Mwenza wa Urias, Balozi Dk. Nchimbi alisema kwa mila za Kiafrika haikubali kuzuia mwili wa marehemu kwenda kuzikwa.

Balozi Dk. Nchimbi alisema siku 100 za kwanza za Mgombea Urais wa Chama, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, ataliondoa na iwapo kutakuwa na deni utatafutwa utaratibu.

DARAJA LA KIGOGO BUSISI

Alisema  Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, alikuta ujenzi wa daraja hilo umefikia asilimia  33 ambapo alihakikisha linakamilika ikiwa ni njia ya kumuenzi mtangulizi wake Hayati Dk. John Magufuli.

NISHATI  YA UMEME

Balozi Dk. Nchimbi alisema mitaa na vijiji vyote vya Mwanza vimeunganishwa na umeme, huku maeneo ya visiwa yakiendelea kupata huduma hiyo.

Pia, kukamilisha uboreshaji wa Uwanja wa Ndege wa Mwanza kwa kuwa na sifa kamilifu  ya kuwa uwanja kimataifa.

“Jambo hili la kukamikisha uwanja limekuwa likiendelea, nataka niwaambie changamoto ndogo zinazotokana na uboreshaji huo tunazifahamu, tutachukua hatua kuhakikisha kwamba, zinaondolewa,”alisema.

Mgombea Mwenza wa Urais alisema mafanikio hayo ni yanatokana na kuwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, anayejali na anayejitahidi kutafuta , kugawanya na kusimamia rasilimali za taifa.

“Hakuna sehemu yoyote ya nchi iliyobaguliwa kwa sababu yoyote, kila sehemu imepata maendeleo kutegemea na mahitaji yaliyopo kutokana na kuwepo kwa wabunge na madiwani wanaotokana na CCM, viongozi wanaotimiza wajibu wao.

“Kipekee tunawapongeza Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, serikali yake na mabaraza la mawaziri, watendaji wa serikali, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, makatibu tarafa , watendaji wa kata wa vijiji, wote hao wamefanya kazi kubwa na viongozi wa CCM katika ngazi zote za usimamizizilishiriki kusimamia kuhakikisha maendeleo ya nchi yetu yanapatikana,”alisema.

Pia, Balozi Dk. Nchimbi aliwashukuru wanaCCM nchi nzima kwa kuhakikisha Chama kinasimamia maendeleo,”alisema.

Previous Post

DK. SAMIA AAHIDI NEEMA ZAIDI GAIRO

Next Post

DK. SAMIA AMETEKELEZA MIRADI MINGI YA MAENDELEO – DK. NCHIMBI

Next Post
DK. SAMIA AMETEKELEZA MIRADI MINGI YA MAENDELEO – DK. NCHIMBI

DK. SAMIA AMETEKELEZA MIRADI MINGI YA MAENDELEO - DK. NCHIMBI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA  AELEZA MAFANIKIO YA UONGOZI WAKE

DK. SAMIA AELEZA MAFANIKIO YA UONGOZI WAKE

1 month ago
DK. SAMIA KUFANYA MKUTANO MKUBWA WA KAMPENI ZA CCM GOMBANI YA KALE

DK. SAMIA KUFANYA MKUTANO MKUBWA WA KAMPENI ZA CCM GOMBANI YA KALE

4 weeks ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.