• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

DK. SAMIA, AHIMIZA WAKULIMA WAJISAJILI KATIKA MFUMO WA RUZUKU YA MBEGU, PEMBEJEO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 4, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
DK. SAMIA, AHIMIZA WAKULIMA WAJISAJILI KATIKA MFUMO WA RUZUKU YA MBEGU, PEMBEJEO
0
SHARES
1
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MUSSA YUSUPH,

Mbeya


MGOMBEA urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan, ametangaza neema kwa wakulima nchini.

Amewataka kujisajili kwa wingi katika mfumo wa ruzuku za mbegu na pembejeo za kilimo, kwani serikali bado ina uwezo wa kutoa ruzuku hiyo kwa wakulima wengi nchini.

Amesema lengo na dhamira yake ni kila Mtanzania aguswe na maendeleo yanayopatikana sekta zote.

Pia, amesisitiza wakulima kutoshirikiana na wahalifu wanaouza pembejeo hizo, kwani mpango wa serikali ni kuongeza wigo wa uzalishaji mazao nchini, hatimaye kuimarisha vipato vyao.

Akihutubia maelfu ya wananchi waliohudhuria mkutano wa kampeni katika Uwanja wa Mlima wa Reli uliopo Mji mdogo wa Mbalizi mkoani Mbeya, Dk. Samia, amesema ruzuku hiyo inatolewa kwa wakulima wote nchini.

“Hadi sasa, mbolea na mbegu za ruzuku, zinagawiwa kwa wakulima nchi nzima. Kuna kila aina ya mbolea za kupandia na kukuzia,” alieleza.
Ameyataja baadhi ya mazao ambayo mbolea na mbegu za ruzuku zinatolewa ni mahindi, mpunga, tumbaku na parachichi.


“Lengo tuzalishe, tujilishe kisha kuuza nje ya nchi. Wakulima endeleeni kujisajili, kwani serikali bado ina uwezo wa kutoa ruzuku.

“Tunzeni namba zenu za siri na msishirikiane na waovu kuuza pembejeo za ruzuku,”  amesisitiza Dk. Samia.

Kuhusu wafugaji, alisema serikali itakamilisha ujenzi wa machinjio ya mifugo ya kisasa, Utengule.

Amesema serikali inaendelea na kampeni ya chanjo na utambuzi wa mifugo, yenye lengo la kuongeza hadhi ya mifugo kutoka Tanzania katika masoko ya kimataifa.

Awali, kabla ya kampeni hiyo, mifugo ya Tanzania, ilikuwa haina soko la uhakika kwa sababu ya kukosa rekodi za chanjo.

Akiwa njiani kwenda Mbalizi, Dk. Samia aliwasalimia wananchi wa eneo la Mlowo na kuwaomba kukipigia kura Chama Cha Mapinduzi.

KAULI YA CHONGOLO

Katibu Mkuu Mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo, amesema ushindi wa Dk. Samia katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu, upo wazi kutokana na utekelezaji mzuri wa miradi ya maendeleo.

Chongolo ambaye pia ni Mratibu wa Kampeni za CCM Nyanda za Juu Kusini, amesema maendeleo makubwa yanayopatikana katika mkoa huo, ni ushahidi wa uongozi mzuri wa Rais Dk. Samia.

Amesema wananchi wa mkoa huo, kwa muda mrefu, walilalamikia kuhusu upanuzi wa barabara kuu kuanzia Igawa – Tunduma kwa njia nne kupunguza msongamano.

Amebainisha kuwa, tayari mkandarasi anaendelea na ujenzi wa barabara hiyo, itakayorahisisha shughuli za kiuchumi.

KIHONGOSI ASHAURI VIJANA

Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Kenani Kihongosi, amewasihi vijana kuwa mstari wa mbele kulinda amani ya nchi.

Amesema kundi hilo muhimu, kamwe lisikubali kuingia katika mtego wa kikundi cha watu wenye dhamira ya kuleta vurugu nchini.
“Vijana wa Tanzania wakiwemo wa Mbalizi, wana wajibu wa kulinda taifa, kwani linawategemea,” amesisitiza.

MGOMBEA UBUNGE MBALIZI

Naye, mgombea Ubunge wa Jimbo la Mbalizi, Patari Shida Patari, alisema mafanikio yaliyopatikana ni matokeo ya uongozi thabiti wa serikali, mshikamano baina ya viongozi na wananchi.

Alieleza kuwa, sekta ya afya, imepata mafanikio makubwa baada ya kupatiwa sh. bilioni sita kutekeleza miradi mbalimbali ya afya.

“Tangu kuanzishwa kwa jimbo mwaka 1980, hakuna hospitali iliyojengwa,  sasa jimbo lina hospitali inayofanya kazi kikamilifu,” ameeleza.

Katika sekta ya maji, alisema sh. bilioni 4.8 zimewekezwa katika mradi wa Ilulu utakaoleta maji safi na salama katika eneo la Mbalizi.

ELIMU

Kuhusu elimu, amesema sh. bilioni 9.3, zimetumika kujenga shule na nyumba za walimu huku sh. bilioni 13.9, zikitumika kujenga madarasa 29 na maabara 14.

Previous Post

SERIKALI YA DK. SAMIA KUIMARISHA UPATIKANAJI UMEME SONGWE

Next Post

DK. MWINYI ATAKA KODI, TOZO NDOGO

Next Post
DK. MWINYI ATAKA KODI, TOZO NDOGO

DK. MWINYI ATAKA KODI, TOZO NDOGO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA BARABARA ZA NDANI KWA KIWANGO CHA LAMI PANGAWE

DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA BARABARA ZA NDANI KWA KIWANGO CHA LAMI PANGAWE

2 weeks ago
DK. NCHIMBI : CCM ITAENDELEA KUMUENZI HAYATI KAWAWA

DK. NCHIMBI : CCM ITAENDELEA KUMUENZI HAYATI KAWAWA

2 weeks ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.