• ePaper
Thursday, June 18, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

SERIKALI YA DK. SAMIA KUIMARISHA UPATIKANAJI UMEME SONGWE

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 4, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
SERIKALI YA DK. SAMIA KUIMARISHA UPATIKANAJI UMEME SONGWE
0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MUSSA YUSUPH,

Songwe

KATIKA kuboresha upatikanaji umeme mkoani Songwe, mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ameahidi kujenga njia ya umeme yenye msongo wa kilovoti 730 itakayokwenda kuimarisha upatikanaji nishati hiyo.

Akihutubia maelfu ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Tunduma mkoani Songwe, Dk. Samia amesema umeme huo pia utauzwa nchini Zambia.

“Serikali imejipanga kutekeleza mradi wa umeme kutoka Iringa – Njombe hadi Tunduma yenye msongo wa kilovoti 730, kati ya hizo kilovoti 400 zitatumika Tunduma na Rukwa huku kilovoti 330 zitakwenda kuuzwa nchini Zambia.

Ameeleza: “Tumeshakamilisha mazungumzo, tumeanza mchakato kujenga njia hii ili umeme ufike kwa uhakika. Hii inakwenda sambamba na uhamasishaji matumizi ya nishati safi kwa sababu umeme pamoja na gesi ni nishati safi,” alieleza.

Dk. Samia ameongeza: “Nataka kuwathibitishia na kuwaahidi, nitaendelea kufanya makubwa katika sekta ya elimu, afya, maji na umeme. Tunakwenda kutoa huduma kwa wananchi, tutaendelea kuongeza shule, elimu bila ada, mikopo kwa wanafunzi wa vyuo na VETA, kujenga vyuo vya VETA kuwawezesha vijana wapate ujuzi na kujiajiri.

Akizungumzia miradi ya maji, amesema serikali yake itahakikisha kila Mtanzania anapata maji safi na salama kama ilivyoelekezwa katika ilani ya uchaguzi.

“Tutaendelea kujenga vituo vya afya na zahanati, tunakwenda kumaliza miradi ya maji lengo kuhakikisha kila Mtanzania apate maji safi na salama kwa asilimia 85 vijijini na asilimia 95 mijini.

Baadhi ya maeneo tumefikia lakini baadhi ya maeneo miradi inaendelea. Umeme tumemaliza vijiji vyote, tupo nusu ya vitongoji na tunakwenda kuunga umeme kila mwananchi afaidike,” amebainisha.

Previous Post

DK. SAMIA NI KIONGOZI MWENYE NGUVU KUIVUSHA TANZANIA – CHONGOLO

Next Post

DK. SAMIA, AHIMIZA WAKULIMA WAJISAJILI KATIKA MFUMO WA RUZUKU YA MBEGU, PEMBEJEO

Next Post
DK. SAMIA, AHIMIZA WAKULIMA WAJISAJILI KATIKA MFUMO WA RUZUKU YA MBEGU, PEMBEJEO

DK. SAMIA, AHIMIZA WAKULIMA WAJISAJILI KATIKA MFUMO WA RUZUKU YA MBEGU, PEMBEJEO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

NMB YAPATA MAFANIKIO MAKUBWA, YAZINDUA MKAKATI WA MIAKA MITANO

NMB YAPATA MAFANIKIO MAKUBWA, YAZINDUA MKAKATI WA MIAKA MITANO

5 months ago
KIPA NIGERIA ASHUSHA PRESHA

KIPA NIGERIA ASHUSHA PRESHA

6 months ago

Popular News

  • WABUNGE: AMANI ISICHEZEWE

    WABUNGE: AMANI ISICHEZEWE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WABUNGE WAIPONGEZA NSSF NA PSSSF KWA KUANZISHA SKIMU YA HIFADHI KWA WALIOJIAJIRI NA UWEKEZAJI WA KIWANDA CHA NGOZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WABUNGE WAPONGEZA UWEKEZAJI KLICL

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAKAGUZI WA CAF WARIDHISHWA NA MAENDELEO YA VIWANJA VYA AFCON 2027

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MKAKATI KUDHIBITI VIFO WAJAWAZITO WAANIKWA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?