• ePaper
Friday, May 15, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

DK. SAMIA NI KIONGOZI MWENYE NGUVU KUIVUSHA TANZANIA – CHONGOLO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 4, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
DK. SAMIA NI KIONGOZI MWENYE NGUVU KUIVUSHA TANZANIA – CHONGOLO
0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MUSSA YUSUPH,

Songwe

KATIBU Mkuu Mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo, amesema CCM kimemchangua Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kugombea Urais kwa sababu ni kiongozi mwenye nguvu ya kuivusha nchi salama.

Chongolo ambaye pia ni mgombea Ubunge katika Jimbo la Makambako mkoani Njombe, amesema Rais Dk. Samia ametekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM (2020 – 2025) kwa mafanikio makubwa.

Akizungumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika viwanja vya Shule ya Msingi Tunduma mkoani Songwe, Chongolo amesema Watanzania wapo tayari kumpigia kura za kishindo katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29 mwaka huu.

“Chama kimemsimamisha Rais Samia kupeperusha bendera kwenye uchaguzi mkuu kwasababu ana nguvu ya kuivusha nchi salama. Nguvu uliyonayo ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025 ambayo umeitekeleza vizuri na kwa weledi. Kwa uliyoyafanya huna haja ya kupiga kampeni, nenda kapumzike mambo ya ukanda huu (nyanda za juu kusini) utayaona katika matokeo baada ya Oktoba 29 mwaka huu,” amesisitiza.

“Mwaka 2020/21, hakukuwa na ruzuku ya pembejeo lakini kutokana na uamuzi mkubwa wa Rais Samia kuwajali wakulima ili wasibebe mzigo, imefanya wananchi kuwa na kazi ya kulima ambapo sasa kuna ziada ya chakula,” amebainisha.

Kuhusu sekta ya afya, amesema wananchi wa Songwe wameendelea kupata huduma za afya baada ya imarishaji wa sekta hiyo kwa kila hospitali ya wilaya kujengwa jengo la huduma za dharura.

Pia, Chongolo ambaye aliwahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Songwe, amesema Rais Dk. Samia amewezesha watoto wa Kitanzania kupata elimu bila kikwazo baada ya kuwezesha upatikanaji elimu hadi kidato cha sita bila ada.

Vilevile, amesema Dk. Samia ameifungua Songwe kwa kujenga barabara ya Isongole – Ileje inayojengwa kwa gharama ya sh. bilioni 79 na ile ya kuunganisha Mkoa wa Mbeya kupitia Wilaya ya Kyela ambako kazi inaendelea.

Kadhalika, amesema serikali inajenga barabara ya Mlowo – Kamsamba ambayo ilishapata mkandarasi pamoja na barabara ya Mbeya – Songwe kupitia Mbalizi.

Katibu mkuu huyo mstaafu amesema Rais Dk. Samia ameimarisha mifumo ya ukusanyaji mapato ambapo kituo cha forodha cha Tunduma kimeongeza ukusanyaji mapato kutoka sh. bilioni 139 hadi kufikia sh. bilioni 204 kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

Previous Post

TCU YAFUNGUA DIRISHA UDAHILI AWAMU YA PILI

Next Post

SERIKALI YA DK. SAMIA KUIMARISHA UPATIKANAJI UMEME SONGWE

Next Post
SERIKALI YA DK. SAMIA KUIMARISHA UPATIKANAJI UMEME SONGWE

SERIKALI YA DK. SAMIA KUIMARISHA UPATIKANAJI UMEME SONGWE

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

RAIS DK. SAMIA KUNG’ARA AU

RAIS DK. SAMIA KUNG’ARA AU

3 months ago
WIZARA YA VIWANDA YAZALISHA AJIRA LUKUKI

WIZARA YA VIWANDA YAZALISHA AJIRA LUKUKI

1 month ago

Popular News

  • KIHONGOSI AKEMEA ‘WANAOVIMBA’ CCM

    KIHONGOSI AKEMEA ‘WANAOVIMBA’ CCM

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MARUFUKU KUZUIA WANAFUNZI MITIHANI KISA ADA – DK. MWIGULU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI WA FEDHA AFUNGUA MKUTANO WA KIMATAIFA WA FORODHA ZANZIBAR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TANZANIA KUENDELEA KUIMARISHA USHIRIKIANO WA FORODHA KIKANDA – CG MWENDA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • HAKIKISHENI GESI YENU INAPIMWA KABLA YA KUNUNUA – KIHULLA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?