• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

UWANJA WA BENJAMIN MKAPA WAFIKIA 90%

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 3, 2025
in Burudani, Michezo
0
UWANJA WA BENJAMIN MKAPA WAFIKIA 90%
0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na VICTOR MKUMBO

UKARABATI wa Uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam umefikia asilimia 90% kukamilika hivi sasa.

 Kwa mujibu wa Mratibu wa Viwanja nchini, Milinde Mahona ukarabati wa Uwanja wa Benjamin Mkapa, umefikia asilimia 90 kukamilika.

Alisema hivi sasa zimebakia asilimia 10 kuhakikisha uwanja huo unakamilika na ambapo unatarajiwa kutumika katika michuano mbalimbali ikiwemo Kombe la Mataifa Afrika (AFCON 2027).

“Hivi sasa Uwanja wa Benjamin Mkapa tayari umeshakamilka kwa asilimia 90 na kwamba zimebakia asilimia 10.

“Ukarabati unakwenda vizuri tuna imani utakamilika kwa wakati kwani ni moja ya viwanja vitakavyotumika katika michuano ya AFCON 2027 ambapo Tanzania tutakuwa wenyeji kwa ushirikiano wa nchi za Kenya na Uganda,” alisema Mahona.

Alisema ukarabati wa uwanja huo umefanyika katika maeneo mbalimbali yakiwemo uwanja (pitch), kufunga viti vipya, kufunga taa ndani na nje na sehemu ya kukaa waandishi wa habari.

Alisisitiza kwa upande wa ujenzi wa Uwanja wa kisasa wa mpira wa soka Arusha, hivi sasa unandelea kufanyika kwa kasi ambapo umefikia asilimia 66.

Alisema awali Oktoba, mwaka huu ujenzi wa uwanja huo ulikuwa umefikia asilimia 63.5.

Uwanja huo ambao upo katika eneo la Olomoti, Arusha ukikamilika unatarajiwa kuwa na uwezo wa kuchukua watazamaji 30,000.

“Ujenzi wa Uwanja Arusha unaendelea kwa kasi ambapo hivi sasa umefikia asilimia 66.

Alisema uwanja huo utamilika kwa wakati kuhakikisha unatumika katika fainali za michuano AFCON 2027 na mashindano mbalimbali.

“Mafundi wanaendelea kufanya kazi kwa kasi na hivi sasa ujenzi wa uwanja wa Arusha umeshafikia asilimia 66.

“Hivi sasa mafundi wameshaanza kuchimba eneo la kuchezea mpira ‘pich’ huku maeneo mengine yakiwa tayari yamekamilika yakiwemo majukwaa ya watazamaji.

“Mbali ya kuanza kuchimba eneo la kuchezea, maeneo mengine ambayo yanafanyiwa kazi kwa ubunifu ni paa la uwanjani, ufungaji wa miundombinu ya umeme, zimamoto, TEHAMA na kuweka mabomba,” alisema.

Mratibu Mahona, alisema kukamilika kwa uwanja huo utalenga kuongeza miundombinu ya michezo nchini na kupanda kwa hadhi kutokana na ubora wake.

“Pia mafundi wanaendelea kufanya kazi kwa bidii huku nje ya uwanja ujenzi ukiendelea ikiwemo maeneo ya kuegeshea magari,” alisema.

Aliongeza kwa upande wa Uwanja wa soka wa Dodoma, hivi sasa wameshaanza kusafisha eneo na baadaye ujenzi utaanza mara moja.

Ujenzi wa Uwanja wa Arusha, Dodoma na ukarabati wa Benjamin Mkapa na Uhuru ni juhudi za Serikali chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kuhakikisha michezo inafanyika katika miundombinu bora zaidi.

Previous Post

MAGOLI AFUNGUKA SIMBASC

Next Post

SIMBASC NJIA HII HAPA MAKUNDI KIMATAIFA

Next Post
SIMBASC NJIA HII HAPA MAKUNDI KIMATAIFA

SIMBASC NJIA HII HAPA MAKUNDI KIMATAIFA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

KOCHA YANGA AFUNGUKA

KOCHA YANGA AFUNGUKA

2 months ago
AFCON 2025 KINAWAKA KATIKA VIWANJA HIVI

AFCON 2025 KINAWAKA KATIKA VIWANJA HIVI

4 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?