• ePaper
Wednesday, June 24, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

DK. MWIGULU ABAINI ‘MADUDU’ MENGINE

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
February 18, 2026
in Habari, Kitaifa
0
DK. MWIGULU ABAINI ‘MADUDU’ MENGINE
0
SHARES
10
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba, amesema anataka kuona kila fedha inayotolewa kwa miradi ya maendeleo, inatumika kama ilivyokusudiwa.

Amesema serikali haiwezi kuvumilia kuona watendaji wenye dhamana, hawafuatilii matumizi ya fedha na kusababisha miradi kushindwa kutekelezwa kwa viwango na ubora kwa manufaa ya wananchi.

Dk. Mwigulu, alisema hayo, alipozungumza na wananchi baada ya kuzindua mitambo ya kuzalisha hewa tiba ya oksijeni katika Hospitali ya Wilaya ya Lushoto mkoani Tanga.

Waziri Mkuu, aliwasisitiza watumishi wa umma kuhakikisha anatekeleza majukumu yao ipasavyo na si vinginevyo.

“Tunataka watu wasilale ofisini, ninyi ni watumishi wa serikali, fedha zikiletwa zikafanye kazi iliyokusudiwa,” alisema.

Dk. Mwigulu, alisema hayo wakati akihoji kukosekana ubora na viwango vya majengo, risiti za malipo, kutofanyika kwa kodi ya zuio, kukosekana cheti cha ubora wa mabati, matofari na saruji katika baadhi ya shule za msingi wilayani humo.

Mradi huo wa kuzalisha hewa tiba ya oksijeni, uliogharimu sh. milioni 526.8, una uwezo wa kuzalisha mitungi 120 ya kilo 50 kwa siku.

Mitambo hiyo imeiwezesha halmashauri hiyo kutolazimika kusafirisha mitungi ya oksijeni hadi jijini Tanga, umbali wa takribani kilometa 175 kwa ujazaji.

Hadi sasa, mtambo umezalisha mitungi 1,440 ya hewa tiba (oksijeni) ya kilo 50 na mitungi 200 ya kilo 15.

Aidha, Waziri Mkuu alionya tabia ya baadhi ya watendaji wa serikali kuwa na utaratibu wa kuzoea matatizo ya wananchi.

Previous Post

MRADI ZIWA VICTORIA MBIONI KUKAMILIKA

Next Post

RAIS DK. SAMIA AMLILIA STEVEN HIZA

Next Post
RAIS DK. SAMIA AMLILIA STEVEN HIZA

RAIS DK. SAMIA AMLILIA STEVEN HIZA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. KIKWETE ASHIRIKI MAZISHI YA KITAIFA YA RAIS MSTAAFU MOGAE WA BOTSWANA, AKIMWAKILISHA RAIS DK. SAMIA

DK. KIKWETE ASHIRIKI MAZISHI YA KITAIFA YA RAIS MSTAAFU MOGAE WA BOTSWANA, AKIMWAKILISHA RAIS DK. SAMIA

1 month ago
MAAGIZO YA DK. MWINYI KWA WATUMISHI Z’BAR

MAAGIZO YA DK. MWINYI KWA WATUMISHI Z’BAR

8 months ago

Popular News

  • YANGA, AZAM FC HAIJAISHA HADI IISHE

    YANGA, AZAM FC HAIJAISHA HADI IISHE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA MIAKA 30 TRA, YAGUSA WABUNGE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • HATUTAVUMILIA UHUJUMU WA MIRADI – NDEJEMBI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA KUZINDUA JENGO LA BILIONI 17/- KCMC

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • BODABODA WAKINGIWA KIFUA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?