• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

JESCA MAGUFULI AWATAKA SHINYANGA KUIAMINI CCM

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 6, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
JESCA MAGUFULI AWATAKA SHINYANGA KUIAMINI CCM

MBUNGE mteule kupitia Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Jesca Magufuli

0
SHARES
8
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NJUMAI NGOTA,

Kahama

MBUNGE mteule kupitia Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Jesca Magufuli, ametaka wananchi wa Wilaya ya Kahama, mkoani Shinyanga, kuendelea kukiamini na kukipa ushindi wa kishindo Chama katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu.

Jesca, mtoto wa Rais wa Awamu ya Tano, Hayati Dk. John Magufuli, amesema hayo, katika Kata ya Kagongwa, wilayani Kahama, aliposimamishwa kutoa salamu kwa wakazi wa eneo hilo na mgombea mwenza wa urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi.

“Wananchi wa Shinyanga, tunaposema tuendelee kukiamini Chama chetu, tunamaanisha. Chama Cha Mapinduzi, ni Chama ambacho kimetekeleza Ilani ya mwaka 2020-2025 kwa vitendo.

“Wanashinyanga ni mashahidi mmeona miradi mikubwa ya miundombinu, barabara, reli ya kisasa ya kiwango cha kimataifa (SGR), maji na nishati, kubwa zaidi katika sekta ya madini imeendelea kuwanufaisha vijana wa Shinyanga,”amesema.

Jesca amesema mafanikio hayo ni matokeo ya uongozi thabiti wa CCM chini ya Mgombea Urais wa CCM, Dk. Samia Suluhu Hassan katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wake.

“Tuendelee kukiamini Chama, katika Ilani ya mwaka 2025-2030 kimeahidi mambo mengi kwa vijana ikiwemo kuongeza ajira, suala la mikopo ambayo itaendelea kutolewa,”amesema.

Pia, Jesca amesema serikali imeendelea kutoa elimu kwa wajasiriamali, kutafuta masoko ya nje na ndani kwa kuwapatia mitaji

“Itakapofi ka Oktoba 29, mwaka huu tuendelee kukiamini Chama chetu, kura nyingi kwa madiwani , wabunge na kura nyingi zaidi kwa mgombea wetu, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan,”amesema.

Naye, Mgombea Ubunge wa Jimbo la Msalala, Mabula Magangila, amesema CCM imefanya kazi kubwa katika utekelezaji wa Ilani ya Chama.

Mabula amesema madarasa, vituo vya afya, barabara ya lami kutoka Kahama kwenda Kakola, hivyo wanatarajia makubwa zaidi katika sekta ya uzalishaji.

Previous Post

WASIRA AVUNJA MAKUNDI CCM ARUSHA, MANYARA

Next Post

YANGA YARIDHISHWA UUZAJI WA JEZI

Next Post
YANGA YARIDHISHWA UUZAJI WA JEZI

YANGA YARIDHISHWA UUZAJI WA JEZI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

1 day ago
MAELFU WAFURIKA UZINDUZI WA KAMPENI ZA CCM DAR

MAELFU WAFURIKA UZINDUZI WA KAMPENI ZA CCM DAR

2 months ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.