• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

DK. NCHIMBI ATOA AHADI YA KONGANI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 11, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
DK. NCHIMBI ATOA  AHADI YA KONGANI

MGOMBEA Mwenza wa Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi

0
SHARES
0
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NJUMAI NGOTA,

Katavi

MGOMBEA Mwenza wa Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, amesema katika kipindi cha miaka mitano ijayo, iwapo watapewa ridhaa ya kuongoza nchi, wataanzisha kongani za viwanda vya ndani katika kila wilaya.

Aliyasema hayo, Kata ya Katumba, iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, mkoani Katavi, aliposimama kuwasalimia wananchi wa eneo hilo, akiwa njiani kwenda Halmashauri ya Wilaya Mlele, Jimbo la Kavuu.

Katika mkutano huo wa hadhara, Dk. Nchimbi, aliwaomba wananchi kumchagua Mgombea Urais wa CCM, Dk. Samia Suluhu Hassan, katika Uchaguzi Mkuu, utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu.

Pia, alieleza utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2020-2025 na kuinadi mpya ya mwaka 2025-2030 kwa wananchi.

Alisema mpango huo ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya CCM na kila wilaya, itatambuliwa kwa uzalishaji mahsusi, kuanzisha viwanda vinavyolingana na rasilimali zilizopo katika maeneo husika.

“Kwa kutambua umuhimu wa viwanda katika Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), tumekubaliana kwamba, miaka mitano inayokuja, tutakuwa na kongani ya viwanda vya ndani kwa maana ya kwamba, kila wilaya katika nchi yetu, tutaitazama inazalisha nini kwa wingi, kitu gani kinapotea bure na kitu gani kinakosa soko.

“Tukishajua, kila maeneo katika nchi yetu, tutapanga viwanda kutegemea na maeneo yaliyopo,” alisema.

Balozi Dk. Nchimbi, alitolea mfano mazao kutoka Mpanda na Katavi, yatasindikwa na bidhaa hizo kufikishwa maeneo mengine, ikiwemo Wilaya ya Nsimbo.

Alisema hiyo itasaidia kuhakikisha bidhaa za Watanzania hazikosi soko.

Mbali na viwanda, Balozi Dk. Nchimbi, alisema dhamira ya Serikali ya CCM ni kuendeleza sekta za afya, elimu, kilimo, maji na miundombinu.

AFYA

Balozi Dk. Nchimbi, alisema katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, wanakusudia kujenga vituo vipya vya afya vitatu na zahanati tatu, kuimarisha utoaji wa huduma hizo karibu zaidi na wananchi.

ELIMU

Kuhusu elimu, alisema katika miaka mitano ijayo, wamedhamiria kujenga shule za sekondari 11, kuimarisha miundombinu ya madarasa kwa kuhakikisha watoto wanasoma katika mazingira bora zaidi.

Alisema katika bajeti ya elimu, itaendelea kuongezwa kuhakikisha kila Mtanzania mwenye nia ya kusoma, anapata fursa hiyo bila vikwazo.

KILIMO

Kwa mujibu wa Balozi Dk. Nchimbi, serikali ijayo, inatarajia kuongeza maradufu bajeti ya ruzuku ya mbolea na mbegu, kwa kutambua Watanzania wengi hutegemea kilimo.

UFUGAJI

 Akizungumzia ufugaji, alisema sekta hiyo, itaendelea kuimarishwa kwa kuongeza chanjo za mifugo, majosho, mabwawa na minada ya kuuza mifugo.

UVUVI

Alisema katika kipindi cha miaka mitano ijayo, serikali ya CCM itawekeza katika uvuvi wa kisasa kwa kutumia vizimba, mabwawa, kuimarisha upatikanaji wa vifaa na masoko kwa wavuvi wadogo.

MADINI

Kuhusu sekta ya madini, Dk. Nchimbi, alisema serikali imeongeza zaidi ya asilimia 50 ya bajeti ya utafiti wa madini huku ikielekeza nguvu katika kuwapa leseni wachimbaji wadogo hususan vijana kuwawezesha kiuchumi.

MAJI

Akielezea upatikanaji wa maji, alisema wamejipanga  kuanzisha miradi ya maji 16 ikijumuisha visima virefu na mabwawa, lengo likiwa ni kuondoa na upungufu wa maji katika maeneo yenye changamoto.

BARABARA

Dk. Nchimbi, alisema katika miaka hiyo ijayo, wanatarajia kuimarisha miundombinu ya barabara kwa kuhakikisha inafanya kazi na zinapitika masika na kiangazi.

Alitumia fursa ya mkutano huo, kuwaomba wananchi kumchagua Mgombea Urais wa CCM, Dk. Samia, wabunge na madiwani kwa kura za kishindo.

Akiwa katika mkutano wa hadhara wa kampeni za Chama uliofanyika Kijiji cha Inyonga, Halmashauri ya Wilaya Mlele, mkoani Katavi, Dk. Nchimbi, alisema wanatarajia kujenga kongani ya viwanda wilayani na mikoani

Previous Post

DK. SAMIA AELEZA MAFANIKIO YA UONGOZI WAKE

Next Post

WALIOONGOZA KURA ZA MAONI WAPEWA JUKUMU

Next Post
WALIOONGOZA KURA ZA MAONI WAPEWA JUKUMU

WALIOONGOZA KURA ZA MAONI WAPEWA JUKUMU

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

JESCA MAGUFULI AWATAKA SHINYANGA KUIAMINI CCM

JESCA MAGUFULI AWATAKA SHINYANGA KUIAMINI CCM

1 month ago
MBETO : HAKUNA WA KUZUIA USHINDI WA CCM ZANZIBAR 2025-2030

MBETO : HAKUNA WA KUZUIA USHINDI WA CCM ZANZIBAR 2025-2030

1 month ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.