• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

NLD KUUNDA SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 12, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
NLD KUUNDA SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA
0
SHARES
0
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na REHEMA MAIGALA

CHAMA cha National League for Democracy (NLD), kimesema iwapo kitapata ridhaa ya kuongoza nchi, kitahakikisha kinaunda serikali ya umoja wa kitaifa, kwa lengo la kujenga mshikamano.

Mgombea urais kupitia chama hicho, Hassan Doyo, alisema hayo, alipokuwa akihojiwa katika kipindi cha Kiongozi 2025 kinachorushwa na Kituo cha Utangazaji cha TBC.

“Chama chetu kikipata ridhaa ya kuongoza nchi, kitahakikisha kinaunda serikali ya umoja wa kimataifa, kwa lengo la kujenga mshikamano wa kweli,” aliahidi.

Aidha, Doyo alisema kwa kuwa Tanzania haina uhasama na nchi yoyote duniani, chama chao kitaendeleza mazuri yaliyofanywa na serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Pia, alisema serikali ya chama chao kitaimarisha uhusiano mzuri wa ndani ya nchi, ndiyo maana kila wakati kinawahimiza Watanzania kudumisha amani, mshikamano na umoja.

Mbali na hayo, Doyo alisema takwimu zinaonesha zaidi ya asilimia 70 ya Watanzania ni wakulima, lakini bajeti ya kilimo ni asilimia 10, hivyo wakipata ridhaa watahakikisha wakulima wanapewa mbegu bora bure, kutafutiwa masoko na kuboreshwa miundombinu ya barabara kuwawezesha kusafirisha mazao yao moja kwa moja sokoni.

Akizungumzia sekta ya elimu, Doyo aliahidi chama chao kitajenga vituo vya elimu ya teknolojia  kila halmashauri.

“Vituo hivyo vitakuwa vya kipekee barani Afrika na vitakusanya vijana kutoka maeneo yote ya halmashauri husika, kuwawezesha kujifunza, kufanya utafiti na kutoa ushauri wa kitaalamu kwa serikali,” alisema.

Aliongeza kupitia vituo hivyo vijana hawatakuwa wasikilizaji tu, bali watashiriki mabadiliko ya teknolojia.

Doyo alisema NLD imejipanga kuboresha huduma bora za kijamii, zikiwemo afya, ajira, elimu na miundombinu ya barabara.

Kuhusu dhamira yake ya kugombea urais, Doyo alisema anataka kulitumikia taifa kwa misingi ya uzalendo, haki na maendeleo.

“Nikipata nafasi ya kuwa rais, serikali yangu itaongozwa na misingi mitatu ambayo ni Uzalendo, Haki na Maendeleo. 

“Nitahakikisha nchi hii inakuwa na maendeleo, huku nikiwahimiza Watanzania kupendana na kuwa na umoja wa kizalendo ulioasisiwa na waasisi wa nchi  hii,” aliahidi.

Previous Post

CCM YAELEZA KUONGEZEKA MBOLEA YA RUZUKU

Next Post

BILIONI 499/- ZAPATIKANA KUPITIA UTALII

Next Post
BILIONI 499/- ZAPATIKANA KUPITIA UTALII

BILIONI 499/- ZAPATIKANA KUPITIA UTALII

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA AAHIDI NEEMA MPYA KWA WAKULIMA

DK. SAMIA AAHIDI NEEMA MPYA KWA WAKULIMA

2 months ago
SERIKALI YA DK. SAMIA KUIMARISHA UPATIKANAJI UMEME SONGWE

SERIKALI YA DK. SAMIA KUIMARISHA UPATIKANAJI UMEME SONGWE

1 month ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.