• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

MSIGWA : DK. SAMIA AMETHIBITISHA UWEZO WAKE WA UONGOZI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 15, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
MSIGWA : DK. SAMIA AMETHIBITISHA UWEZO WAKE WA UONGOZI
0
SHARES
21
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NJUMAI NGOTA,

Tanga

KADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mchungaji Peter Msigwa, amesema Dk. Samia Suluhu Hassan,amethibitisha uwezo mkubwa kwa kuleta mageuzi chanya katika kipindi cha miaka minne na nusu ya uongozi wake.

Pia, Chama kimejidhihirisha kuwa na sera madhubuti, itikadi imara na falsafa makini, kuleta maendeleo kwa Watanzania.

Mchungaji Msigwa, alisema hayo Uwanja wa Cleopa Msuya, wilayani Mwanga, mkoani Kilimanjaro, katika mkutano wa kampeni za Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu.

“Tumeshuhudia ujenzi wa zahanati, upatikanaji majisafina salama, barabara za lami na uboreshaji wa huduma zaafya na elimu.

“Mama Samia ameonesha weledi wa hali ya juu namapenzi ya dhati kwa nchi yetu,” alisema.

Aidha, katika kuonesha dhamira ya kuendeleza kasi yamaendeleo, Mchungaji Msigwa, alisema Dk. Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, kuwa Mgombea Mwenza huku akieleza kuwa, ni kiongozi mwenye uwezomkubwa, uzoefu na uchapakazi.

“Kama zawadi kubwa kwa kazi nzuri ya Dk. Samia, nikumpa kura za ndiyo kwa wingi.
“Pia, tunamletea Dk. Nchimbi kuwa, Mgombea Mwenza. Huu ni uteuzi makini, unaoonesha nia ya kuendeleza mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita,” alisema.

MAFANIKIO YA SERIKALI

Msigwa aliwataka wananchi waendelee kuiamini CCM kwa sababu, mafanikio yaliyopatikana, yanazungumza yenyewe kama kuongezeka vituo vya afya, kupungua kwavifo vya watoto wachanga, ujenzi wa madarasa unaosaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi, kuongezeka kwa barabara za lami na huduma za jamiivijijini na mijini.

“Mkiulizwa kwa nini CCM tena? Waambieni tunaona maendeleo kwa macho yetu.

“Tunaona shule zikijengwa, tunapunguza ujinga, tunalima kwa weledi, tunafanya kazi kwa ujuzi kwa sababu yauongozi madhubuti wa Dk. Samia,” alisisitiza.

MSIGWA ATAKA KURA TATU KWA CCM

Msigwa aliwaomba wakazi wa Mwanga, kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura, Oktoba 29, mwaka huu nakuhakikisha wanapiga kura zote tatu kwa CCM kwa Dk. Samia, Mbunge wa Jimbo la Mwanga, Dk.  Ngwalu Maghembe na udiwani kwa wagombea wa CCM katika kata zote.

“Hakikisha unapiga kura ya ndiyo kwa Dk. Samia, kuraya ndiyo kwa Dk. Maghembe kuwa Mbunge na kura zakutosha kwa madiwani wa CCM. Tufanye kazi hii kwaumoja na ari mpya,” alisema.

Previous Post

MRATIBU ACT ATOBOA SIRI KUJIUNGA CCM

Next Post

NCHIMBI : NIDHAMU NGUZO KUIMARISHA DEMOKRASIA

Next Post
NCHIMBI : NIDHAMU NGUZO KUIMARISHA DEMOKRASIA

NCHIMBI : NIDHAMU NGUZO KUIMARISHA DEMOKRASIA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MSIGWA : DK. SAMIA AMETHIBITISHA UWEZO WAKE WA UONGOZI

MSIGWA : DK. SAMIA AMETHIBITISHA UWEZO WAKE WA UONGOZI

4 weeks ago
VYAMA 18 Z’BAR VYASAINI FOMU KUELEKEA UCHAGUZI

VYAMA 18 Z’BAR VYASAINI FOMU KUELEKEA UCHAGUZI

2 months ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.