• ePaper
Sunday, May 31, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

MRATIBU ACT ATOBOA SIRI KUJIUNGA CCM

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 15, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
MRATIBU ACT ATOBOA SIRI KUJIUNGA CCM
0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na WAANDISHI WETU,

Kigoma

MRATIBU na mwanachama wa ACT-Wazalendo mkoani Kigoma, Said Bakema, ametoboa siri ya kukihama chama hicho na kujiunga Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Amesema utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa muda mfupi aliyofanya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan mkoani humo ndiyo sababu iliyomfanya kuhamia CCM.

Bakema alieleza hayo mkoani Kigoma katika mkutano wa kampeni za mgombea Urais CCM, Dk. Samia ambapo alisisitiza amejiunga Chama tawala kwa ridhaa yake.

“Ardhi hii ina kitovu cha wazazi wangu, nasimama kuwaambia kwa ridhaa yangu nimeamua kuachana na chama nilichokuwepo na kujiunga CCM mchana kweupe,”alisema Bakema.

Alisema chama alichotoka alikuwa mgombea ubunge jimbo la Kigoma Kusini mwaka 2015 huku 2020 akiwa mratibu wa Mkoa wa Kigoma katika uchaguzi mwaka huu.

“Leo nasema ACT kwaherini naingia CCM rasmi, sijashawishiwa na mtu yeyote, bali kilichonishawishi ni matokeo ya muda mfupi ambayo umeyafanya wewe (Dk. Samia), naachana na chama ambacho mtu akiamka na hasira siku hiyo wote mnakuwa na hasira au akiamka ana furaha mnakuwa na furaha wote,” alieleza.

Bakema alisema amehamia CCM sababu ni Chama kinachoendeshwa kitaasisi badala ya kufanya mambo kwa danadana.

“Nimekuja nikiwa najiamini nimeingia katika chama imara, kinachoendeshwa na mtu imara na tutafika mbali,”alisema Bakema.

Aliwaambia watanzania na wana-Kigoma, Dk. Samia ni mgombea urais wa CCM, ambaye siyo katika Tanzania tuu hata Afrika Mashariki ndiye mgombea anayekubalika.

“Nina faraja kujiunga chama kinachoongozwa na mtu mwenye maono makubwa ya kuwatumikia watanzania na mimi nataka niwatumikie watanzania. Kigoma umetusaidia sana katika kipindi kifupi, matokeo makubwa yameonekana,” alisema mratibu huyo.

Alitoa mfano Kigoma ilikuwa abiria akipanda basi saa moja jioni anafika Dar es Salaam saa moja jioni maana yake anatumia saa nyingi njiani kinyume na hivi sasa.

“Siko peke yangu nina watu wengi zaidi wapo tayari kunifuata ni matokeo ya kazi uliyofanya ningewaleta hapa kusingekuwa na sehemu ya kukaa, nitanya kazi usiku na mchana lengo langu ushindi utakaoupata na mimi niongeze asilimia kadhaa ya kura,” aliongeza Bakema.

Awali, Naibu Katibu Mkuu CCM Bara, John Mongela alisema wameona waanze na Bakema, ambaye walikutana naye njiani walipokuwa wakienda katika mkutano wa kampeni ya uchaguzi utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu.

“Tuliona tupo katika mawindo tunatafuta tembo Oktoba 29, lakini tumekutana na mbogo njiani tukasema tuanze naye wakati tunaelekea huko mbele,” alibainisha Mongela.

Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Kenani Kihongosi alisema Bakema ana wafuasi zaidi ya 200 ambao watakabidhiwa kwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kigoma.

Previous Post

WASIRA : MAENDELEO YALIYOPO, UTHIBITISHO WA UONGOZI MAHIRI

Next Post

MSIGWA : DK. SAMIA AMETHIBITISHA UWEZO WAKE WA UONGOZI

Next Post
MSIGWA : DK. SAMIA AMETHIBITISHA UWEZO WAKE WA UONGOZI

MSIGWA : DK. SAMIA AMETHIBITISHA UWEZO WAKE WA UONGOZI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA AFUNDA VIJANA

DK. SAMIA AFUNDA VIJANA

7 months ago
DK. MWINYI : YAJAYO YANAFURAHISHA KASKAZINI UNGUJA

DK. MWINYI : YAJAYO YANAFURAHISHA KASKAZINI UNGUJA

8 months ago

Popular News

  • SERENGETI BOYS KILA KONA, RAIS SAMIA AWAPA MILIONI 500/-

    SERENGETI BOYS KILA KONA, RAIS SAMIA AWAPA MILIONI 500/-

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAS: UTUNZAJI MAZINGIRA AJENDA YA KIPAUMBELE KWA MKOA WA MWANZA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • UPELE UMEPATA MKUNAJI STARS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ‎ RAIS DK. SAMIA: POLISI MSIDHARAU TAARIFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWIGULU ATETA NA WAZIRI MKUU WA CONGO BRAZZAVILLE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?