• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

DK. SAMIA AAHIDI FURSA ZAIDI KWA VIJANA NCHINI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 19, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
DK. SAMIA AAHIDI FURSA ZAIDI KWA VIJANA NCHINI

MGOMBEA Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan

0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MUSSA YUSUPH, 

UNGUJA

MGOMBEA Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema amedhamiria kujenga taifa imara, litakalofungua fursa zaidi kwa vijana kufanya kazi zitakazowaingizia kipato, kujiegemea kiuchumi.

Dk. Samia alisema hayo alipozungumza na maelfu ya wananchi katika mkutano wa kampeni za Uchaguzi Mkuu za CCM, uliofanyika Uwanja wa Hamburu, Jimbo la Nungwi Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Alieleza kufikia hatua hiyo, lazima kila mwananchi hususan vijana wawe na shughuli zitakazowapa kipato.
“Na hii ndiyo kazi inayoendelea kufanywa na CCM, kuandaa mazingira rafiki kwa vijana kuwa na shughuli za kufanya, kila mmoja awe na kipato mweyewe, asimame, ajitegemee.

“Kuweka mazingira kwa vijana wetu kuwa na shughuli za kujishughulisha kuingiza kipato, kila mmoja ainue ustawi wa maisha yake, ndiyo tunasema, Kazi na Utu, Tunasonga Mbele,” alisisitiza Dk. Samia.

WAGOMBEA UBUNGE WAZUNGUMZA

Wakizungumzia maendeleo aliyopatikana pande zote za Muungano, baadhi ya wagombea ubunge kutoka majimbo mbalimbali visiwani hapa, walisema kazi kubwa imefanyika kuimarisha amani, utulivu, hivyo kuchochea maendeleo kila sekta.

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chaani, Ayoub Mohammed Mahmoud, alisema wananchi wanawapongeza Rais Dk. Samia na mgombea urais wa Zanzibar kupitia CCM, Dk. Hussein Ali Mwinyi kwa kuongoza mapambano ya maendeleo katika miaka mitano.

Alisema katika mapambano hayo, wamefaulu kuwaletea maendeleo wananchi wa pande zote za Muungano.

“Upande wa elimu ya juu, mimi ni mlezi wa TAHLISO (Shirikisho la Wanafunzi wa Elimu ya Juu) nimeshuhudia uamuzi wetu wa kuhakikisha mnatoa fedha za mikopo kwa wanafunzi wa diploma umesaidia wazazi.

“Uamuzi huu umesaidia watoto wa familia za kinyonge kupata elimu. Nyie ni majemedari, wapo waliojaribu kututikisa nyie hamkutikisika. Mmekuwa mstari wa mbele kutuongoza,” alieleza.

Kwa upande wake, mgombea ubunge wa Jimbo la Donge, Sadifa Juma Khamis, alisema katika jimbo hilo tayari CCM ina uhakika wa kura za kutosha.

“Wananchi wamesema kura zote wanakwenda kumpigia Dk. Samia kwa upande wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Dk. Mwinyi kwa Zanzibar. Hii ni kwa sababu mara ya kwanza miradi mikubwa ya maendeleo inatekelezwa kwa pamoja.

“Katika sekta ya afya kuna hospitali za kisasa kama hoteli za nyota tano. Kwa wajasiriamali tulizindua Soko la Chuini, juzi kuna Mzungu alipotea akidhani anaingia hotelini kumbe ni soko,” alisema.

Alisema hizo ndizo salamu za wananchi wa Zanzibar kwa sababu Ilani ya Uchaguzi ya CCM imetekelezwa kwa zaidi ya asilimia 100.

Mbunge wa Viti Maalumu, Riziki Pembe Juma, alisema Dk. Samia na Mwinyi wanapaswa kuungwa mkono kwa kasi ya maendeleo yaliyopatikana.

“Ninawaomba viongozi wangu mtembee kifua mbele, sisi wanawake tutapita kichochoro kwa kichochoro, mitaa kwa mitaa kuzisaka kura, viongozi hawa tulionao wanatosha na chenji inabaki,” alisisitiza.

Previous Post

KISHINDO CHA DK. NCHIMBI RUVUMA

Next Post

DK. MIGIRO ATAJA SABABU ZITAKAZOMPA USHINDI DK. SAMIA

Next Post
DK. MIGIRO ATAJA SABABU ZITAKAZOMPA USHINDI DK. SAMIA

DK. MIGIRO ATAJA SABABU ZITAKAZOMPA USHINDI DK. SAMIA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

KISHINDO CHA DK. NCHIMBI RUVUMA

KISHINDO CHA DK. NCHIMBI RUVUMA

4 weeks ago
WASIRA : MAENDELEO YALIYOPO, UTHIBITISHO WA UONGOZI MAHIRI

WASIRA : MAENDELEO YALIYOPO, UTHIBITISHO WA UONGOZI MAHIRI

1 month ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.