• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

CCM YAAHIDI KILIMO CHA BIASHARA KWA WAKULIMA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 26, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
CCM YAAHIDI KILIMO CHA BIASHARA KWA WAKULIMA

MGOMBEA Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan

0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na   MUSSA YUSUPH,

LINDI

MGOMBEA Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema mkakati wa serikali yake pindi atakapopata ridhaa ya kuliongoza Taifa ni kukifanya kilimo kiwe cha kibiashara.

Dk. Samia aliyasema hayo katika mkutano wa kampeni uliofanyika Jimbo la Ndanda mkoani Mtwara, ambapo alisema lengo la serikali ni kukuza kilimo kiwe cha kibiashara.

Alisema hatua hiyo itawawezesha wakulima kunufaika kupitia shughuli zao za kilimo.

“Kupitia pembejeo za ruzuku kwa kweli mmetenda haki na uzalishaji umekua, sasa tutaendelea kutoa ruzuku kwenye pembejeo na pia kuwawezesha kuendelea kuzalisha zaidi kwa sababu lengo letu ni kufanya kilimo biashara,” alisema.

Pia, aliwaahidi wananchi kwamba serikali itaunganisha Ndanda na Mji wa Masasi kwa barabara ya lami.

“Ahadi yangu ni kwamba tutaboresha barabara kwa kiwango cha lami na changarawe ndani ya Jimbo la Ndanda na zile za kuifungua Ndanda. Lengo letu ni kuinganisha Ndanda na Mji wa Masasi ili mazao yasafirishwe kwa haraka sana,” alieleza.

Dk. Samia alitumia fursa hiyo kuwapongeza wananchi wa Ndanda kwa kuzalisha mazao ya chakula na biashara kwa wingi.

Alisema katika sekta ya elimu, ataendelea kutoa elimu bila malipo lakini pia elimu jumuishi ili watoto wenye mahitaji maalumu waweze kupata elimu.

“Natambua kwamba hapa Ndanda kuna shule maalumu, niwaahidi tunaenda kuboresha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji ikiwemo kujenga karakana ili vijana watoke na ujuzi,” alisisitiza.

Kwa upande wa maji, Dk. Samia alisema miaka mitano iliyopita serikali yake ilitoa sh. bilioni 13 na kutekeleza miradi ya maji 63.

Akiwa Jimbo la Mtama, Dk. Samia alitoa wito kwa wananchi pindi watakapovuna mazao yao watunze akiba ya fedha kujiunga bima ya afya kwa wote.

Previous Post

DK. SAMIA ASEMA UMEME WA KUTOSHA UMEPELEKWA VIJIJINI

Next Post

SIMBU APANDISHWA CHEO

Next Post
SIMBU APANDISHWA CHEO

SIMBU APANDISHWA CHEO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

“Wasichana milioni mbili wanufaika na elimu ya stadi za maisha

2 months ago
DK. SAMIA ASEMA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA VIPO TAYARI KULINDA NCHI WAKATI WA UCHAGUZI MKUU

DK. SAMIA ASEMA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA VIPO TAYARI KULINDA NCHI WAKATI WA UCHAGUZI MKUU

4 weeks ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.