• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Burudani

YANGA, SINGIDA, MLANDEGE MZIGONI TENA KIMATAIFA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 27, 2025
in Burudani, Habari, Kimataifa, Michezo
0
YANGA, SINGIDA, MLANDEGE MZIGONI TENA KIMATAIFA
0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
Na AMINA KASHEBA


WAWAKILISHI watatu wa nchi katika michuano ya kimataifa, leo wanashuka dimbani katika viwanja tofauti kuwania nafasi ya kucheza hatua ya pili ya mtoano.


Wawakilishi hao ni Yanga ya Dar es Salaam na Mlandege ya Zanzibar zinazoshiriki Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) pamoja na Singida Black Stars kutoka Singida iliyopo katika Kombe la Shirikisho Afrika (CAFCC).


Katika ratiba hiyo, Yanga itarudiana na Wiliete de Benguela ya Angola katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam (Saa 11:00 jioni) wakati Mlandege ikicheza na Ethiopian Coffee ya Ethiopia katika Uwanja wa New Amaan Complex, Unguja (Saa 10:15 jioni).


Yanga itaingia katika mtanange huo ikiwa na mtaji wa mabao 3-0 wakati Mlandege ikiwa imefungwa mabao 2-0 katika mechi ya kwanza.


Katika CAFCC, Singida Black Stars itachuana na Rayon Sports saa 1:00 usiku katika Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam huku ikiwa na mtaji wa bao 1-0 iliyoupata ugenini nchini Rwanda.


Akizungumza maandalizi ya mchezo wa leo, Kocha wa Yanga, Romain Folz, alisema amejipanga vizuri kupata ushindi ambao utaisogeza mbele miamba hiyo katika hatua ijayo.


"Mchezo utakuwa mgumu lakini wachezaji wangu wamejipanga kuhakikisha tunapata ushindi ambao utatuweka katika nafasi nzuri katika michuano," alisema.


Kocha huyo alisema ana imani na kikosi chake kutokana na kila mchezaji wake kuwa bora, hivyo anawaomba mashabiki kujitokeza kwa wingi katika mchezo huo.


Kocha Mkuu wa Wiliete, Bruno Ferry alisema mchezo huo utakuwa mgumu lakini wamejipanga vizuri kupata matokeo ambayo yatawaweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele.


"Tuna uwezo wa kucheza vizuri zaidi ya mechi ya kwanza, tumeshatambua makosa yetu hivyo tutapambana kuhakikisha tunapaata matokeo," alisema.


Wakati huo huo , Ofisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliwataka mashabiki waklabu hiyo kujitokeza kwa wingi katika mchezo huo muhimu licha ya kupata ushindi mkubwa katika mechi ya kwanza.


Katika mchezo huo viingilio vitakuwa ni sh. 3,000 katika eneo la mzunguko, VIP C sh. 10,000, VIP B sh. 20,000 na VIP A itakuwa sh. 30,000.
Previous Post

MAJALIWA : MRADI GESI YA LNG KUIKOMBOA LINDI KIUCHUMI

Next Post

DK. SAMIA AFICHUA FAIDA MAPINDUZI YA VIWANDA

Next Post
DK. SAMIA AFICHUA FAIDA MAPINDUZI YA VIWANDA

DK. SAMIA AFICHUA FAIDA MAPINDUZI YA VIWANDA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. MWINYI AFUNGUKA MALENGO SERA YA NISHATI

DK. MWINYI AFUNGUKA MALENGO SERA YA NISHATI

1 month ago
DK. SAMIA AAHIDI MAGEUZI MAKUBWA YA KILIMO

DK. SAMIA AAHIDI MAGEUZI MAKUBWA YA KILIMO

1 month ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.