• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

MTANDAO WA GESI KINYEREZI HADI CHALINZE, SASA WANUKIA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 29, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
MTANDAO WA GESI KINYEREZI HADI CHALINZE, SASA WANUKIA

MGOMBEA Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan

0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

MUSSA YUSUPH

MGOMBEA Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema kama CCM ikipewa ridhaa ya kuliongoza taifa, serikali yake imejipanga kujenga mtandao wa gesi kutoka Kinyerezi hadi Chalinze mkoani Pwani.

Amesema mtandao huo wa nishati ya gesi, utakuwa na matoleo kuelekea maeneo ya uwekezaji ya TAMCO, Zegereni, Kwala na Bagamoyo, kwa sasa mkandarasi mshauri, anaendelea kufanya tathmini ya njia ya kupitisha bomba hilo.

Dk. Samia, aliyasema hayo alipohutubia maelfu ya wananchi katika mkutano wa kampeni za Uchaguzi Mkuu katika uwanja wa Sabasaba mjini Kibaha mkoani Pwani.

Aliongeza kuwa ujio wa gesi utazidi kuvutia uwekezaji mkoani Pwani kwani viwanda vitaendeshwa kwa gharama nafuu zaidi na bidhaa zitakazozalishwa zitapungua bei.

Dk. Samia, alisema miongoni mwa ahadi katika ilani ya CCM ni kuchukua hatua kupunguza gharama za vifaa vya ujenzi nchini, kuwezesha wananchi wa kipato cha chini, kujenga nyumba bora za kisasa kwa gharama nafuu.

Alibainisha kuwa, mwelekeo wa serikali ni kuendeleza mpango wa ujenzi makazi bora kwa bei nafuu.
Vilevile, alisema serikali yake, itaendelea kuboresha makazi mijini kwa kuhakikisha makazi, nyumba na majengo yote yanarasimishwa kwa kupimwa, kupangwa na kumilikishwa.

Kuhusu miradi ya maji, alisema serikali imeendelea kutoa fedha katika mkoa huo, kuhakikisha miradi mbalimbali ya maji inakamilishwa
“Katika kukabiliana na changamoto ya maji tulileta sh. bilioni 187.3 katika mkoa huu. Alibainisha kuwa, miradi hiyo, imeanza kutekelezwa itakayohudumia kata 53 za Wilaya ya Rufiji, Kibiti, Mkuranga na Kisarawe.

Pia, alisema mradi wa maji Kwala, utanufaisha maeneo ya Kwala, Bandari Kavu na maeneo ya viwanda.

Alisema mradi wa maji Pangani, utatatua changamoto ya maji Kata ya Pangani na maeneo ya Msufini, Lulanzi na TAMCO.

Mbali na miradi hiyo, alisema miradi mingine midogo yenye kuhusisha upanuzi wa mtandao wa maji kutoka Mlandizi, Bokomlegela, Janga, Mtongani na Kawawa itatekelezwa.

Alisema serikali itajenga mradi wa maji katika eneo la viwanda wenye gharama ya sh. bilioni 10.9, ambao utanufaisha maeneo tofauti ya mkoa huo.

Previous Post

MGOMBEA URAIS AAHIDI UTEKELEZAJI BARABARA KIBAHA – CHALINZE – MORO

Next Post

CHINI YA DK. SAMIA, USTAWI UMEONEKANA – DK. MIGIRO

Next Post
CHINI YA DK. SAMIA, USTAWI UMEONEKANA – DK. MIGIRO

CHINI YA DK. SAMIA, USTAWI UMEONEKANA – DK. MIGIRO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA ATANGAZA HATUA ZA MWISHO UTEKELEZAJI MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA

DK. SAMIA ATANGAZA HATUA ZA MWISHO UTEKELEZAJI MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA

2 weeks ago
SIMBU APANDISHWA CHEO

SIMBU APANDISHWA CHEO

3 weeks ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.