• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

CHINI YA DK. SAMIA, USTAWI UMEONEKANA – DK. MIGIRO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 29, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
CHINI YA DK. SAMIA, USTAWI UMEONEKANA – DK. MIGIRO

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Asha-Rose Migiro

0
SHARES
8
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

MUSSA YUSUPH

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Asha-Rose Migiro, ameeleza kuwa, Tanzania chini ya uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, ustawi wa wananchi umeonekana.

Dk. Asha – Rose, aliyasema hayo alipohutubia maelfu ya wananchi katika mkutano wa kampeni za Uchaguzi Mkuu katika Uwanja wa Sabasaba mjini Kibaha mkoani Pwani.

Alisema kuwa, Mkoa wa Pwani ni kituo cha biashara na utalii kupitia vivutio mbalimbali vilivyokuwa sehemu ya masimulizi kupitia filamu ya Tanzania Royal Tour.
Aliwaomba wananchi kujitokeza kwa wingi Oktoba 29, mwaka huu kumpigia kura Dk. Samia, wabunge na madiwani wa CCM, kwani kufanya hivyo ni kupigia kura maendeleo na utu wa Mtanzania.

Mratibu wa Kampeni Kanda ya Pwani, ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu, Halima Mwamuya, alisema hadi sasa, ushindi mkubwa utapatikana katika mikoa hiyo.
Alieleza kuwa, wagombea ubunge na udiwani katika kanda hiyo yenye kujumuisha mikoa ya Pwani, Tanga na Morogoro wanakubalika.

Halima, alisema alikutana na kundi la wazee ambao nao wamemhakikishia kwamba, wanamuunga mkono Dk. Samia katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Pwani, Mwinshehe Mlawu, alisema wananchi wa mkoa huo, wanamshukuru Dk. Samia, kwani hakuna sekta yenye kumnufaisha mwanadamu ambayo haijaguswa.

Alisema upatikanaji pembejeo za mazao ya korosho na ufuta zimechangia kuongeza vipato vya wakulima.

Hata hivyo, aliomba barabara ya kwenda mikoa ya kusini eneo la Kokoto Mbagala kwani kipande hicho kimeendelea kuleta changamoto kwa wananchi.
Vilevile, aliomba ujenzi wa kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoa ya kusini.

Previous Post

MTANDAO WA GESI KINYEREZI HADI CHALINZE, SASA WANUKIA

Next Post

DK. NCHIMBI ATANGAZA NEEMA YA MAJI UBUNGO

Next Post
DK. NCHIMBI ATANGAZA NEEMA YA MAJI UBUNGO

DK. NCHIMBI ATANGAZA NEEMA YA MAJI UBUNGO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

AWESO AAGIZA MGAWO MAJI UWE SHIRIKISHI

AWESO AAGIZA MGAWO MAJI UWE SHIRIKISHI

4 months ago
SIMBA QUEENS MENO NJE, YANGA YALIA NA WACHEZAJI

SIMBA QUEENS MENO NJE, YANGA YALIA NA WACHEZAJI

4 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?