• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Burudani

MOROCCO ATAJA KILICHOIPONZA STARS

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 9, 2025
in Burudani, Habari, Michezo
0
MOROCCO ATAJA KILICHOIPONZA STARS
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na AMINA KASHEBA

KOCHA timu ya taifa ‘Taifa Stars’, Hemedi Sulemain ‘Morocco’,  amesema sababu ya kushindwa kupata ushindi katika mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia 2026 dhidi ya Zambia ni wachezaji wake kukosa umakini wa kutumia nafasi.

Juzi, Stars ilifungwa bao 1-0 dhidi ya Zambia katika mchezo wa mwisho wa kuwania kufuzu Kombe la Dunia, uliofanyika dimba la New Amaan Complex, Zanzibar.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa mchezo huo, kocha huyo alisema wachezaji wake kutokuwa makini katika umaliziaji ndiyo sababu ya kushindwa kupata ushindi.

” Bado umakini wa eneo la umalizaji kupata mabao limekuwa tatizo katika kikosi.

“Tunalijua suala la kutokufunga ila baada ya muda mfupi litakaa vizuri, tutalifanyia utatuzi, kwa sababu kupata mchezaji wa kufunga kama Mbwana Samatta ni ngumu lakini tuna imani tutapata,” alisema.

Kocha huyo alisema hivi sasa wachezaji waliopo katika kikosi wanapaswa kupata mechi mbalimbali kwa lengo la kupata uzoefu hadi ikifika michuano ya AFCON 2025, ana imani kikosi kitakuwa vizuri katika eneo la kufunga.

“Ni suala la muda, kwa wachezaji waliopo katika kikosi wakipata mechi mbalimbali za kucheza nina imani watakaa sawa hadi ikifika AFCON tutakuwa vizuri katika kupata mchezaji ambaye atakuwa mzuri katika eneo la umaliziaji,” alisema.

Katika kundi E, kuwania kufuzu Kombe la Dunia, Taifa Stars imemaliza nafasi ya tatu kwa alama 10, kinara Morocco ina pointi 21, Niger inafuatia kwa alama 12, Zambia ina pointi tisa wakati Congo Brazaville ikiwa na pointi moja.

Previous Post

DK. SAMIA, MWINYI WAMELETA MAENDELEO NCHINI – DK. NCHIMBI

Next Post

DK. SAMIA ATAJA SIFA ZA VIONGOZI WANAOFAA

Next Post
DK. SAMIA ATAJA SIFA ZA VIONGOZI WANAOFAA

DK. SAMIA ATAJA SIFA ZA VIONGOZI WANAOFAA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA, AHIMIZA WAKULIMA WAJISAJILI KATIKA MFUMO WA RUZUKU YA MBEGU, PEMBEJEO

DK. SAMIA, AHIMIZA WAKULIMA WAJISAJILI KATIKA MFUMO WA RUZUKU YA MBEGU, PEMBEJEO

1 month ago
CCM YAELEZA KUONGEZEKA MBOLEA YA RUZUKU

CCM YAELEZA KUONGEZEKA MBOLEA YA RUZUKU

1 month ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.