• ePaper
Saturday, November 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home AFYA

COMORO YAENDELEA KUDUMISHA USHIRIKIANO NA TANZANIA KATIKA SEKTA YA AFYA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 6, 2025
in AFYA, Habari, Kitaifa
0
COMORO YAENDELEA KUDUMISHA USHIRIKIANO NA TANZANIA KATIKA SEKTA YA AFYA
0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na Mwandishi Wetu,
Dar es Salaam

MAKAMU wa Rais wa Comoro ambaye pia ni Spika wa Bunge la Taifa hilo, Moustadroine Abdou, amesema Serikali ya Comoro itaendelea kudumisha ushirikiano wa kidugu na Tanzania, hususan katika sekta ya afya ambayo imekuwa mfano wa mafanikio ya ushirikiano wa kikanda.

Akizungumza alipotembelea Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORCI) jijini Dar es Salaam, baada ya kuwasili nchini kumwakilisha Rais wa Comoro katika sherehe za uapisho wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, Abdou amesema amevutiwa na maendeleo makubwa ya huduma za afya nchini.

“Nimefika Tanzania kwa mara ya tatu. Nchi hii ni tulivu, yenye amani na watu wenye upendo. Nawapongeza kwa uchaguzi mzuri na kumpata kiongozi bora, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan,” amesema Abdou.

Ameongeza kuwa ushirikiano kati ya Tanzania na Comoro katika sekta ya afya umeendelea kuimarika, ambapo madaktari wa Tanzania wamekuwa wakitoa huduma na mafunzo nchini humo, sambamba na wananchi wa Comoro kufika Tanzania kupata matibabu kutokana na vifaa vya kisasa na miundombinu bora iliyopo.

Kwa upande wake, Balozi wa Tanzania nchini Comoro, Said Yakoub, amemshukuru Makamu wa Rais huyo kwa kuitembelea ORCI na kueleza kuwa amekuwa balozi mzuri wa kuitangaza Tanzania kwa wananchi wa Comoro kutokana na mapenzi makubwa aliyonayo kwa nchi hii.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa ORCI, Dk. Diwani Msemo, amesema uhusiano wa Tanzania na Comoro ni wa kihistoria na umejikita katika misingi ya urafiki wa watu na serikali zao, ambao sasa unaendelea kuimarishwa kupitia sekta mbalimbali ikiwemo afya.

“Tuna furaha kuona viongozi wa Comoro wanatambua mchango wa Tanzania katika afya na kuendeleza ushirikiano huu wa kidugu,” amesema Dk. Msemo.

Previous Post

MBETO : RAIS DK. SAMIA, MWINYI WAMEAPA KULINDA WATANZANIA NA AMANI YA TAIFA

Next Post

NECTA : TUMETOA MATOKEO KWA NAMBA KULINDA TAARIFA BINAFSI ZA WANAFUNZI

Next Post
NECTA : TUMETOA MATOKEO KWA NAMBA KULINDA TAARIFA BINAFSI ZA WANAFUNZI

NECTA : TUMETOA MATOKEO KWA NAMBA KULINDA TAARIFA BINAFSI ZA WANAFUNZI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

CCM YAONESHA KUKUBALIKA, MAELFU WAMIMINIKA

CCM YAONESHA KUKUBALIKA, MAELFU WAMIMINIKA

2 months ago
DK. NCHIMBI : DK. SAMIA KIONGOZI WA MAJAWABU

DK. NCHIMBI : DK. SAMIA KIONGOZI WA MAJAWABU

1 month ago

Popular News

  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAAGIZO MATATU KWA DK. NCHEMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NI MARIDHIANO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.