• ePaper
Sunday, January 11, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

MWAKINYO APEWA MBINU YA KUMCHAPA MNIGERIA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 17, 2025
in Burudani, Michezo
0
MWAKINYO APEWA MBINU YA KUMCHAPA MNIGERIA
0
SHARES
9
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na AMINA KASHEBA

WADAU wa ngumi za kulipwa nchini, wamempa mbinu bondia Hassan Mwakinyo za kushinda katika pambano lake dhidi ya Stanley Eribo wa Nigeria.

Wakizungumza jijini Dar es Salaam kwa nyakati tofauti, Wadau hao walisema Mwakinyo anatakiwa kuweka mbele nidhamu ya mchezo, kujiamini na kutomdharau mpinzani wake.

Pambano hilo lisilo la ubingwa raundi 10 uzito wa kati linatarajiwa kufanyika Desemba 26, mwaka huu Ukumbi wa Warehouse uliopo Masaki, jijini Dar es Salaama

Bondia mkongwe,Rashidi Matumla, alisema jambo la kwanza Mwakinyo anapaswa kufanya mazoezi kwa bidii kwa kuwa, yatampa nguvu ya kushinda pambano hilo.

“Anapaswa kujiamini, kuwa na nidhamu ya mchezo na kutomdharau mpinzani wake kwa sababu ana rekodi nzuri,” alisema Matumla.

Mkongwe huyo aliongeza kuwa Mwakinyo anatakiwa kufuata mafunzo aliyopewa na makocha wake.

Bondia wa zamani wa kick boxing, Japhet Kaseba, ambaye ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mabondia wa Ngumi za Kulipwa Tanzania, alimtaka Mwakinyo kucheza kwa kujiamini.

“Kila kitu kinawezekana kwa kuwa rekodi hiyo ya Mnigeria inaweza kufutwa kama hajawahi kupigwa ni muda wa Mwakinyo kupambana na kuweka rekodi ya kumpiga Eribo.

“Kitu kingine anatakiwa kujiamini, kuwa na nidhamu na kutomdharau mpinzani wake maana na yeye anaenda kujipanga kwa lengo la kupata ushindi ugenini,” alisema Kaseba.

Naye bondia, Feriche Mashauri, alisema ana imani  Mwakinyo atafanya vizuri kwa kumpiga na kumaliza pambano mapema, japo awamu hii kuna ugumu kutokana na Mwakinyo kukaa nje ya ulingoni muda mrefu.

Katika rekodi ya mabondia hao,Mwakinyo amecheza jumla ya mapambano 27, ameshinda 24 na kupoteza mapambano matatu ajawahi kutoka sare.

Bondia Eribo amepanda ulingoni mara 19, ameshinda mapambano 18 na kutoka sare pambano moja hajawahi kupigwa.

Mwakinyo mara ya mwisho kupanda ulingoni ilikuwa Novemba 16, mwaka 2024, alipomchakaza kwa TKO raundi ya tisa katika pambano la kutetea mkanda wake wa Ubingwa wa WBO dhidi ya bondia, Daniel Lartey kutoka Ghana.

Previous Post

YANGA, SIMBA NI VIKUMBO

Next Post

SERIKALI MATUMAINI KIBAO AFCON

Next Post
SERIKALI MATUMAINI KIBAO AFCON

SERIKALI MATUMAINI KIBAO AFCON

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

FADLU AWAONGEZEA ‘DOZI’ MASTAA WAKE

FADLU AWAONGEZEA ‘DOZI’ MASTAA WAKE

4 months ago
KOCHA TAIFA STARS UHAKIKA KWA NIGER

KOCHA TAIFA STARS UHAKIKA KWA NIGER

4 months ago

Popular News

  • RAIS DK. SAMIA ATAJA SABABU MABADILIKO BARAZA LA MAWAZIRI

    RAIS DK. SAMIA ATAJA SABABU MABADILIKO BARAZA LA MAWAZIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DIAMOND KUTOKA KIVINGINE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KOCHA SIMBA AJITETEA, MASHABIKI WACHARUKA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WADAU MICHEZO WAMTUMIA SALAMU WAZIRI MAKONDA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMANZI WATOTO WAKIFIA NDANI YA SWIMMING POOL

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?