• ePaper
Monday, January 19, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

KOCHA SIMBA AJITETEA, MASHABIKI WACHARUKA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 10, 2026
in Burudani, Habari, Michezo
0
KOCHA SIMBA AJITETEA, MASHABIKI WACHARUKA
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

BAADA ya kuondolewa katika michuano ya Kombe la Mapinduzi, Kocha wa Simba, Steve Barker amesema sababu ya kupoteza bao 1-0 katika mchezo dhidi ya Azam FC ni kuwachelewa kambini kwa wachezaji wake, mashabiki wameonekana kuchukizwa na kiwango cha kikosi hicho.

Simba, ilikubali kufungwa bao 1-0 dhidi ya Azam, katika mchezo wa nusu fainali uliofanyika Uwanja wa Amaan Complex, Zanzibar.

Aliwataja baadhi ya wachezaji waliochelewa kuingia kambini kujiandaa na Kombe la Mapinduzi ni Jean Ahoua, Elie Mpanzu na Jonathan Sowah.

Akizungumza baada ya mchezo huo, Kocha Barker alisema kuwa mbali na hilo wachezaji wake walitengeneza nafasi lakini walishindwa kuzitumia ipasavyo kupachika mabao.

Alisema kuwa lengo lao lilikuwa ni kupata matokeo mazuri na kutinga fainali ya michuano hiyo msimu huu, lakini ilishindikana.

Alisema anakwenda kukisuka vyema kikosi chake kwa maandalizi ya michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara na Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL).

Kocha huyo alisema kuwa siku chache alizokaa na kikosi chake ameona nini anatakiwa kuanza nacho ili aweze kukijenga na kuwa bora kwa ajili ya mashindano yajayo.

“Tumepoteza lakini sababu kubwa ni baadhi ya wachezaji kushindwa kuingia kambini kwa wakati kipindi cha kufanya maandalizi.

“Pia tulitengeneza nafasi lakini tulishindwa kuzitumia ipasavyo kupachika mabao wavuni, tunakwenda kujipanga upya kuhakikisha tunafanya vyema katika michuano ya Ligi na CAFCL,” alisema.

Naye Kocha wa Azam FC, Florent Ibenge alisema kuwa haikuwa rahisi kuifunga Simba, hivyo anawapongeza vijana wake kwa kazi kubwa waliyoifanya.

Alisema kuwa licha ya kukutana na ugumu katika mchezo huo lakini walibaki katika malengo yao ambayo wameyatimiza na hivi sasa watapambana kubeba taji.

 “Ilikuwa mechi ngumu, kwani haikuwa rahisi kupata ushindi mbele ya Simba lakini niwapongeze wachezaji wangu kwa kazi kubwa waliyoifanya hadi kufikia malengo ya kutinga fainali ya mashindano haya,” alisema Ibenge.

Wakati kocha wa Simba akijitetea, mashabiki wa klabu hiyo wamesisitiza kwamba hawajaridhishwa na kiwango cha wachezaji wao.

Shabiki aliyejitambulisha kwa jina la Dokta Moo alisema kuwa, amechukizwa na kipigo walichokipata kutoka Azam FC kwani wamefungwa na wachezaji vijana wa U20.

Alisema kuwa katika kikosi cha Azam wachezaji wachache walitoka kikosi cha kikubwa huku kikijumuisha wengi wa U20, hivyo hajaridhishwa na kiwango cha Simba katika michuano hiyo.

“Bado tuna safari kubwa ndani ya kikosi chetu, tuliingia katika mchezo huo wachezaji wakionekana hawapo tayari kwa ajili ya ushindi, sijaridhishwa na timu, tunahitaji mabadiliko makubwa na ya haraka,” alisema Dokta Moo.

Naye baba mzazi wa Ofisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe, ambaye ni shabiki wa Simba, Shabani Kamwe alisema kuwa hali ni mbaya ndani ya kikosi chao bado wanahitaji kujipanga zaidi ili kushinda katika mechi kubwa.

Alisema kuwa timu yao haina muunganiko unaoweza kusababisha wachezaji kupambana na kupata matokeo mazuri hasa katika mechi kubwa.

“Kikosi chetu bado hakipo vizuri, tunahitaji uboreshaji mkubwa kwa hali kikosi kilivyo hatuwezi kufika mahali popote.

“Hatuna muunganiko wa wachezaji wanaoweza kupambana kuamua matokeo chanya, tunahitaji suluhisho la mapema ili kuinusuru timu yetu msimu huu,” alisema.

Azam msimu huu imetinga fainali ya michuano hiyo kwa mara saba baada ya 2012, 2013, 2017, 2018, 2019, 2022 na sasa 2026.

Katika misimu saba imebeba mataji matano mwaka 2012, 2013, 2017, 2018 na 2019.

Previous Post

WADAU MICHEZO WAMTUMIA SALAMU WAZIRI MAKONDA

Next Post

DIAMOND KUTOKA KIVINGINE

Next Post
DIAMOND KUTOKA KIVINGINE

DIAMOND KUTOKA KIVINGINE

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

SIMBA, NSINGIZINI BALAA ZITO CAFCL

SIMBA, NSINGIZINI BALAA ZITO CAFCL

3 months ago
SIMBACHAWENE ATAJA MAAGIZO YA RAIS DK. SAMIA

SIMBACHAWENE ATAJA MAAGIZO YA RAIS DK. SAMIA

3 weeks ago

Popular News

  • KOFANE ALIVYOANDIKA HISTORIA CAMEROON AFCON MSIMU HUU

    KOFANE ALIVYOANDIKA HISTORIA CAMEROON AFCON MSIMU HUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MIGIRO KATIBU MKUU WA  KWANZA MWANAMKE NA MIKAKATI YA KUIMARISHA MASHINA KATIKA MITAA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SAFARI KUMALIZA CHANGAMOTO UMEME IRINGA, DODOMA YAIVA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TANZANIA YAINGIA 10 BORA KUVUTIA UWEKEZAJI AFRIKA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AMREJESHA MAKONDA AFCON

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?