• ePaper
Sunday, January 11, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

RAIS DK. SAMIA: HAKUNA MAENDELEO BILA AMANI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 17, 2025
in Habari, Kitaifa
0
RAIS DK. SAMIA: HAKUNA MAENDELEO BILA AMANI

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan

0
SHARES
0
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amelitaka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), kuendelea kuimarisha ulinzi kwa kuwa, ulinzi imara ndiyo msingi wa amani na maendeleo ya nchi.

Amesema hakuna maendeleo bila amani, hivyo JWTZ inategemewa kuendeleza usalama na amani, wananchi waendelee kushiriki kikamilifu shughuli za kila siku.

Rais Samia aliyasema hayo mkoani Tanga, alipozungumza katika Mkutano wa Tisa wa Mkuu wa Majeshi (CDF) na Makamanda, uliyofanyika Shule ya Kijeshi ya Ulinzi wa Anga (SKUA).

“Hakuna maendeleo bila amani, sasa Jeshi la Wananchi wa Tanzania likiwa chombo muhimu cha ulinzi wa ndani na nje ya nchi, linategemewa kuendeleza usalama na amani, wananchi waendelee kushiriki kikamilifu shughuli za maendeleo.

Alisema mbali na kuwekeza katika mafunzo na mazoezi ya kijeshi, pia ushirikiano na vyombo vingine vya ulinzi na usalama ni muhimu katika kudhibiti matishio ya usalama ukiwemo ugaidi.

Rais Samia, alifafanua kila chombo kina majukumu yake, lakini dhima kuu ni ulinzi wa uhuru, mamlaka na heshima ya nchi.

Vilevile, Rais Samia, alisema muda mrefu, JWTZ imeendelea kuwa mfano katika ukanda wa Afrika na Dunia kwa ujumla kutokana na weledi, nidhamu na utii.

Pia, aliwapongeza wanajeshi wanawake kwa kushiriki katika fani mbalimbali za urubani, uhandisi, udaktari na maeneo mbalimbali ya kiteknolojia.

Alisema wanawake wanaendelea kuthibitisha uwezo katika maeneo mbalimbali ya kijeshi, zikiwemo fani za urubani.

“Wanawake wanaendelea kuthibitisha uwezo katika maeneo mbalimbali ya kijeshi, katika fani za urubani, nilipokwenda kuangalia ndege zile za mafunzo tulizonunua, nimekuta marubani wanawake wako pale,”alisema.

Previous Post

TANZANIA YAPONGEZWA UTEKELEZAJI MKATABA WA UMOJA WA MATAIFA DHIDI YA RUSHWA

Next Post

YANGA, SIMBA NI VIKUMBO

Next Post
YANGA, SIMBA NI VIKUMBO

YANGA, SIMBA NI VIKUMBO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. MWINYI ACHUKUA FOMU ZANZIBAR, AHADHARISHA CHUKI

DK. MWINYI ACHUKUA FOMU ZANZIBAR, AHADHARISHA CHUKI

4 months ago
DK. MIGIRO AJA KIVINGINE CCM

DK. MIGIRO AJA KIVINGINE CCM

2 days ago

Popular News

  • RAIS DK. SAMIA ATAJA SABABU MABADILIKO BARAZA LA MAWAZIRI

    RAIS DK. SAMIA ATAJA SABABU MABADILIKO BARAZA LA MAWAZIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DIAMOND KUTOKA KIVINGINE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KOCHA SIMBA AJITETEA, MASHABIKI WACHARUKA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WADAU MICHEZO WAMTUMIA SALAMU WAZIRI MAKONDA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMANZI WATOTO WAKIFIA NDANI YA SWIMMING POOL

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?