• ePaper
Thursday, July 30, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

BARKER, IBENGE VITA YA MBINU ‘MZIZIMA DERBY’

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 8, 2026
in Burudani, Kitaifa, Michezo
0
BARKER, IBENGE VITA YA MBINU ‘MZIZIMA DERBY’
0
SHARES
10
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

WAKATI Simba na Azam FC zikichuana katika dabi ya Mzizima, makocha Steve Barker na Florent Ibenge, wanatarajiwa kuwa na vita kubwa ya mbinu katika mtanange huo utakaopigwa leo visiwani Zanzibar.

Simba itachuana na Azam FC saa 2:15 usiku katika Uwanja wa New Amaan Complex, Unguja katika mtanange wa nusu fainali ya Kombe la Mapinduzi 2026.

Wekundu hao wa Msimbazi wametinga nusu fainali baada ya kuongoza kundi C kwa alama sita wakati Azam FC ikishika nafasi ya kwanza kundi A kwa pointi saba.

Akizungumzia mchezo huo Kocha wa Simba, Barker raia wa Afrika Kusini, alisema amekiandaa vyema kikosi chake na ataingia na mbinu bora kuhakikisha wanashinda.

Muafrika Kusini huyo alikiri mtanange huo utakuwa mgumu lakini pia utakuwa muhimu kwa lengo la kuiimarisha timu yake.

“Ni mchezo muhimu kwetu kuhakikisha tunapata ushindi, najua tulipoteza mchezo wa mwisho, hivyo ninahitaji kukijenga kikosi chetu kiwe bora na chenye ushindani mkubwa tufunge magoli na kutinga fainali ili turudishe furaha ya Wanasimba,” alisema Barker.

Pia, Barker alisema mchezo huo utampa picha ya kujua ubora wa kikosi chake hivi sasa katika kucheza na timu kubwa hususan baada ya michuano hiyo watakabiliwa na michezo migumu katika Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Esperance ya Tunisia, Stade Malien ya Mali na Petro Atletico ya Angola.

Naye Kocha Ibenge alisema tayari amesuka mbinu bora kupata ushindi japokuwa wataingia katika mtanange huo kwa kuwaheshimu wapinzani wao.

“Ninaiheshimu Simba, ina kikosi kizuri lakini nitahakikisha tunaingia katika mchezo huo na mbinu za kushambulia zaidi tupate ushindi,” alisema.

Katika michuano hiyo, Simba ilishinda mechi zake mbili za kundi B wakati Azam FC ikishinda mbili na kutoka sare moja katika kundi A.

Simba ilishinda 1-0 dhidi ya Muembe Makumbi na 2-1 ilipocheza na Fufuni wakati Azam FC ikishinda 2-0 na Mlandege, 2-1 na URA na sare ya bao 1-1 ilipocheza na Singida Black Stars.

Previous Post

WACHINA WANAODAIWA KUKUTWA NA MABILIONI WAPANDISHWA KORTINI

Next Post

DK. MIGIRO AJA KIVINGINE CCM

Next Post
DK. MIGIRO AJA KIVINGINE CCM

DK. MIGIRO AJA KIVINGINE CCM

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

TUUNGANE KUJENGA NCHI – BALOZI NYALANDU

TUUNGANE KUJENGA NCHI – BALOZI NYALANDU

3 months ago
RAIS DK. SAMIA APOKEA UJUMBE WA RAIS PUTIN

RAIS DK. SAMIA APOKEA UJUMBE WA RAIS PUTIN

9 months ago

Popular News

  • MVUTANO MAZISHI YA WAMBURA WAFIKA KORTINI, DALILI ZA MARIDHIANO ZACHOMOZA

    MVUTANO MAZISHI YA WAMBURA WAFIKA KORTINI, DALILI ZA MARIDHIANO ZACHOMOZA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA ATAJA SIFA ZA MAWASILIANO SERIKALINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • 50 BORA ‘FORM SIX’ KUSOMA AI NJE YA NCHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DHAHABU YENYE THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 1.2/- YAKAMATWA IKITOROSHWA DAR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA ATAKA UADILIFU, USHIRIKIANO NA MATOKEO KWA VIONGOZI WAPYA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?