• ePaper
Sunday, January 11, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

SIMANZI WATOTO WAKIFIA NDANI YA SWIMMING POOL

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 9, 2026
in Habari, Kitaifa
0
SIMANZI WATOTO WAKIFIA NDANI YA SWIMMING POOL
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na LILIAN JOEL, Arusha

VILIO na majonzi vimetawala katika Kijiji cha Kimnyaki, kilichopo Wilaya ya Arumeru mkoani Arusha, baada ya watoto wawili wa familia moja kupoteza maisha wakati wakiogelea katika bwawa (swimming pool) la Kilimanjaro Court, lilipo katika moja ya hoteli maarufu wilayani humo.

Akizungumza kwa masikitiko makubwa, msemaji wa familia ya watoto hao ambaye ni Mwenyekiti wa Kijiji cha Kimnyaki, Samwel Meliyo, alisema tukio hilo lilitokea Januari 7, mwaka huu, majira ya saa 9:00 alasiri.

Meliyo aliwataja waliofariki kuwa, ni Abednego Joachim (13), ambaye mwaka huu alitarajiwa kuanza kidato cha kwanza katika Shule ya Sekondari ya Serikali ya Mwanderi na Ebenezer Joachim (9), ambaye alikuwa anasoma darasa la tatu katika shule ya Blue Berry.

“Tumepokea msiba huu kwa mshtuko na masikitiko makubwa, kwa sababu watoto hawa waliondoka na mama yao mzazi wakiwa wazima lakini, baada ya muda mfupi tukapata taarifa kwamba wamepoteza maisha wakiogelea,” aliongeza.

“Nilipojulishwa kwamba kuna msiba umetokea hapa bomani nilidhani babu wa watoto hawa mzaa baba yao, kwa sababu ni mgonjwa alitibiwa Selian kisha kupewa rufaa ya kwenda Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya KCM, lakini baada ya kufika nikajulishwa siyo yeye ni watoto, nilipata mshtuko mkubwa,” alisimulia kwa maumivu.

Kwa mujibu wa Meliyo, hawezi kueleza kwa kina kilichowasibu watoto wao wakati wakiogelea kwani mama yao mzazi ambaye alikuwa nao amelezwa hospitalini kutokana na hali yake kutokuwa nzuri, huku baba yao akiwa katika hali ngumu ya mawazo.

Aidha, Meliyo alitumia fursa hiyo kuiomba serikali kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya wamiliki wa eneo hilo kutokana na uzembe uliosababisha watoto hao kupoteza maisha, akidai inawezekana hapakuwa na wa kuangalia watoto wakiogelea.

“Tumejulishwa kwamba meneja wa eneo hilo na watu wengine wanne wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha. Niiombe serikali ichukue hatua kali za kisheria pale itakapobaini kulikuwa na uzembe,”aliomba.

Kuhusu mazishi ya watoto hao, Meliyo alisema yatafanyika Januari 10 mwaka huu, nyumbani kwao Kimnyaki na kwamba hali za wazazi wa watoto hao siyo nzuri.

Mmoja wa wanafamilia aliyejitambulisha kwa jina la  Kenyata Joel maarufu (Dad), alisema alipigiwa simu na baba wa marehemu, akimuomba awahi Hospitali ya St. Joseph, iliyopo jirani na eneo hilo kwa madai kwamba watoto wamepata ajali.

“Nilikuwa Ngaramtoni, nikatoka mara moja nikidhani wamepata ajali ya gari lakini nilipofika hospitalini hapo nilikuta ni ajali ya maji kisha tukaenda Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mount Meru, lakini watoto walikwishafariki,” alifafanua kwa huzuni.

MBUNGE 

Mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi, Johannes Lukumay, alitoa rai kwa wamiliki wa maeneo ya kuogelea katika jimbo hilo kuajiri watumishi wenye taaluma ya kuogelea ili tatizo likitokea uokozi ufanyike kwa haraka bila kuleta majanga.

Kamanda wa Kikosi cha Zimamoto Mkoa wa Arusha, Oswad Mwanjenjele, alikiri kulijua tukio hilo lakini, hawakupata taarifa mapema hivyo marehemu hao waliokolewa na watu wengine.

Previous Post

RAIS DK. SAMIA AONYA WAVURUGA AMANI

Next Post

WADAU MICHEZO WAMTUMIA SALAMU WAZIRI MAKONDA

Next Post
WADAU MICHEZO WAMTUMIA SALAMU WAZIRI MAKONDA

WADAU MICHEZO WAMTUMIA SALAMU WAZIRI MAKONDA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

JESCA MAGUFULI AWATAKA SHINYANGA KUIAMINI CCM

JESCA MAGUFULI AWATAKA SHINYANGA KUIAMINI CCM

4 months ago
DK. SAMIA AMELETA MIRADI MIKUBWA LINDI – MAJALIWA

DK. SAMIA AMELETA MIRADI MIKUBWA LINDI – MAJALIWA

4 months ago

Popular News

  • RAIS DK. SAMIA ATAJA SABABU MABADILIKO BARAZA LA MAWAZIRI

    RAIS DK. SAMIA ATAJA SABABU MABADILIKO BARAZA LA MAWAZIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DIAMOND KUTOKA KIVINGINE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KOCHA SIMBA AJITETEA, MASHABIKI WACHARUKA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WADAU MICHEZO WAMTUMIA SALAMU WAZIRI MAKONDA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMANZI WATOTO WAKIFIA NDANI YA SWIMMING POOL

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?