• ePaper
Tuesday, April 21, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Biashara

SERIKALI YAWATAKA WATANZANIA KUCHANGAMKIA FUSRA AFCON

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 3, 2025
in Biashara, Burudani, Habari, Michezo
0
SERIKALI YAWATAKA WATANZANIA KUCHANGAMKIA FUSRA AFCON
0
SHARES
8
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na AMINA KASHEBA

SERIKALI imewataka Watanzania kujipanga na kuchangamkia fursa katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2027).

Michuano hiyo inatarajiwa kufanyika kwa mara ya kwanza katika nchi za Tanzania, Kenya na Uganda.

Akizungumza Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo wa Taifa (BMT), Neema Msitha amesema Watanzania wanatakiwa kuchangamkia fursa mbalimbali kuhakikisha wananufaika na fainali hizo.

“Mashindano ya Kombe la Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN), tuliona Watanzania mbalimbali walivyonufaika nayo kwa kujiongezea kipato kupitia biashara zao.

“Tunaomba Watanzania wajipange kuhakikisha wanachangamkia fura zitakazojitokeza katika michuano ya AFCON 2027, kwani kuna fursa mbambali ambazo wakizitumia vizuri zitawasaidia kujiongezea kipato,” amesema.

Katibu huyo alisema Watanzania wanatakiwa kuhakikisha wanatumia vizuri fursa za mashindano ya AFCON kwani kutakuwa na wageni wengi ambao watakuja nchini.

“Usishangae uwanjani wakajaa wageni kuliko wenyeji kutokana na ukubwa wa mashindano hayo na watu ambao watakuwa wanakuja kusindikiza timu zao, kujifunza na kufuatilia michuano.

“Watanzania wasione mashindano ya AFCON 2027 yapo mbali, hivyo waanze maandalizi ya mapema kuhakikisha wanafikia malengo waliyojiwekea,” amesema.

Katibu huyo alitoa shukrani kwa Watanzania ambao waliojitokeza kwa wingi katika michuano ya CHAN 2024 na kuipa sapoti yakutosha Taifa Stars ambayo ilitolewa hatua ya robo fainali.

Previous Post

DK. MWINYI: SITAKI KUACHA DENI

Next Post

FADLU AWAONGEZEA ‘DOZI’ MASTAA WAKE

Next Post
FADLU AWAONGEZEA ‘DOZI’ MASTAA WAKE

FADLU AWAONGEZEA ‘DOZI’ MASTAA WAKE

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. MWINYI ACHUKUA FOMU ZANZIBAR, AHADHARISHA CHUKI

DK. MWINYI ACHUKUA FOMU ZANZIBAR, AHADHARISHA CHUKI

8 months ago
HESABU KALI SIMBA,YANGA ZIKIWAWINDA AL AHLY, ESPERANCE

HESABU KALI SIMBA,YANGA ZIKIWAWINDA AL AHLY, ESPERANCE

3 months ago

Popular News

  • SIMBA KASI ILE ILE

    SIMBA KASI ILE ILE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DAKTARI ATAJA DALILI ZA SHINIKIZO LA DAMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WANASIASA WATAJA FAIDA ZA MUUNGANO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU AKOMAA NA WAKANDARASI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • AJIRA 45,000 ZANUKIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?