• ePaper
Monday, January 19, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

DK. MWINYI: SITAKI KUACHA DENI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 2, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa
0
DK. MWINYI: SITAKI KUACHA DENI

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi

0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

NA HANIFA RAMADHANI,

Zanzibar

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema dhamira yake ni kuhakikisha anapoondoka madarakani, haachi deni lolote kwa serikali ambalo alikopa kutekeleza miradi ya maendeleo.

Amesema hilo litawezekana kwa kuwa serikali yake imeweka mfumo wa kulipa madeni kwa kuanzisha akaunti maalumu na kila mwezi inaweka dola za Marekani milioni 15 kulipa madeni.

Dk. Mwinyi ameyasema hayo Ikulu Mjini Unguja qlipokuwa akizungumza na wahariri na waandishi wa habari kutoka Tanzania Bara na Zanzibar.

Amesema kuwa, serikali imeiagiza Wizara ya Fedha kuhakikisha kila mwezi fedha hizo zinaingia katika akaunti maalumu kulipa mikopo, ndio maana inapata nguvu ya kuendelea kukopa kwa maendeleo ya Zanzibar.

“Nitaondoka katika uongozi siachi deni hata la senti tano. Ndani ya nafsi yangu nitahakikisha siachi deni ambalo serikali imelikopa,” amesema.

Dk. Mwinyi  ameweka wazi siri ya mafanikio ya utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo katika kipindi kifupi cha uongozi wake huku amani ikiwa jambo kubwa zaidi.

SIRI YA MAFANIKIO SERIKALI YA AWAMU YA NANE

Mambo mengine ni utulivu uliopo, usimamizi mzuri katika ukusanyaji wa mapato na usimamizi wa matumizi..

Aidha, amesema umoja na utulivu wa wananchi hata katika maeneo ambayo awali yalikuwa yakionekana yana rabsha sasa kumetulia hivyo kutoa fursa ya kuleta maendeleo.

“Namshukuru Mungu, tangu nilipoingia madarakani nimekuta wananchi ni wamoja, hata zile zehemu ambazo zilikuwa na mtafaruku mkubwa sasa zimekuwa tulivu kabisa,” amesema.

Ameeleza kuwa, jambo hilo limeipa nafasi serikali kufanya mambo ya maendeleo ikiwemo kujenga shule, hospitali, barabara, miradi ya maji, umeme, viwanja vya ndege na bandari.

Pia, amesema mafanikio yaliyopatikana yamechochewa na ukusanyani mzuri wa mapato ambayo yameipa nguvu serikali yake kufanya mambo makubwa kwa kuwa fedha zipo.

“Wakati naingia madarakani ZRA wakati ule ZRB (Mamlaka ya Mapato Zanzibar) ilikuwa ikikusanya sh bilioni 20 kwa kwa mwezi lakini sasa inakusanya sh. bilioni 80, TRA (Mamlaka ya Mapato Tanzania) ilikuwa ikikusanya sh. bilioni 20 hadi 25 kwa mweli, sasa inakusanya sh. bilioni 50,” amesema.

Mbali na hayo, Dk. Mwinyi amesema mafanikio yanayoonekana sasa ndani ya kipindi kifupi cha utawala wake yametokana na usimamizi thabiti wa matumizi ya serikali.

WITO KUELEKEA UCHAGUZI

Akitoa ujumbe kwa wananchi kuelekea, amesisitiza kuimarisha, umoja amani na mshikamano.

“Natumia fursa hii kuwasihi wananchi tujitahidi kufanya uchauzi wa amani. Mtu yeyote anayeitakia mema nchi hii atangulize amani.

“Kila mtu ahubiri amani, viongozi wa dini wahubiri amani, wanasiasa wahubiri amani, waandishi wa habari wasisitize amani,” ameeleza.

Previous Post

BALOZI NCHIMBI AMSIFU DK. SAMIA KUIMARISHA UHUSIANO

Next Post

SERIKALI YAWATAKA WATANZANIA KUCHANGAMKIA FUSRA AFCON

Next Post
SERIKALI YAWATAKA WATANZANIA KUCHANGAMKIA FUSRA AFCON

SERIKALI YAWATAKA WATANZANIA KUCHANGAMKIA FUSRA AFCON

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MGOMBEA URAIS CCM KURINDIMA RUVUMA LEO

MGOMBEA URAIS CCM KURINDIMA RUVUMA LEO

4 months ago
WASIRA : VIJANA MSIKUBALI KUTUMIKA KUVURUGA AMANI

WASIRA : VIJANA MSIKUBALI KUTUMIKA KUVURUGA AMANI

2 months ago

Popular News

  • KOFANE ALIVYOANDIKA HISTORIA CAMEROON AFCON MSIMU HUU

    KOFANE ALIVYOANDIKA HISTORIA CAMEROON AFCON MSIMU HUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MIGIRO KATIBU MKUU WA  KWANZA MWANAMKE NA MIKAKATI YA KUIMARISHA MASHINA KATIKA MITAA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SAFARI KUMALIZA CHANGAMOTO UMEME IRINGA, DODOMA YAIVA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TANZANIA YAINGIA 10 BORA KUVUTIA UWEKEZAJI AFRIKA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AMREJESHA MAKONDA AFCON

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?