• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Burudani

TAIFA STARS, ZAMBIA NI MECHI YA HESHIMA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 8, 2025
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
TAIFA STARS, ZAMBIA NI MECHI YA HESHIMA

STARS

0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na AMINA KASHEBA

TIMU ya Taifa ‘Taifa Stars’ itashuka dimbani leo kupambana na Zambia katika mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia 2026.

Mchezo huo umepangwa kufanyika saa 4:00 usiku katika Uwanja wa New Amaan Complex, visiwani Zanzibar.

Akizungumza na vyombo vya habari, Kocha Mkuu wa Stars, Hemed Suleiman ‘Morocco’ amesema maandalizi yote yamekamilika kuelekea pambano hilo.

“Tuko vizuri wachezaji wote wamejipanga vizuri na kila moja anahitaji kuonesha ushindani, tunatambua mechi ni ngumu dhidi ya Zambia tutapambana kushinda,” alisema.

Morocco alisema wachezaji wake wapo  fiti kuikabili Zambia na kushinda mchezo huo.

“Wachezaji wana morali ya kutosha kila moja nashukuru wana fanya vizuri, wananipa moyo kutokana na kiwango chao kuwa kizuri,” alisema Morocco.

Kocha huyo aliwaomba Watanzania kujitokeza kwa wingi uwanjani katika mchezo huo kwa lengo la kuwapa hamasa wachezaji hao.

Mwakilishi wa wachezaji, Bakari Mwamnyeto alisema wachezaji wapo tayari kupambana katika mchezo huo kupata ushindi.

“Tumejipanga na tutasikiliza maelekezo ya mwalimu kwa lengo la kupata ushindi katika mchezo huu, tunatambua mechi ni ngumu tutahakikisha tunapata ushindi,” alisema.

Kocha wa Zambia, Avram Grants alisema wachezaji wake hawana presha kuelekea katika mchezo huo japokuwa utakuwa mgumu.

“Wachezaji wako vizuri kuelekea mchezo wa leo, kila kitu kipo sawa tumejipanga kuhakiksha tunapata ushindi,” alisema.

Kocha huyo alisema mipango yake ni kushinda katika mchezo huo, ingawa amekiri mchezo utakuwa mgumu, lakini hana wasiwasi wowote wa kupata matokeo mazuri.

Mwakilishi wa wachezaji wa Zambia, Kennedy Musonda alisema wamejipanga kuhakisha wanafanya vizuri katika mchezo huo.

“Natambua uzuri wa wachezaji wa Tanzania sisi wachezaji tumejipanga kuhakikisha tunafanya vizuri na kupata ushindi, hatuna presha yoyote zaidi ya kupambana na kupata matokeo mazuri,”alisema Musonda.

Katika msimamo wa kundi E, Stars ipo nafasi ya pili ikiwa na pointi 10, Morocco inaongoza kundi hilo, ikiwa  imefuzu huku ina pointi 21.

Timu ya Niger  ipo nafasi ya tatu katika msimamo huo ikiwa na pointi tisa, Zambia ina pointi sita.

Timu ya Congo inaburuza mkia katika kundi hilo, ikiwa na alama moja.

Previous Post

DK. NCHIMBI AELEZA DK. SAMIA  ALIVYOSIMAMIA USALAMA NCHINI

Next Post

DK. SAMIA KUISUKA MWANZA YA KIMATAIFA

Next Post
DK. SAMIA KUISUKA MWANZA YA KIMATAIFA

DK. SAMIA KUISUKA MWANZA YA KIMATAIFA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA ATANGAZA HATUA ZA MWISHO UTEKELEZAJI MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA

DK. SAMIA ATANGAZA HATUA ZA MWISHO UTEKELEZAJI MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA

2 weeks ago
DK. SAMIA, BALOZI NCHIMBI WAAHIDIWA KURA ZA KISHINDO

DK. SAMIA, BALOZI NCHIMBI WAAHIDIWA KURA ZA KISHINDO

2 months ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.