• ePaper
Friday, May 8, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

DK. SAMIA ATAJA SIFA ZA VIONGOZI WANAOFAA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 10, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
DK. SAMIA ATAJA SIFA ZA VIONGOZI WANAOFAA

MGOMBEA Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan

0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MUSSA YUSUPH,

Bunda

MGOMBEA Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan, ametoa angalizo kwa wananchi kutofanya majaribio ya kuchagua viongozi katika uendeshaji wa nchi.

Amesema uongozi wa nchi, anapewa kiongozi mwenye kuaminika na mwenye uwezo wa kuliendesha Taifa kwa maslahi ya wananchi.

Dk. Samia ameyasema hayo katika mkutano wa kampeni uliofanyika wilayani Bunda mkoani Mara na kusisisitiza kuwa, Chama pekee ambacho kinafanyakazi kwa kuzingatia maslahi ya wananchi ni CCM.

“Katika uendeshaji wa nchi hakuna majaribio, unampa nchi yule ambaye unamwamini atakayeiendesha vyema nchi kwa maslahi ya wananchi.

“Ukiangalia kwetu Tanzania, chama ambacho ukweli kitafanyakazi na maendeleo ya wananchi yatapatikana ni Chama Cha Mapinduzi peke yake. Mkiwapa wengine wanakwenda kuwafuja, wanakwenda kuwapoteza.

“Kwa sababu wakiingia kwanza ni kujifunza. Na utakapompa jimbo asiyekuwa wa CCM, anakwenda kuongea na nani? anakwenda kumwomba barabara nani?”alihoji.

Dk. Samia alisema sehemu sahihi ya kuchagua viongozi watakaoliletea maendeleo taifa ni wagombea wa CCM.

“Ndugu zangu, msicheze na hiyo kitu kabisa. Pelekeni kura kwa wateuliwa, wateuliwa hawa ni wagombea wa Chama Cha Mapinduzi. Wapeni kura safari yetu ya maendeleo iendelee.

“Msidanganyike maendeleo na maslahi yenu yatatokana na serikali ya Chama Cha Mapinduzi,” alieleza.

Dk. Samia alisema katika ilani ya uchaguzi CCM (2025 – 2030) ina sera za aina mbili ambayo kwanza ni maendeleo ya jamii yenye kujumuisha maji, umeme, afya na elimu.

Alisema imani ya CCM ni kuhakikisha mwananchi wanakuwa salama katika maeneo hayo hatua itakayowawezesha kuchangia uchumi wa nchi.

“Tunakwenda kukamilisha katika maendeleo ya jamii na pia tunaweka nguvu katika maendeleo ya kiuchumi ambayo tunazungumzia kilimo, uvuvi, ufugaji na njia za usafiri.

“Kwa upande wa kilimo miaka mitano iliyopita, tulijitahidi katika maeneo mbalimbali kujenga skimu za umwagiliaji ili wakulima walime mara mbili kwa mwaka,” alisisitiza.

Vilevile, alisema serikali ilitoa mbolea na mbegu za ruzuku kumwezesha mkulima kuzalisha kwa wingi hatua ambayo imeleta matokeo mazuri kwa Tanzania kujitosheleza kwa chakula kwa asilimia 128.

Kuhusu uvuvi, alieleza kuwa serikali imejenga vizimba 47 vya kufugia samaki pamoja na mabwawa matano katika Wilaya ya Bunda hatua ambayo imezalisha ajira kwa vijana.

“Hatutaishia hapo, ilani yetu kwa miaka mitano ijayo inazungumza tuongeze nguvu katika sekta ya uvuvi na pia tuweke viwanda vya kuchakata mazao ya uvuvi pale ambapo yatapatikana kwa wingi.

“Kwa kazi ambayo tumeifanya miaka mitano iliyopita, tumeweza kuongeza mapato kwa wavuvi katika Wilaya ya Bunda kutoka sh. bilioni tisa hadi sh. bilioni 38 fedha ambazo zimeingia mifukoni mwa wavuvi,” alisisitiza.

Awali, Mgombea Ubunge Jimbo la Bunda Mjini, Ester Bulaya, alisema Dk. Samia amefanya makubwa katika sekta za afya, maji na elimu.

Alisema serikali ya Dk. Samia imekamilisha ujenzi wa zahanati 13, hospitali ya halmashauri ya mji, vituo vya afya na nyumba za madaktari katika vituo vya afya.

Bulaya alisema katika elimu, madarasa zaidi ya 50 yamejengwa, matundu ya choo zaidi ya 100 na ujenzi wa shule za msingi na sekondari umekamilika.

Akizungumzia miradi ya maji, alieleza kuwa sh. bilioni 26 zimetengwa kukamilisha miradi tisa ya maji kati ya hizo sh. bilioni 13 zimeshatolewa kwa wakandarasi.

AKIAHIDI ANATEKELEZA

Awali akiwa katika Jimbo la Busega, Dk. Samia alisema akiahidi anatekeleza na ndiyo sababu ya kutoa fedha za ujenzi wa soko na kituo cha mabasi kama alivyoahidi.

Alisisitiza kuwa, alitoa fedha kujenga soko eneo la Lamadi na kituo cha mabasi Nyashimo hata hivyo madiwani wamekuwa wakivutana.

Pia, alisema ametoa fedha hizo, kutekeleza ahadi ya ujenzi wa soko Lamadi na kituo cha mabasi kijengwe eneo la Nyashimo.

Hivyo, alitoa rai kwa viongozi hao kuzingatia ahadi aliyoitoa ili wananchi wapate huduma hizo.

Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dk. Asha – rose Migiro, alisema eneo la Lamadi ni muhimu kwani ni kiunganishi kikubwa kati ya mikoa ya Mwanza, Simiyu na Mara.

Alisisitiza kuwa, ifikapo Oktoba 29, mwaka huu wananchi wajitokeze kwa wingi kumpigia kura Dk. Samia

Kwa upande wake, Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Kenan Kihongosi, alisema katika Kata ya Lamadi kulikuwa na changamoto ya maji ambapo kazi kubwa imefanyika kusimamia mradi wenye thamani zaidi ya sh. bilioni 400.

Alisema maji hayo, yatasambazwa Meatu, Busega, Itilima hadi Bariadi, hivyo kuondoa kero ya uhaba wa maji.

Pia, alisema wananchi wa eneo la Nyanshimo wameondokana na kero ya mafuriko baada ya Dk. Samia kutoa fedha za kujenga daraja.

Kihongosi ambaye aliwahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, alitoa wito kwa vijana kutokubali kutumika kisiasa kuvuruga amani ya nchi.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Shamsa Mohammed, alisema katika sekta za afya, barabara, mifugo na uvuvi mengi ya maendeleo yamefanyika.

“Wananchi watahakikisha Oktoba wanakwenda kupiga kura za kishindo kwa Dk. Samia, wabunge na madiwani,” alisisitiza.

Mgombea Ubunge Jimbo la Busega, Saimon Songe, alisema jimbo hilo lina kila sababu kumpigia kura za kishindo Dk. Samia ifikapo Oktoba 29 mwaka huu.

Alizitaja moja ya sababu hizo ni kwamba, Dk. Samia alitoa sh. bilioni 13 katika elimu hatua ambayo imewezesha ujenzi wa shule ya sekondari na msingi Kata ya Lamadi na madarasa.

Previous Post

MOROCCO ATAJA KILICHOIPONZA STARS

Next Post

DK. MWINYI ATANGAZA NEEMA KWA VIJANA

Next Post
DK. MWINYI ATANGAZA NEEMA KWA VIJANA

DK. MWINYI ATANGAZA NEEMA KWA VIJANA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. MWINYI AFUNGUKA MALENGO SERA YA NISHATI

DK. MWINYI AFUNGUKA MALENGO SERA YA NISHATI

8 months ago
DK. NCHIMBI AITEKA RORYA | WANANCHI WATHIBITISHA KUTIKI OKTOBA  29 KWA KISHINDO

DK. NCHIMBI AITEKA RORYA | WANANCHI WATHIBITISHA KUTIKI OKTOBA  29 KWA KISHINDO

8 months ago

Popular News

  • YANGA MBELE KWA MBELE

    YANGA MBELE KWA MBELE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WATAALAMU WAFUNGUKA MITAZAMO YA MIKATABA 8

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA AKEMEA VIONGOZI ‘KUVIMBA’

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DEMOKRASIA ISIZICHAFUE NCHI ZETU – RAIS DK. SAMIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ZIARA YA RAIS KAGAME, RUTO KUIMARISHA DIPLOMASIA KIUCHUMI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?