• ePaper
Wednesday, September 9, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

DK. SAMIA KUWAINUA WANANCHI KIUCHUMI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 11, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
DK. SAMIA KUWAINUA WANANCHI KIUCHUMI

MGOMBEA Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan

0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MUSSA YUSUPH,

Musoma

MGOMBEA Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema mkakati wa serikali katika miaka mitano ijayo ni kuendelea kuwawezesha wananchi kiuchumi.

Akizungumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika Musoma Mjini mkoani Mara, Dk. Samia alisema kipaumbele cha serikali ni kuimarisha maisha ya wananchi.

“Kwa upande wa uwezeshaji wa wananchi kiuchumi, serikali inakuja na mradi wa kujenga stendi na masoko nchi nzima kutoa fursa kwa wafanyabiashara ndogondogo.

“Kupitia mfuko wa halmashauri wa asilimia 10 ambao tumeugawa kwa makundi ya wanawake, vijana na wenye ulemavu nayo hiyo ni fursa nyingine ya kuwezesha wananchi kiuchumi,” alisema.

Alisisitiza: “Hivyo kijana jipange ujue unataka kufanya biashara gani, stendi tunajenga, masoko tunajenga, mifuko ya kukuwezesha ipo hivyo sema unataka kufanya biashara gani?

“Kubwa zaidi tumesema katika ilani mpya tunakwenda kurasimisha biashara ndogondogo zitambulike, ziwe rasmi mfaidike sawa na wafanyabiashara wengine.”

Dk. Samia alisema katika kuwawezesha wananchi, serikali pia imekuja na mfumo wa ruzuku katika kilimo na pembejeo.

Alisema serikali inaendeleza mkakati wa kilimo cha umwagiliaji kwa kujenga skimu na mabwawa huku upande wa uvuvi imefanya mengi zaidi ikiwemo ufugaji samaki kwa mabwawa na vizimba.

Previous Post

DK. SAMIA : WANAWAKE TUNA UWEZO KUONGOZA

Next Post

KIHONGOSI AWATAKA VIJANA KUTOKUBALI KUVURUGA AMANI

Next Post
KIHONGOSI AWATAKA VIJANA KUTOKUBALI KUVURUGA AMANI

KIHONGOSI AWATAKA VIJANA KUTOKUBALI KUVURUGA AMANI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

RAIS DK. SAMIA ATOA AGIZO  KOMBE LA DUNIA 2026

RAIS DK. SAMIA ATOA AGIZO  KOMBE LA DUNIA 2026

4 months ago
TANZANIA, UGANDA KATIKA TAKWIMU

TANZANIA, UGANDA KATIKA TAKWIMU

9 months ago

Popular News

  • RAIS DK. SAMIA, NDEJEMBI TURUFU YA MAENDELEO KWA WATANZANIA

    RAIS DK. SAMIA, NDEJEMBI TURUFU YA MAENDELEO KWA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI AONYA, ATOA SIKU 60 WENYE SILAHA HARAMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NDEJEMBI MZIGONI RASMI, AKEMEA KAZI KWA MAZOEA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUME MIPANGO, NIRC WAJADILI UBORA MIRADI YA UMWAGILIAJI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MASAUNI AANIKA UMAHIRI WA TANZANIA INAVYOLINDA UDONGO, MATUMIZI MBOLEA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?