• ePaper
Sunday, August 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Biashara

TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 15, 2025
in Biashara, Habari, Kitaifa
0
TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

WAFANYABIASHARA KARIAKOO

0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

KAMISHNA Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Yusuph Mwenda, amewahakikishia wafanyabiashara wa soko la Kimataifa la Kariakoo usalama wa biashara zao.

Mwenda aliyekutana na viongozi wa wafanyabiashara hao, wamachinga na wafanyabiashara wenyewe, aliwapa pole kutokana na kufunga biashara zao katika kipindi cha uchaguzi pamoja na madhara waliyopata katika kipindi hicho.

“Nimekuja kuona shughuli mnazofanya, pia kuwapa pole kwa changamoto zilizotokea, nimekuja kuona biashara zinaendeleaje na nimefurahi kuona biashara zinaendelea kama kawaida na nimethibitishiwa na wauzaji nilizungumza nao kuwa, wanauza kama kawaida na wateja wanakuja,”alisema Mwenda.

Pia, kamishna huyo alishuhudia shughuli za biashara zikiendelea kama kawaida katika soko la Kariakoo hali ikiwa shwari na kuwahakikishia wafanyabiashara TRA itaendelea kulinda ustawi wa biashara zao kwa kuendelea kutatua changamoto zinazowakabili.

“Biashara zenu binafsi ni biashara za umma, na sisi ni wabia wa biashara hizo, hivyo tuna wajibu wa kuzilinda na kuhakikisha zinastawi,” alisema Mwenda.

Alisema kuimarika biashara katika soko la Kariakoo kunahakikisha kufunguka biashara katika maeneo mengine ya nje ya jiji la Dar es Salaam na nchi jirani na kuwataka viongozi wa wafanyabiashara wafanye tathmini ya athari zilizotokana na changamoto zilizojitokeza kipindi cha uchaguzi mkuu katika biashara zao kushauri hatua zinazopaswa kuchukuliwa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa wafanyabiashara wa Kariakoo, Severin Mushi, alisema hali ya biashara katika soko la Kariakoo imeimarika na kueleza wateja na wafanyabiashara wapo salama, huku akitoa wito kwa wananchi kwenda kufanya manunuzi.

Naye, Mwenyekiti wa Wamachinga, Stephen Lusinde, alisema biashara zao ndani ya soko la Kariakoo na nyingine zililindwa na vijana takriban 150 katika kipindi chote cha changamoto na kuwahakikishia usalama wananchi wanaotaka kwenda Kariakoo kununua bidhaa.

Previous Post

MAAGIZO MATATU KWA DK. NCHEMBA

Next Post

KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

Next Post
KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

UWEKEZAJI NSSF WA MZIZIMA TOWERS KUFUNGUA FURSA MPYA ZA BIASHARA NA UTALII DAR

UWEKEZAJI NSSF WA MZIZIMA TOWERS KUFUNGUA FURSA MPYA ZA BIASHARA NA UTALII DAR

5 months ago
SIMBA YAKIMBILIA MAFICHONI

SIMBA YAKIMBILIA MAFICHONI

6 months ago

Popular News

  • KIINI DABI KARIAKOO KUPIGWA ZANZIBAR

    KIINI DABI KARIAKOO KUPIGWA ZANZIBAR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TAMU, CHUNGU DABI YA K’KOO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA AKUTANA NA VIONGOZI WA TEC

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA AWAPA RAHA VIGOGO USHIRIKA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • BILIONI 30/- KUJENGA UWANJA WA KISASA SIMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?