• ePaper
Wednesday, June 17, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 15, 2025
in Burudani, Kimataifa, Michezo
0
KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO
0
SHARES
9
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

KAIMU Kocha Mkuu wa timu ya taifa ‘Taifa Stars’, Miguel Gamondi, leo atakabiliwa na mtihani wake wa kwanza atakapoiongoza miamba hiyo katika mchezo wa kujipima nguvu dhidi ya Kuwait.

Taifa Stars itachuana na Kuwait saa 1:00 usiku katika mechi iliyopo katika kalenda ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), itakayopigwa Uwanja wa Al Salam uliopo jijini Cairo, Misri.

Gamondi ataiongoza Stars kwa mara ya kwanza ikiwa siku kadhaa tangu alipopewa mikoba baada ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kuachana na mzawa Hemed Suleiman Morocco.

Akizungumzia mechi ya leo, Gamondi amesema pamoja na timu yao kushindwa kufanya maandalizi ya kutosha, lakini ana imani watashinda katika mchezo huo.

Amesema ana imani kubwa na kikosi chake kwani kila mchezaji ametoka katika mashindano katika klabu hivyo hana hofu na viwango vyao.

Gamondi amesema anafurahi kuona kila mchezaji ana morali ya kutosha kuhakikisha wanatumia vyema kila mbinu aliyowapatia.

“Tunaingia katika mchezo huo kwa kuwaheshimu wapinzani na kucheza kwa tahadhari kubwa, lengo kuhakikisha tunapata ushindi, nina imani hilo linawezekana kutokana na ubora mkubwa tuliokuwa nao,” amesema.

Kocha huyo amesema atahakikisha anakipanga vyema kikosi chake kwa kutumia mbinu tofauti kupata matokeo ya ushindi.

Nyota wa timu hiyo, Shomari Kapombe, amesema wachezaji wamejipanga vizuri kuhakikisha wanapata ushindi katika mchezo huo.

Amesema anajua mchezo utakuwa mgumu lakini atahakikisha anapambana kupata matokeo.

Kapombe amesema wachezaji wote wana morali ya kutosha na kila mmoja ana uhitaji mchezo huo.

Naye mshambuliaji wa timu hiyo, Kelvin John, amesema huo ni mchezo muhimu kwao kujipima kwa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON), kujua wapi walipo na wapi wanatakiwa kufanya marekebisho.

“Huu ni mchezo muhimu kwetu hasa kuelekea katika mashindano ya AFCON, mwalimu atapata nafasi ya kujua nini aongeze na kipi apunguze kwa hiyo ni mechi nzuri ya kujipa na kujua wapi tunakosea hivyo tutapambana kuonyesha ubora tuliokuwa nao,” alisema.

Previous Post

TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

Next Post

YANGA, SIMBA KAZI KAZI

Next Post
YANGA, SIMBA KAZI KAZI

YANGA, SIMBA KAZI KAZI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MSUVA NA REKODI YA MAANA AFCON

MSUVA NA REKODI YA MAANA AFCON

6 months ago
TRA YABAINI MCHEZO MCHAFU UKWEPAJI KODI  BANDARI KAVU

TRA YABAINI MCHEZO MCHAFU UKWEPAJI KODI  BANDARI KAVU

4 months ago

Popular News

  • WABUNGE WAIPONGEZA NSSF NA PSSSF KWA KUANZISHA SKIMU YA HIFADHI KWA WALIOJIAJIRI NA UWEKEZAJI WA KIWANDA CHA NGOZI

    WABUNGE WAIPONGEZA NSSF NA PSSSF KWA KUANZISHA SKIMU YA HIFADHI KWA WALIOJIAJIRI NA UWEKEZAJI WA KIWANDA CHA NGOZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WABUNGE WAPONGEZA UWEKEZAJI KLICL

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAKAGUZI WA CAF WARIDHISHWA NA MAENDELEO YA VIWANJA VYA AFCON 2027

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MKAKATI KUDHIBITI VIFO WAJAWAZITO WAANIKWA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WASOMI, WANASIASA WAKOSHWA TOZO KUCHANGIA BIMA YA AFYA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?