• ePaper
Sunday, January 11, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

YANGA, SIMBA NI VIKUMBO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 17, 2025
in Burudani, Michezo
0
YANGA, SIMBA NI VIKUMBO

YANGA NA SIMBA

0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

KLABU za Yanga na Simba zimeanza kupigana vikumbo kuwania saini za baadhi ya nyota wanaowataka katika dirisha dogo la usajili.

Timu hizo, zimeanza kusaka wachezaji wapya watakaoongezwa ndani ya timu hizo kwa kuboresha vikosi vyao ambavyo vinashiriki michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara na Ligi ya Mabingwa Afrika.

YANGA

Hadi sasa, tetesi zinaeleza kuwa kocha mkuu wa Yanga, Pedro Goncalves, ametaka kuongeza wachezaji watatu wapya.

Yanga wapo katika harakati ya kusaka saini ya nyota wa timu ya Taifa ya Uganda (Cranes), Allan Okello.

Okello anaichezea timu ya Vipers ya Uganda amekuwa na kiwango cha juu msimu huu.

Habari zaidi zinaeleza kuwa, kocha Pedro anamuhitaji Okello na nyota kutoka Angola, Laurindo Dilson Maria Aurélio, kuongeza nguvu katika kikosi chake.

Pia, imeelezwa kwamba Yanga imevutiwa na uwezo wa mchezaji wa timu ya TRA United, Emmanuel Mwanengo.

Uhuru ilimtafuta Ofisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe ambaye alisema tayari wamepokea ripoti kutoka kwa mwalimu wao.

 “Tumeona wachezaji wengi wanatajwa kuhusishwa na timu yetu, siyo wachezaji wabaya ni wazuri na wenye viwango vikubwa, tuwe na uvumilivu kwa kuwa kila mchezaji ambaye atasajiliwa tutamuweka wazi dirisha litakapofunguliwa,” alisema Kamwe.

Alisema kuwa watafanya usajili mapema zaidi kukimbizana na muda.

SIMBA

Uongozi wa klabu ya Simba umepanga kusajili wachezaji watatu pekee kuimarisha kikosi chao.

Simba ambayo ipo katika hatua ya mwisho ya kumtangaza kocha mpya muda wowote, kuchukua mikoba ya Dimitar Pantev.

Wekundu hao wa Msimbazi wapo katika rada ya kuwania saini ya mchezaji kutoka Stade Malien, Ismaïla Simpara.

Pia, kuna taarifa kuwa Clatous Chama anataka kurejea ndani ya klabu hiyo.

Hata hivyo, uongozi wa Simba unasubiri kutoa uamuzi wa kocha atakapokuja kama Jean Ahoua na Rushine  Reuck atawahitaji au vinginevyo.

Tayari Ahoua anatakiwa na timu moja ya nchini Morocco huku Rushine anaweza kurudi Mamelodi Sundowns.

Lakini viongozi wa Simba wanataka kumpa mkataba wa kudumu beki huyo ambaye alikuja kwa Wekundu wa Msimbazi kwa mkopo.

Uhuru ilimtafuta Meneja wa Habari na Mawasiliano Simba, Ahmed Ally,  alisema  kuhusiana na kumrudisha Chama ndani ya kikosi chao na kumsajili Ismaïla Simpara hilo ni suala la muda kwa kuwa Simba wakimuhitaji mchezaji yeyote hawawezi kumkosa.

 “Chama bado ni kipenzi cha Simba, kama viongozi wataona anafaa kurejea kikosini hapa hakuna atakayepinga, niwaambie tu kaeni mkao wa kula kwa sababu kuna wachezaji bora na wenye uwezo mkubwa watasajiliwa kurudisha makali yetu,” alisema Ahmed.

Previous Post

RAIS DK. SAMIA: HAKUNA MAENDELEO BILA AMANI

Next Post

MWAKINYO APEWA MBINU YA KUMCHAPA MNIGERIA

Next Post
MWAKINYO APEWA MBINU YA KUMCHAPA MNIGERIA

MWAKINYO APEWA MBINU YA KUMCHAPA MNIGERIA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

BONDIA MWAKYEMBE KUTOA ZAWADI YA KRISMASI

BONDIA MWAKYEMBE KUTOA ZAWADI YA KRISMASI

1 month ago
MRADI WA UMEMEJUA KISHAPU KULETA MAPINDUZI SEKTA YA NISHATI – MAKAMBA

MRADI WA UMEMEJUA KISHAPU KULETA MAPINDUZI SEKTA YA NISHATI – MAKAMBA

1 day ago

Popular News

  • RAIS DK. SAMIA ATAJA SABABU MABADILIKO BARAZA LA MAWAZIRI

    RAIS DK. SAMIA ATAJA SABABU MABADILIKO BARAZA LA MAWAZIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DIAMOND KUTOKA KIVINGINE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KOCHA SIMBA AJITETEA, MASHABIKI WACHARUKA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WADAU MICHEZO WAMTUMIA SALAMU WAZIRI MAKONDA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMANZI WATOTO WAKIFIA NDANI YA SWIMMING POOL

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?