• ePaper
Thursday, April 30, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

BONDIA MWAKYEMBE KUTOA ZAWADI YA KRISMASI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 11, 2025
in Burudani, Michezo
0
BONDIA MWAKYEMBE KUTOA ZAWADI YA KRISMASI

Emmanuel Mwaykembe

0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na AMINA KASHEBA

BONDIA wa ngumi za kulipwa, Emmanuel Mwaykembe amehaidi kutoa zawadi ya sikukuu ya Krisimasi katika pambano lake la Punch To Punch’ litakalofanyika Jumapili ya wiki  hii.

Mwakyembe atapanda ulingoni kuzichapa na Tionge Chingeni kutoka Malawi katika pambano lisilo la ubingwa raundi nane, uzito wa kati litakalofanyika Ukumbi wa The Sea View Dome Banguel ulipo Kawe jijini Dar es Salaam.

Akizungumza Dar es Salaam, jana,bondia huyo alisema hivi sasa anafanya mazoezi mepesi huku akisubiri kupima uzito, keshokutwa katika Viwanja vya Las Vega Mabibo.

“Niko fiti kabisa nahitaji kutoa zawadi ya sikukuu ya Krisimasi kwa Watanzania wote na mashabiki zangu kwa ujumla,” alisema.

Mwakyembe aliongeza kuwa Watanzania wanapaswa kufurahia mafanikio ya mchezo wa ngumi na yeye atawapa.

“Hivi sasa Tanzania inafanya vizuri katika michezo mbalimbali ndiyo maana sisi mabondia tunapambana kuongeza bidii katika mazoezi, kuwapiga wapinzani wetu kutoka nje ya nchi kama kwangu nipo fiti na pambano langu kumchakaza Mmalawi,” alisema Mwakyembe.

Promota wa pambano hilo, Latifa Jabiri alisema mpinzani wa bondia Mwakyembe, ameshafika Tanzania anasubiri siku ya kupima uzito.

“Kila kitu kinaenda vizuri kutakuwa na mapambano makali nina imani wadau wa masumbwi watafurahi kwa sababu kila bondia atayepanda ulingoni ataonyesha mchezo nzuri na kutoa burudani ya kutosha,” alisema.

Promota huyo alisema kutakuwa na mapambano 15 ambayo wadau wa masumbwi watashuhudia vijana wakipimana ubavu.

Previous Post

MASTAA YANGA, SIMBA WAPEWA PROGRAMU ZA MAZOEZI

Next Post

WATAALAMU WATAJA MAMBO 8 KUEPUKA UHABA WA MAJI DAR

Next Post
WATAALAMU WATAJA MAMBO 8 KUEPUKA UHABA WA MAJI DAR

WATAALAMU WATAJA MAMBO 8 KUEPUKA UHABA WA MAJI DAR

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MSIGWA AELEZA MANUFAA UBORESHAJI RELI YA TAZARA

MSIGWA AELEZA MANUFAA UBORESHAJI RELI YA TAZARA

4 months ago
DK.NCHIMBI AMTAJA ASKOFU MFUMBUSA NGUZO YA UMOJA

DK.NCHIMBI AMTAJA ASKOFU MFUMBUSA NGUZO YA UMOJA

1 week ago

Popular News

  • TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VYALENGA KUIJENGA JAMII KIUCHUMI NA KIROHO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUVUMILIANA MUHIMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI SANGU ABAINISHA HIFADHI SKIMU INAVYOENDA KUBADILI MAISHA YA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?