• ePaper
Thursday, April 30, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

MASTAA YANGA, SIMBA WAPEWA PROGRAMU ZA MAZOEZI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 11, 2025
in Burudani, Michezo
0
MASTAA YANGA, SIMBA WAPEWA PROGRAMU ZA MAZOEZI

MASTAA YANGA, SIMBA

0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

WACHEZAJI wanaoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara, wamepewa programu maalumu za mazoezi wanapokwenda nyumbani ili kulinda viwango vyao.

Ligi Kuu Tanzania Bara, imesimama kwa muda kupisha michuano ya Fainali yza Kombe la Mataifa ya Afrika(AFCON) 2025 inayotarajiwa kufanyika nchini Morocco.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Meneja wa Habari na Mawasiliano Simba, Ahmed Ally alisema kuwa wachezaji ambao hawajaitwa katika timu za taifa ,wamepewa programu ya mazoezi ya asubuhi na jioni ili kuhakikisha hawaongezeki uzito.

“Mara nyingi wachezaji wakiwa katika mapumziko wamekuwa wakizembea kufanya mazoezi ,lakini safari hii mwalimu, Suleiman Matola amewapa kazi maalumu huku kila mmoja akitakiwa kuripoti katika makundi maalumu kujiweka fiti.

“Kila mchezaji amepewa programu yake maalumu kwa kipindi hiki ligi imesimama, mwalimu hataki masihara anataka kuona kila mchezaji akifanya mazoezi na kuonyesha kile ambacho amembiwa kufanya lakini pia wanatakiwa kuingia kumbi za mazoezi Gym kuweka miili yao sawa,” alisema Ahmed.

Hata hivyo, Ahmed alisema wachezaji ambao hawajaitwa katika kikosi cha timu ya Timu zao za Taifa wamepewa mapumziko hadi Desemba 28, mwaka huu ndio watarejea  kambini.

Ofisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe alisema kuwa kocha wao, Pedro Goncalves amewapa programu maalumu wachezaji wake kuhakikisha wakiwa katika mapumziko hawatakiwa kubweteka.

Alisema kila mchezaji amepewa mazoezi ambayo anatakiwa kufanya lengo likiwa ni kurejea wakiwa imara na bora zaidi ya walivyokuwa mwanzo.

“Tunajua kutakuwa na mapumziko ya muda mrefu, lakini mwalimu wetu Pedro amempa kila mchezaji programu maalumu ya kufanya katika kipindi hiki cha mapumziko, mwalimu amesisitiza kila mmoja kufanya kile ambacho amemuagiza na atayepuuza basi adhabu kali itamkumba,” alisema.

Kamwe aliongeza kuwa timu imepewa mapumziko hadi Desemba 15, mwaka huu ambapo wataanza mazoezi hadi Desemba 20 na Desemba 21 watapumzika tena hadi Desemba 28 na Desemba 29, mwaka huu wachezaji wote wanatakiwa kurejea kambini,” alisema Kamwe.

Naye Meneja wa Habari na Mawasiliano Azam FC, Zacharia Thabit ‘Zaka za Kazi’, alisema wachezaji wa timu yao wamepewa mapumziko hadi Desemba 22 mwaka huu ndio wataingia kambini kwa ajili ya programu zinazofuatia.

Alisema kuwa pamoja na mapumziko hayo lakini mwalimu Florent Ibenge amewapa mazoezi maalumu wachezaji wake  kujiweka sawa.

“Timu ipo mapumziko, lakini mwalimu wetu amewapa mazoezi maalumu wachezaji wake ambapo kwa siku watafanya mazoezi asubuhi na mchana ili kuhakikisha wanarejea wakiwa fiti na bora kwa ajili ya kuendeleza mapambano,” alisema Zaka.

Previous Post

MCHUJO MKALI  KOCHA SIMBA

Next Post

BONDIA MWAKYEMBE KUTOA ZAWADI YA KRISMASI

Next Post
BONDIA MWAKYEMBE KUTOA ZAWADI YA KRISMASI

BONDIA MWAKYEMBE KUTOA ZAWADI YA KRISMASI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

 WAZIRI GWAJIMA AANIKA MIZIZI YA UKATILI NCHINI

 WAZIRI GWAJIMA AANIKA MIZIZI YA UKATILI NCHINI

4 months ago
UNDANI WA REKODI YA MSUVA AFCON

UNDANI WA REKODI YA MSUVA AFCON

4 months ago

Popular News

  • TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VYALENGA KUIJENGA JAMII KIUCHUMI NA KIROHO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUVUMILIANA MUHIMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI SANGU ABAINISHA HIFADHI SKIMU INAVYOENDA KUBADILI MAISHA YA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?