• ePaper
Thursday, April 30, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

MCHUJO MKALI  KOCHA SIMBA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 11, 2025
in Burudani, Michezo
0
MCHUJO MKALI  KOCHA SIMBA

SIMBASC

0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

BODI ya Wakurugenzi wa klabu ya  Simba,  imekaa kikao kizito kufanya mchujo wa maombi ya makocha zaidi ya 100 wanaotaka nafasi hiyo.

Simba inasaka kocha mpya baada ya kumtema Dimitar Pantev aliyetambulishwa kama meneja akiitumikia kwa siku 61 baada ya kuwa na mwenendo mbaya ndani ya kikosi chao.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Meneja wa Habari na Mawasiliano Simba, Ahmed Ally alisema kuwa mchakato wa kusaka kocha mpya unaendelea na hivi sasa viongozi wanachakata maombi yaliyotumwa.

“Kuna maombi mengi  ya makocha kutoka nchi mbalimbali wakitaka kuifundishia Simba, lakini viongozi watahakikisha wanachagua kocha mwenye CV nzuri kuweza kuifundishia Simba.

“Hadi sasa tumepokea maombi zaidi ya 100 hivyo kazi kubwa inaendelea ya kuchakata maombi hayo, tupate kocha bora mwenye viwango vya kimataifa,” alisema.

Ahmed aliongeza kuwa kwa  kipindi hiki, wanahitaji kocha bora na imara ambaye ataisaidia timu yao kuweza kufikia malengo waliojiwekea katika Ligi Kuu Tanzania Bara na michuano ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika.

Alifafanua kuwa hali hiyo, inatokana na timu yao kuwa na ngumu kwa kipindi hiki hivyo mashabiki na wapenzi wa timu yao wanatakiwa kutulia wakati timu inatafuta suluhisho litalokuwa bora.

Hata hivyo, taarifa za ndani zinaeleza kuwa Simba imeanza mazungumzo na makocha Antonio Casano Cantos kutoka Hispania akiwa na sifa za kufundisha soka  nchi za Angola na Morocco.

Pia,  kupitia timu za Petro Atletico na Moghreb Atletico Tetouan na Steve Barker wa Stellenbosch ya Afrika Kusini.

Lakini Meneja wa Habari na Mawasiliano Simba, Ahmed Ally alishindwa kueleza kwa undani juu ya kuwepo habari hizo.

Wakati huo huo, dirisha dogo la usajili linatarajiwa kufunguliwa Januari Mosi, mwakani na Simba imepanga kusikilizia mapendekezo ya kocha mpya au Seleman Matola kama atapenya kisha kujiweka tayari kwa mechi nne za Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya makundi ikiwemo michezo miwili ua nje na ndani dhidi ya Esperance ya Tunisia.

Simba ipo Kundi D, mbali na Esperance pia zipo Stade Malien ya Mali na Petro Atletico ya Angola ikisaka nafasi ya kucheza robo fainali kwa mara ya saba tangu 2018-2019.

Previous Post

MOGELLA, MTEMI WAMKINGIA KIFUA GAMONDI KIKOSI STARS

Next Post

MASTAA YANGA, SIMBA WAPEWA PROGRAMU ZA MAZOEZI

Next Post
MASTAA YANGA, SIMBA WAPEWA PROGRAMU ZA MAZOEZI

MASTAA YANGA, SIMBA WAPEWA PROGRAMU ZA MAZOEZI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

TRA INAVYOIMARISHA USHIRIKIANO NA WAFANYABIASHARA KUKUZA UCHUMI

TRA INAVYOIMARISHA USHIRIKIANO NA WAFANYABIASHARA KUKUZA UCHUMI

4 months ago
HOFU YA WANAUME KUOA WANAWAKE WAREMBO IKO HAPA

HOFU YA WANAUME KUOA WANAWAKE WAREMBO IKO HAPA

4 months ago

Popular News

  • TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VYALENGA KUIJENGA JAMII KIUCHUMI NA KIROHO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUVUMILIANA MUHIMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI SANGU ABAINISHA HIFADHI SKIMU INAVYOENDA KUBADILI MAISHA YA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?